Kwa picha: Ufahamu kuhusu Ulimwengu

Kwa picha: Ufahamu kuhusu Ulimwengu

Vyakula vya GMO.

Vyakula hivi kwa kitaalamu vinaitwa ‘biotechfoods’. Kwa mara ya kwanza vyakula hivi viliingizwa sokoni mwaka 1996 vikijumuisha mazao ya maharage,mchele,mafuta yambegu za pamba,mahindi na mihogo. Matunda ya GMO yanajumuisha machungwa,malimao,miwa na mananasi,tikiti maji. Vyakula pamoja na matunda ya GMO kwa harakaharaka ni vigumu kuyabaini bali yana sifa kuu ya kutokuwa na ladha ya asili.

Kwa kiasi kikubwa mseto wa GMO unapatikana katika mafuta ya kula tunayozalisha ili kurandana na kasi ya ushindani wa bidhaa hii sokoni. Mafuta ya kula yetu yanachanganya kitu kinachoitwa omega-3-fatty acids.

Omega-3-fatty acids: hii ni bidhaa ya mafuta ambayo ilianzwa kuzalishwa maabara mwaka 2006 ambapo wanabaiteknolojia waling’amua DNA za minyoo ijulikanayo kitaalam round worms na kuichakata kwa mbinu za uhandisi wa genetikia na kuitia ndani ya mwili wa nguruwe na hatimaye kuzalisha mafuta ya kula mengi kwa kasi kubwa zaidi kupitia nguruwe. Aidha mafuta haya yameweza pia kuchakatwa na kuweza kuzalishwa kupitia samaki,mayai na nyama.

Athari za kiafya za Omega-3-fatty acids:imeelezwa katika majarida mbalimbali kama vile jarida la muungano wa madktari wa Marekani(journal of the Americanmedical association) kuwa Omega-3-fattyacids ilibuniwa kwa malengo ya kutibu magonjwa mbalimbali yanayomuandama mwanadamu. Lakini kinyume chake mafuta haya yamemuweka mwanaadamu kikaangoni kupitia maradhi sugu yakijumuisha
1. magonjwa ya kansa
2. magonjwa ya moyo na kiharusi (stroku
3. TB
4. wendawazimu (psychiatricdisorders)

5. kububujikwa sana damu za hedhi na
6. kisukari
7. kudhoofisha mwili wa mwanadamu na kuufanya ushambuliwe kirahisi na magonjwa ; hii imeripotiwa zaidi katika jarida la microbial ecology in health and disease, kwamba wakati wa usafirishaji wa DNA baina ya wanyama kunaweza kupitisha vimelea vya bakteria
8.maambukizi ya HIV iwapo mnyama aliyefanyiwa ung’amuziwa DNA amebeba vimelea vya virusi vya UKIMWI..

Mazao ya GMO

Takriban kati ya mwaka 1996 na 2011,jumla ya sehemu ya ardhi iliyolimwa mazao ya ya GMO ni kilometa za mraba 17,000 ambazo ni sawa na ekari 42,000. halikadhalika hadi kuingia mwaka 2012 kumekuwa na ongezeko kubwa la sehemu ya ardhi inayolimwa mazao ya GMO amabayo ni sawa na kilometa za mraba 1,600,000 hii ndio kusema ni ekari milioni 395.

Mazao haya kwa mara kwanza yalizalishwa nchi za Marekani ya kusini na kwa kadiri yalivyopata soko kubwa zaidi yakasamabaa pande nyingine za dunia hasa katika nchi zinazoendelea ikiwemo Afrika ya kusini,Bukinafaso,Tanzania na kadhalika. Katika nchi ya Marekani mnamo mwaka 2010 asilimia 93 ya zao la maharage,aslimia 93 ya pamba na asilimia 95 ya miwa ya sukari ilipatikana kupitia GMO .

Aidha tecknolojia ya GMO katika nchi zinazoendelea imeweza kuzalisha na kuingiza sokoni mazao ya viazi vitamu(genetically modified sweet potato), mchele wa rangi ya dhahabu na unga wa ngano.
 
