'Magari ya Makonda' yakwama kukarabatiwa, mwenyewe agoma kutoa ushirikiano

VUTA-NKUVUTE

JF-Expert Member
Nov 25, 2010
6,135
17,802
Unakaribia mwezi mmoja sasa tangu msafara Ndugu Paul Makonda, Katibu wa Itikadi, Uenezi na Mafunzo wa CCM Taifa, upate ajali kule Sululu, Masasi mkoani Mtwara. Ajali hiyo iliyohusisha magari yapatayo 10, ilitokea tarehe 11 mwezi uliopita na kusababisha uharibifu wa magari kadhaa yakiwamo ya serikali.

Katika kile kinachosemwa kama kiburi na jeuri ya kimadaraka chamani, Makonda amegoma kutoa ushirikiano kufanikisha marekebisho ya magari hayo yaliyohifadhiwa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA). Ushikirikiano utakiwao ni ripoti ya mkuu wa msafara juu ya ajali hiyo ambayo hadi sasa haijatolewa.

Makonda amewaambia maafisa wa kichama na kiserikali kuwa wakitaka kujua lolote wakakiulize chama kwakuwa ndicho kilichoruhusu na kuwezesha ziara yake mikoani-ikiwemo hiyo ailiyokuwa akitokea mkoani Ruvuma. Mkwamo wa matengenezo hasa unazikumba gari za serikali ambazo huhitaji ripoti kamilifu ili ziweze kutengenezwa.

Idara ambazo zinamiliki magari hayo ya serikali zilizopata ajali hiyo zinawataka maafisa wake na madereva wao waseme kwanini walikuwepo kwenye msafara huo wa kichama; hoja ambayo inapaswa kujibiwa na Makonda aliyegoma kufanya hivyo. Ripoti haijatolewa na magari hayajashughulikiwa.

Makonda, chama ni nani ili akaulizwe hata ajali yako ya Masasi?

Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa Sombetini, Arusha)
 
Unataka kutuambia kuna mgogoro wa kiutendaji kati ya CCM na serikali yake?

Kwani ni mara ya kwanza magari ya serikali kutumika kwenye shughuli za chama chenu?

Kama sio mara ya kwanza, kwanini Makonda apate kigugumizi kuwajibu hao wanaomuuliza hayo maswali?

Inawezekana vipi vigogo wa serikalini waingie kwenye hayo magari wazunguke na Makonda, kisha baada ya ajali kutokea waanze kumuuliza Makonda kwanini alitumia hayo magari ya serikali?! wao kwanini walizunguka nae?

Hayo magari yameachwa hapo TEMESA kwa sababu maalum, wanatafuta gap waje kutupiga mbele ya safari, wao watachota pesa za umma wakanunue magari mengine mapya muda wao ukifika.

Sent from my SM-G900H using JamiiForums mobile app
 
Mleta mada muongo chama hakiwezi jieleza kwa sababu ya magari ya serikali wale waliongozana kwenda kwenye
mkutano kusikiliza kero za wananchi na kuzipa majibu

Kiongozi wa serikali kusikiliza.kero za wananchi ni moja ya majukumu yake
 
Unataka kutuambia kuna mgogoro wa kiutendaji kati ya CCM na serikali yake?

Kwani ni mara ya kwanza magari ya serikali kutumika kwenye shughuli za chama chenu?

Kama sio mara ya kwanza, kwanini Makonda apate kigugumizi kuwajibu hao wanaomuuliza hayo maswali?

Hayo magari yameachwa hapo TEMESA kwa sababu maalum, wanatafuta gap waje kutupiga mbele ya safari, wao watachota pesa za umma wakanunue magari mengine mapya muda wao ukifika.

Sent from my SM-G900H using JamiiForums mobile app
Kwani hao wanaouliza hawajui kama gari zilikuwa kwenye msafara wa karibu mwenezi
 
Mleta mada muongo chama hakiwezi jieleza kwa sababu ya magari ya serikali wale waliongozana kwenda kwenye
mkutano kusikiliza kero za wananchi na kuzipa majibu

Kiongozi wa serikali kusikiliza.kero za wananchi ni moja ya majukumu yake
Weka facts basi za kusindikiza hoja yako
 
Unataka kutuambia kuna mgogoro wa kiutendaji kati ya CCM na serikali yake?

Kwani ni mara ya kwanza magari ya serikali kutumika kwenye shughuli za chama chenu?

