Miss Zomboko
JF-Expert Member
- May 18, 2014
- 4,502
- 9,280
Ukaguzi wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) umebaini jumla ya Magari ya Serikali 547 yalikuwa yameegeshwa kwenye Karakana za Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) na katika baadhi ya Taasisi za Serikali
Aidha, baadhi ya magari yaliyotelekezwa hayakuwa kwenye mipango ya matengenezo au ya uondoshwaji. Ukaguzi ulibaini kuwa asilimia (43%) ya magari yalikuwa yameegeshwa kwenye Karakana za TEMESA kwa zaidi ya miaka mitatu (3) kutokana na sababu mbalimbali kama vile ajali, matengenezo, maegesho, na kusubiri vibali vya uondoshaji.
Uwepo wa magari mengi ya serikali yaliyoegeshwa kwa muda mrefu bila kutumika ulitokana na baadhi ya Taasisi kutofanya uhakiki wa hali za mali zake ili kufahamu kama ziondolewe au zitengenezwe. Kuwepo kwa magari mabovu ya Serikali ambayo yameegeshwa na hayatumiki kwa muda mrefu bila kuondoshwa kulikuwa na athari zifuatazo:-
a) Magari kuchakaa na kuharibika zaidi na kwa kasi hali inayopelekea kupungua kwa thamani ya magari haya pale ambapo Serikali itaamua kuyaondoa;
b) Madhumuni ya ununuzi wa magari hayafikiwi ipasavyo kwa sababu magari hayafanyi kazi kulingana na madhumuni yaliyokusudiwa;
c) Kuongezeka kwa gharama za matengenezo kutokana na uchakavu wa magari mabovu ambayo yamehifadhiwa na hayatumiki kwa muda mrefu; na
d) Upotevu wa rasilimali-fedha za umma.
Aidha, baadhi ya magari yaliyotelekezwa hayakuwa kwenye mipango ya matengenezo au ya uondoshwaji. Ukaguzi ulibaini kuwa asilimia (43%) ya magari yalikuwa yameegeshwa kwenye Karakana za TEMESA kwa zaidi ya miaka mitatu (3) kutokana na sababu mbalimbali kama vile ajali, matengenezo, maegesho, na kusubiri vibali vya uondoshaji.
Uwepo wa magari mengi ya serikali yaliyoegeshwa kwa muda mrefu bila kutumika ulitokana na baadhi ya Taasisi kutofanya uhakiki wa hali za mali zake ili kufahamu kama ziondolewe au zitengenezwe. Kuwepo kwa magari mabovu ya Serikali ambayo yameegeshwa na hayatumiki kwa muda mrefu bila kuondoshwa kulikuwa na athari zifuatazo:-
a) Magari kuchakaa na kuharibika zaidi na kwa kasi hali inayopelekea kupungua kwa thamani ya magari haya pale ambapo Serikali itaamua kuyaondoa;
b) Madhumuni ya ununuzi wa magari hayafikiwi ipasavyo kwa sababu magari hayafanyi kazi kulingana na madhumuni yaliyokusudiwa;
c) Kuongezeka kwa gharama za matengenezo kutokana na uchakavu wa magari mabovu ambayo yamehifadhiwa na hayatumiki kwa muda mrefu; na
d) Upotevu wa rasilimali-fedha za umma.