Hawa watu ndio hatar ktk uzalishaji wa mazao ya GMO, MONSTER SANTO kifupi (MONSANTO)
 
kama ni kweli hizi mbegu zina madhara makubwa kiasi hicho basi hapa duniani si salama tena.

masikititiko yangu utakuta serikali inafahamu vyema athari ya vitu vya maabara lakini wameshinda kulinda wananchi wake na kizazi kijacho.

kuna wakati fulani alikuwepo nabii wa kanisa la siloam hapa Tz kabla ya kufariki aliwahi kusema alitafuta mbegu za asili za mahindi karibu nchi nzima alikosa na alikuja kuzipata singida huko vijijini.
alisema yule malaika alikua akitaka kumpindua Mungu kabla ajafanikiwa alipinduliwa yeye, ameendelea kuharibu uumbaji wa Mungu kila leo ili ausimamishe ufalme wake lakini hangefanikiwa kwakua yeye alikuja ili amuangamize huyo malaika kwa jina akiitwa kerubi. lakini bahati isio njema nabii aliwahi kufa lakini ilisemekana alimuua huyo kiumbea ambae ni shetani pia. Mungu amlaze kwema.
 
Kuna Maelfu ya sayari nyingine katika ulimwengu,tuna sayari nane katika mfumo wa jua ingawa nje ya mfumo wa jua kuna sayari nyingi sana,kuna sayari 1800 zilizothibitishwa na 3000 zinasubr kudhibitishwa
 
Katika Anga za juu ngozi humomonyoka hali hyo husababishwa na uwepo wa micro gravity,katika anga za juu hakuna mashine za kufulia wanasayansi hutakiwi kuvaa Nguo moja kwa wiki kadhaa,kwan kila kitu huelea
 
Ukubwa wa jua ni sawa na dunia Mara milioni moja
 
Unaweza kulia ukiwa anga za juu ila machozi hayaendi chini hubaki hapo hapo!
 
Katika kituo cha kimataifa cha anga ISS Nguo chafu na tishu hutumika kukuza!
 
Ukiwa katika anga za juu metali mbili hujivuta pamoja na kitu kimoja,ukizigusisha ni kama unafanya welding zinaganda pamoja,wanapenda kuiita hyo hali a cold welding
 
Hali mbaya ya hewa
Wakati mwingine katika sehemu kadhaa wa kadhaa zilizopo ufukweni tumekuwa tukishuhudia hali mbaya ya hewa ingawa dunia ni sehemu ya kustaajabisha yenye hali nzuri kabixa ya hewa kwa viumbe vyake,
Katika sayari ya Jupiter kuna pepo Kali na vimbunga
Katika Venus na mars kunatokea mabadiliko makubwa sana ya hali ya hewa ndani ya Sikh mfano kuna hali ya joto linazolidi maji yanayochemka kwa Mara tano na zaidi,katika Uranus na Saturn pia kuna pepo Kali zivumazo,ila katika Neptune upepo hasafiri kwa kasi kubwa ya 1600 mph!
 
Wanasayansi wengi wamekuwa wakielezea ulimwengu wetu kuwa ni dude kubwa mno lisilo kuwa na mwisho(means the universe size is almost infinity)
Leo hebu tuchambue na kuangalia ukubwa wa dunia yetu
Kabla ya kuendelea naomba kuelezea kidogo kuhusu Galaxy, huu ni mkusanyiko wa nyota,sayari na vyote vilivyoko katika ukanda husika,Galaxy hutofautiana sana kwa ukubwa ila ya kati inakadiriwa kuwa na nyota bilioni 400 na mabilioni ya sayari,Galaxy yetu inaitwa milky way ambayo ina mabilioni ya sayari na na nyota,hebu sasa twende kwa picha
1.Hii ni dunia yetu,sehemu tunamoishi
e7986b4df1a6dcfd7bd4dbac927c3958.jpg

2:Huu ni mfumo wetu wa jua,solar system
c9cc15d9ceacb485408d64d38227c771.jpg

3.Huu ni umbali kutoka duniani mpaka mwezini
6648e54ecb397ba1b7796197f9719faf.jpg

katika umbali Huu wa mwezini mpaka duniani waweza Panga sayari Tisa na zikaenea!
b9d1c30e8299e0fe4170436c29090c2e.jpg

