Kiboko ya Jiwe
JF-Expert Member
- Apr 7, 2020
- 12,702
- 36,132
Sijaiona picha ya sehemu za nyuma za gari hii. Ikiwa imeharibika hapo tu panapoonekana kwenye picha serikali itatumia zaidi ya milioni 50 kutengeneza gari hii.
Gari itakaguliwa na TEMESA, serikali italipa gharama za ukaguzi, kisha TEMESA watatoa tenda kwenye garage binafsi kama vile KINAI, ADAM MOTORS, NDUVINI, CHUNGA, KWADU, n.k maana TEMESA haiwezi kukubali kubeba mzigo huu. Ili pesa ipigwe vizuri inabidi utoe tenda then ukale na uliyempa tenda.
Garage zilizothibitika kukidhi viwango ziko nyingi, ni zaidi ya 20.
Mwenye garage ataweka dau lake na watu wa TEMESA manager, fundi mkuu n.k watataka fungu lao pia.
Kwa ufupi hii ni neema kwa baadhi ya watu.
Hivyo serikali itatumia zaidi ya milioni 50 hapo kulirudisha hili gari katika hali yake.