Ndugu Mkandara,
Hivi watu kuhamia sehemu kunaweza kujulikana tu watu wakiulizwa dini zao? Watoto wakiwa wengi serikali itapanga maendeleo kama huduma za afya na uzazi, mipango ya badae ya kujenga shule kulingana na idadi hiyo. Je, ikipata wapagani ni wengi zaidi itapanga mipango ya kuwapelekea misikiti na makanisa?
Ukweli ni kuwa popote walipo ndugu zetu waislamu watadai kufanyiwa vitu ambavo zinapaswa kufanywa na dini badala ya serikali hii ni kwa kuwa secularism kwa waislamu ni msamiati. Badala ya kutenga huduma au mambo yao na serikali watataka huduma nyingi zitoke serikalini au ziwe katika mfumo wa serikali. Huu mfumo unawezekana tu ambapo watu au waislamu ni wengi hivyo akili zao ziko sawa kidini na njia hiyo ya kuendesha serikali. Ni mfumo ambao ni wa ajabu kabisa lakini kwao uko sahihi. Nafikiri kwa idadi yoyote ambayo wangepata kwenye sensa wangeanza kudai haki za kuhudumiwa na serikali kwa huduma ambazo zinapaswa kuwa za kidini kama mahakama ya kadhi.
Mimi siamini waislamu ni wengi nchi hii hata nikichukua ramani ya Tanzania niiweke mkononi mwangu halafu nianze kuanisha maeneo ambako kuna waislamu. Ndio si kidogo lakini ni sehemu ndogo tu kulinganisha na maeneo walipotapakaa wakristo. Huko kwetu ukienda watu ambao hawajatembelea mjini hawajui kuna dini inaitwa uislamu labda kwa sasa kwa kuwa mawasiliano yapo kwa wingi. Nilitamani serikali ifanye hiyo sensa ili waislamu wajue ukweli kuwa ni wachache. Lakini najua hilo lisingeishia hapo. Swali; Wangekubali ni wachache? Wasingeanzisha malumbano mengine?
Na kwasababu Mkandara hujajibu swali la Jmushi1. Mimi naliuliza tena hilo swali; Serikali ikishajua waislamu, wakristo au wapagani ni wangepi inakuwaje? Inasaidia nini serikali? Inatusaidia nini watanzania katika kusukuma gurudumu la maendeleo?
Bado akili yako inafikiri kwamba kazi ya serikali ni kugawa vipande vya mkate kulingana na hesabu ya watu wake na ndio ndio maana tunahitaji sensda ya kuhesabu vichwa vya watu.. Tatizo lako bado huelewi nini umuhimu wa sensa ktk nchi ya Kibepari na zinafanyika kila nchi wakijua hesabu ya WATU wote kwa matabaka yao waishio nchi zao na sii kuhesabiwa kama machungwa.
Nitarudia kusema serikali haipeleki maendeleleo kwa wananchi bali inaanda mipango ya maendeleo kwa WATU wake wenye tofauti zao kulingana na mfumo uliopo (Kibepari). Na kibaya zaidi mnachanganya sana kati ya kupelekea maendeleo kwa wananchi jambo ambalo lilikuwa likifanywa wakati wa Nyerere na Ujamaa na Kujitegemea tofauti na sasa ambapo ni kazi ya usambazaji maendeleo ni jukumu la wananchi (WATU) ndio wanaofungua miradi ya maendeleo kwa jamii hizo kwa kuwezeshwa (polcies) na serikali yao.
Leo hii nenda Canada, marekani au UK waulize kuna watanzanioa wangapi waiajua hesabu. Kuna waislaam wangai wanajua, kuna Jews wangapi, Shikh, na hata Baniani wanajua na jamii zenyewe wamewezeshwa kujipenyeza ktk ujenzi wa taifa hilo bila kukwazwa na sera au ilani. Kw akuelewa umuhim wa jamii hizo viongozi hupenda kujua maswala ya mila, tamaduni na ibada zao kuwawezesha zaidi kuwa huru na kupewa haki wanayostahili kuishi nchi hizo. Hivyo sio swala la WINGI hakuna mtu anayetaka kujua wingi wa wahusika bali nafasi zao ktk jamii zetu iwe Ukerewe au Kariakoo na hii ndio maana na umuhimu wa neno DIVERSITY ktk Utaifa.
Hivyo sensa sio swala la serikali kujua wingi wa watu wake, hapa hatupo ktk mandalizi ya Harusi. Tunapoalikwa kwenye sherehe kuulizana tutakuwa na wageni wangapi ili kufanya maandalizi ya ukumbi, viti na sahani za chakula. Sisi wananchi sio receiving end bali ni wahusika wa maandalizi na upelekaji wa wamendeleo hayo, sensa inatusaidia sisi wote kujuana na sio kufichana ukweli ktk makusanyo ya nguvu kazi na uwekezaji. Report ya sensa sio kwa ajili ya serikali pekee bali ni pamoja na jamii zetu kwa kupitia asasi na wadau wake kujihusisha na upelekaji wa huduma hizo kwa wananchi wake. Ni kutokana na sensa kama hizi OIC, Vatican, AghaKhan, Jews pamoja na benki za nje zimekuwa na interest ya kuwekeza ama kutoa misaada nchini.
Kutokuwepo kwa ukweli ktk sensa zetu za mfumo kristu, mfumo wa kikoloni ambao hupendelea jamii moja kwa kuwajengea sababu na uhalali wa kuwa wao wabora zaidi. Mfumo ambao Waktistu wanaruhusiwa kufungua benki zao lakini Waislaam hawaruhusiwi isipokuwa kwa kupitia benki za serikali.. Waislaam wanazuiwa kujiunga na OIC kwa dhana kwamba Tanzania hatuihitaji japokuwa wakristu wanapewa misaada toka Vatican. Hata chombo chao cha dini kinatawaliwa na serikali (Bakwata) viongozi wake wako answerable kwa rais na sio kwa waislaam ni dalilitosha za defence mnayoiweka wakati mnatuita nyie waislaam fanyeni hivi ama vile kwa kutuamria na sio maamuzi yetu. Once unaposema waislaam hivi ama vile tayari unakubali kuwepo kwa tofauti lakini unaazimisha kuwa hazipo na ndio maana sisi tunailalamikia serikali (sio kanisa wala Mkristu) lakini mkristu ndiye anayetupa jibu..
Kwa majabu ya Firaun, tunapouliza muafaka wa MoU, wakristu wanaodai serikali iishindwa kuendesha shule zetu (kupeleka maendeleo kwa wananchi) hivyo Vatican kupitia CSSC wakapewa kazi hiyo lakini hamtaki kutazama kwamba swala hili ni kinyume isipokuwa pale waislaam wanapodai nafasi sawa ktk kulijenga Taifa japokuwa CSSC chombo cha kikristu kwa kushirikiana na serikali wanapeleka maendeleo kwa wananchi. Hivyo jibu la swali lako ni kwamba sensa sio kwa ajili ya serikali laa ni kwa ajili yetu sisi wote kufahamu tutaweza vipi kujiendeleza, kusambaza huduma na mahitaji yetu pasipo kumkwaza mtu mwingine ambaye tunafikiria hayupo kumbe yupo. kama leo unaamini CSSC inaleta maendeleo nchini na inasukuma gurudumu la maendeleo unashindwa nini kuelewa kwamba vyombo vingine pia vinaweza kuifanya kazi hiyo?..