Kama sio mara ya kwanza, kwanini Makonda apate kigugumizi kuwajibu hao wanaomuuliza hayo maswali?

Hayo magari yameachwa hapo TEMESA kwa sababu maalum, wanatafuta gap waje kutupiga mbele ya safari, wao watachota pesa za umma wakanunue magari mengine mapya muda wao ukifika.

Sent from my SM-G900H using JamiiForums mobile app
Na hapo ndio utajua uongo wa mtoa mada yani anajaribu kutuambia kuwa magari hayo yalikwenda kwenye msafara wa Makonda bila ruhusa? Huu ndio uongo mkubwa! Yani CCM na serikali walumbane kukarabati magari?
Yani hapa ni sawa kutuambia CCM na CCM wana lumbana!

Kiufupi huu ni uongo kwani CCM ni wale wale na tamesa hawana uwezo wa kupingana na CCM maana wanalipwa na CCM…
Mtoa mada huwa hampendi Makonda sema sasa ndio yupo pale na sasa ana jifariji……
 
Nadhani mleta mada ni mbumbumbu wa mambo mengi sana, Ajali aliyepata ni dereva unadanganya watu eti maelezo yanatakiwa kutolewa na mkuu wa msafara, Huu ni ulongo wa hali ya juu. Hivi ni nani anayejua chanzo cha ajali zaidi ya dereva aliyepatwa na ajali husika?

Ulongo mwingine ni kuhusu kukwama kwa matengenezo ya gari etuli kwa sababu idara za Serikali zinahoji kwanini magari husika yalikuwa kwenye ziara ya Makonda!!

Ifahamike kuwa ziara ya kiongozi yeyote wa CCM ni ziara ya kukagua utendaji wa Chama na Serikali, kwa upande wa Serikali wanaokaguliwa ni Watumishi wa Serikali wanaotekeleza Ilani ya Chama kilichoko madarakani, sasa kwa akili yako ulitarajia kwenye msafara wasiwepo wanaokaguliwa? Hapa huna hoja zaidi ya chuki binafsi kwa Makonda. Bahati mbaya sana unakuja kuposti utumbo kwenye ukrasa wa Jamiiforum sehemu ambayo tunaamini wamejaa intellectuals jitahidi ukumbi huu uwe unauposti Facebook, TikTok au Instagram kule.
 
Na hapo ndio utajua uongo wa mtoa mada yani anajaribu kutuambia kuwa magari hayo yalikwenda kwenye msafara wa Makonda bila ruhusa? Huu ndio uongo mkubwa! Yani CCM na serikali walumbane kukarabati magari?
Yani hapa ni sawa kutuambia CCM na CCM wana lumbana!

Kiufupi huu ni uongo kwani CCM ni wale wale na tamesa hawana uwezo wa kupingana na CCM maana wanalipwa na CCM…
Mtoa mada huwa hampendi Makonda sema sasa ndio yupo pale na sasa ana jifariji……
Huwa yanaenda lakini yanaporudi bila shida hakuna tatizo.

Sasa yameharibika. Hapo kila mtu anaanz akujitoa.
 
Nadhani mleta mada ni mbumbumbu wa mambo mengi sana, Ajali aliyepata ni dereva unadanganya watu eti maelezo yanatakiwa kutolewa na mkuu wa msafara, Huu ni ulongo wa hali ya juu. Hivi ni nani anayejua chanzo cha ajali zaidi ya dereva aliyepatwa na ajali husika?

Ulongo mwingine ni kuhusu kukwama kwa matengenezo ya gari etuli kwa sababu idara za Serikali zinahoji kwanini magari husika yalikuwa kwenye ziara ya Makonda!!

Ifahamike kuwa ziara ya kiongozi yeyote wa CCM ni ziara ya kukagua utendaji wa Chama na Serikali, kwa upande wa Serikali wanaokaguliwa ni Watumishi wa Serikali wanaotekeleza Ilani ya Chama kilichoko madarakani, sasa kwa akili yako ulitarajia kwenye msafara wasiwepo wanaokaguliwa? Hapa huna hoja zaidi ya chuki binafsi kwa Makonda. Bahati mbaya sana unakuja kuposti utumbo kwenye ukrasa wa Jamiiforum sehemu ambayo tunaamini wamejaa intellectuals jitahidi ukumbi huu uwe unauposti Facebook, TikTok au Instagram kule.
Mtoa mada alijua kuna wajinga wa facebook jf
 
Back
Top Bottom