4.Hii ni sayari ya Jupiter ni kubwa sana
0b66cffcacac5cd083e22849f048212a.jpg

Hicho kidoti kidogo amerika kaskazini
a4af9f3b32530281e4184ea8d20c8193.jpg

5.Huu ni mwonekano wa Saturn ukiweka dunia katika ringi zake,mwonekano wa dunia sita katika ringi zake
d363ce0def4d123c246389f455408808.jpg

6.Hebu tulinganishe Jua na dunia,
Jua 1=dunia milioni 1!!!,yaani dunia kwenye jua inaingia mara milioni 1
b18457c5d884695615d8095dcc497ccb.jpg

7.Hii ni picha maarufu ya dunia iliyochukuliwa kutoka maili bilioni 4 ,hicho kidoti kidogo ni dunia
5d5ee427832ee423816e3dbd1bc9772d.jpg

8.Tuliangalia kuwa katika jua dunia huingia Mara milioni moja
fcb3df21189b9d9ea6926a457d1042a6.jpg


Hebu tulinganishe jua na nyota zingine
9.Kuna nyota inaitwa Articus ni Mara 16,000 ya jua,hicho kidoti kidogo ni jua
64b433d6d1d3b05c1731f809a5063a62.jpg

10:Kuna nyota inaitwa Alpha scropti ni kubwa Mara 690 milioni kuliko jua,hicho kidoti kidogo ni jua
a2b368b17cdfd5177a52ac4d12436df6.jpg

11.Kuna nyota inaitwa VY Canis major ni kubwa Mara bilioni 2.9
Kuliko jua,hapo usisahau kulinganisha jua na dunia!
fef7532d17719d0420b80a1a605613da.jpg

Hicho kidoti kidogo cha mwisho ni jua
12.Hebu tuangalia galaxy yetu,ni ukanda wenye nyota zaidi ya bilioni 400 pamoja na sayari zake
Ndani ya sekunde moja mwanga huzunguka dunia Mara saba na nusu,ukienda kwa speed hiyo ulitakuchukua miaka 100,000 kutoka katika ukanda wetu(milky way Galaxy)
13:milky way Galaxy ni kubwa sana,na hyo doti ya njano ni nyota tyu ambazo unauwezo wa kuziona kati ya mabilioni ya nyota
cb99f170004423544bae1d96e9f873eb.jpg


Najua umeshawishika kuona milky way Galaxy(ukanda wetu wa nyota ni mkubwa sana lakini nikuambia kuwa ni kidude kidogo sana ukilinganishwa na dubwasha kubwa la Galaxy liitwalo 1C1011,galaxy Hii ukienda na speed ya mwanga ambayo nilikueleza kuwa itakuchukua miaka 6,000,000
2e1681e59adcd87b3035e72beebb87d0.jpg

Milky way ni hicho kidoti kidogo kulinganisha na 1C1011 Galaxy

14.Hebu tuchukue Hubble telescope, picha Hii ina mabilioni ya Galaxy na kila Galaxy ina mabilioni ya nyota na sayari mabilioni pia na kila doti unayoona hapo ni galaxy nzima
270ca90c1ef5a2a0ab539407f434105a.jpg



Oooh umechoka[emoji2] [emoji2] [emoji2] [emoji2],subiri
Hii ni dunia
06314a6385d6488cc978c347e1c4ca27.jpg

Tukizoom zaidi Hii ni solar system
07554949025788fdc0f74b2d2fe6e3a9.jpg

Tukizoom tena tunaona majirani katika solar system katika picha nzima ya galaxy
f6bb8c4146cf6f0f0ef7117edcc249d1.jpg

Tukizoom tunaona milky way galaxy ni hicho kidoti!
d1d08b6ad4f60041a5ab3166a3e29af2.jpg

Itaendelea...
Tupe maelezo ya kutosha kuhusu hicho kidoti
 
mada imeenda mbali zaidi mpaka uharibivu wa mazingira na magonjwa.
lakini kule kwenye ulimwengu, galaxy, na dunia bado kuna mengi ya kujiuliza.

kama ilivyosemekana kwamba mwanga ndio husafiri kwa mwendo kasi zaidi kuliko chochote, na kama ilivyosemekana kwamba ziko galaxy nyingi katika ulimwengu na zinagarimu miaka bilion nyingi kuzifikia tena kwa kasi ya mwendo wa mwanga!
na hapo tunaona bado darubini hazija weza kuona mwisho wa ulimwengu, au ilipo mbingu makao makuu ya Mwenyezi Mungu.

sasa, kama kutoka katika galaxy ya kwetu ambayo pia ni ndogo kuliko nyingine inagarimu miaka milion kadhaa, je huko kwa Mungu ambako kuna binadamu waliwahi kusema wamefika mbingu ya 3 kati ya 7 walitumia muda kiasi gani?
kwamaana nataka kuamini mbingu ya kwanza mpaka hio ya saba ni nje ya ulimwengu.

Au Bwana Yesu alipo paa mbinguni kam ya semavyo maandiko huenda mpaka leo hajafika!!
tuchukue mwendo wake ni mara 100 ya kasi ya mwanga bado inagarimu mamilioni ya miaka!

mtazamo wangu kuna sehemu hatuambiwi ukweli kati ya sayansi na dini.
lakini Mungu atukuzwe maana hakuna kama yeye.
Suala la kina yesu kupaishwa au ile mitume kwenda mpaka mbingu ya 7 huo ni uwezo wa mungu c wa kibinadamu na hakuna mwanasayansi yeyote anaeza sibitisha kwanza hawaamini mungu kama yuko...na kingine sie tumepewa akili ya kuishi kwenye mazingira yetu
 
elimu ya science ya ulimwengu ni elimu ya kusadikika haina ukweli wowote wala haiingii akilini kama tutakuwa na uwezo wa kufikiri,binadamu hatuwezi kuishi kwenye dunia yenye shepu ya chungwa,na kama ingekuwa kweli tungekuwa tunaweza kuishi kwenye milima mikubwa kwa kuganda pembezoni mwa milima bila ya kuanguka.

dunia haiwezi kuwa duara na maji kuganda nje ya dongo la dunia na kisha iwe inaruka angani kwa speed na masafa tunayoambiwa hii haiwezekani kabisa,katika uhalisi wa maji hayawezi kupinda kufata umbo la nje la kitu chochote,maji popote yalipo ni lazima yawe level hio ndio sifa kuu ya maji,na ndio mana tunatumia lever za maji kujengea majumba ili kupata usawa wa nyumba

jua na mwezi ni vitu vipo sawa sawa na umbali wake kutoka ardhini ni sawa sawa kama tunavyoviona,pia kama utaangalia jua na mwezi utakuta vipo ndani ya wingu la blue havipo umbali wanaosema,pia mwezi hauna ardhi ya watu kwenda kutua,tukiwa hapa tunauona kuwa mwezi ni kitu kinapitisha mwangaza(transparent),utazame mwezi mchana utaliona wingu la buluu kwenye mwezi na usiku utaona wingu jeusi kupitia kwenye mwezi.

tumefundishwa gravity ndio inayotuzuia tusipeperushwe na speed ya dunia hiki ni kichekesho kikubwa,kwanini gravity haiwezi kuzuia mabofu na mifuko ya plastic na ni vyepesi sana, kwa ufupi hakuna gravity ni vitu vizito vinabaki ardhini na vyepesi vinakwenda angani

hatuwezi kufahamu kila kitu lakini upo uwezekano kuwa ukubwa wa dunia ndio hauna mwisho(infinity) wala sio duara na haizunguki wala kuruka,uhalisi ni kama tunavyoona kila siku dunia ipo tuli imetulia.
Hapo kwenye force of gravity kasome tena..
 
Tupe maelezo ya kutosha kuhusu hicho kidoti
Hicho kidoti ni Galaxy yetu Yaani ukanda wetu wa nyota ambao una sayari mabilioni na nyota mabilioni

Na kanda kama hizi zenye mabilioni ya nyota na sayari katika ulimwengu wote zinakadiriwa ziko trillioni 2
 
Back
Top Bottom