jmushi1,Mkuu,kuna watanzania wa tofauti,kuna wale wenye kuelewa kuwa kuna utofauti kati ya kusimamia issue za taifa vs zile za dini,kuna wale wasiojuwa utofauti huo.Na pia kuna wale wanaojuwa tofauti hizo,lakini wanachaguwa maslahi ya dini kabla ya yale ya taifa.Ndo maana kuna tawala zilizowahi kupinga mambo ya dini kwenye mataifa wanayoyaongoza,Burundi ilikuwa ni mfano mmojawapo.Ninavyofahamu,kuna wananchi ambao wanafuata taratibu ama sheria za kimila inapokuja kwenye ndoa na mambo ya mirathi,na hayo wala serikali haihusiani nayo.
Ninasema hivyo kwasababu wale wanaotambua taifa kwanza then dini baadaye,wanaweza wasielewe,na inabidi waeleweshwe baada ya kukubaliana na wale wanaoelewa kwamba wale wasioelewa,basi waeleweshwe.
Pia binafsi nina swali,je mahakama hizo zinaweza kufunguliwa na misikiti bila kuihusisha serikali?kwa mfano,hata wakristo wana taratibu na sheria zao,na huwa zinafuatwa bila kuihusisha serikali.Nafahamu kuna wale wanaosema kuwa sheria zetu tulizoziadapt,basi chimbuko lake ni ukristo,na ndiyo maana wakristo huwa hawana shida nazo.Lakini ukiangalia kwa makini sheria wanazozitaka,basi ni sharia law.
Halafu pia, kuna wale wasiojuwa utofauti,yani hawajui kama mambo ya mahakama ya kadhi yana tofauti na sheria za nchi husika,wale ambao wanaweza kuona kama vile serikali iko bias.Ambao wanahisi kwamba sheria za mahakama ya kadhi ziko derived from sharia law,hao pia wanahitaji kueleweshwa.Kwahiyo kama wewe naelewa hayo,si kila mwananchi nayaelewa.
It's very unfortunately that u're dragging me to the discussion that had never been of my interest! Narudia, unanilazimisha kwenye mjadala ambao cjawahi hata mara moja kuupigia upatu hapa ingawaje si kwamba naona wale wanaoujadili hawana umuhimu wa kufanya hivyo. Nalazimika kuyajadili haya kwa shingo upande hususani pale ninapoona watu ama kwa kutofahamu au kwa makusudi kupotosha! I'd like to explain very short about this here; i'd appreciate kama utaridhika na yale machache na kama hutaridhika nayo basi, with due resect ningekuomba utafute thread inayoelezea masuala ya mahakama ya kadhi ukajifunze huko kama kweli una nia ya kujifunza! Nafahamu hiyo thread humu jamvini ipo ingawaje sizani kama nimeshawahi kuipitia au kuchangia chochote huko coz' it's not part of my interest. Na hata kama nimepata kuchangia, basi sizani kama nilipata kuwa active contributor kama ambavyo nimepata kuwa kwenye baadhi ya mada. Na kama ungependa kufahamu msimamo wangu kwenye suala la Mahakama ya Kadhi, then simple and clear kwamba itakuwa unfair kama mahakama hiyo itahitaji kutumia national resources; kodi za wananchi in particular ingawaje kwenye baadhi ya nchi za Africa ambako hata hao Muslims sio largest population, bado mahakama hizo ni sehemu ya mahaka zinazohudumiwa na serikali...... Hata hivyo, vile vile mahakama hizo hazitakuwa na maana endapo hazitapata legal approval frm the government....kama hazitakuwapo kwa mujibu wa sheria za nchi! Kenya na Uganda, mahakama hizi zipo kwa mujibu wa sheria (KATIBA)
Sasa, turudi kwenye suala la mahakama yenyewe!
Machache ambayo ningependa kuyasema hapa ni kwamba watu wanapotosha kwa makusudi kuhusu suala zima la mahakama ya kadhi. Watu wanapenda sana kuingiza suala la Sharia Law ili ionekane ni jinsi gani Mahakama ya Kadhi isivyofaa kwenye jamii yetu....!! Hii ni kwavile, tunapozungumzia Sharia Laws, watu akili zao wanazipeleka moja kwa moja kwenye watu kukatwa mikono, watu kupigwa mawe hadi kufa kama hukumu ya uzinzi na mambo mengine kama hayo! Huu ni upotoshaji wa makusudi coz' hilo sio lengo la mahakama ya kadhi na wala haitakuja kuwa lengo lake hususani kwa nchi kama Tanzania. Karibu nchi zote za Kiislamu zina Mahakama ya Kadhi lakini ni chache sana kati ya hizo zenye zina-apply Full Sharia kwenye mahakama hizo...hilo lazima ufahamu kama kweli ulikuwa hufahamu! Hata hapa East Africa, kuna Uganda na Kenya zote zina Mahakama za Kadhi ambazo zipo kwa mujibu wa katiba na zote hizo zina-deal only na muslims personal matters [ndoa, taraka na mirathi]!
Likewise, tujaribu kutofautisha kati ya Canon Laws na Mahakama ya Kadhi....hivi vitu ni tofauti kimfumo! Kwa lugha nyepesi, tunaweza kufananisha Canon Laws na sheria za kimila wakati Mahakama ya Kadhi tunaweza kufananisha na mahakama za kimila! Canon Laws, kama ilivyo kwa sheria za kimila, hazikupata kufutwa na serikali lakini Mahakama za Kadhi kama zilivyo mahakama za kimila; zilifutwa na serikali! Wanachohitaji waislamu ni kurudishiwa mahakama zao na sio sheria zao coz' sheria zipo pale pale na wala hakuna wa kuzifuta labda hadi pale Uislamu utakapotokemea duniani kama itakuja kutokea jambo hilo! Aidha, Mahakama za Kadhi si Misikiti bali ni Mahakama za Kisheria to deal ONLY to matters affecting personal status of muslims ambazo ni masuala ya ndoa, taraka na mirathi....PERIOD! Hii wala si mahakama ambayo mwizi atapelekwa kuhukumiwa ingawaje wapotoshaji wanapenda kusema huo utakuwa mwanzo tu lakini hapo baadae watataka zikate watu mikono!!
MAHAKAMA ZA KADHI NA CANON LAWS:
Kama nilivyotangulia kusema hapo awali, kuna tofauti kati ya Mahakama za Kadhi na Canon Laws. Na sizani kama kwenye Biblia kuna sehemu yoyote ambayo inaeleza ni namna gani mirathi inapaswa kugawanywa au ni namna gani taraka inapaswa kutolewa na rights za wahusika. Katika Quran wameeleza ni namna gani mirathi inapaswa kugawanywa ni akina nani wana haki ya kurithi kulingana na status ya marehemu(deceased family set up) na vile vile imeeleza vizuri mchakato wa taraka! Katika Uislamu, taraka ni suala la mchakato na sio suala la kuamka na kuandika taraka na kumwambia mkeo "TAKE THIS AND GO!" Kwenye Uislamu, except kwa suala la mirathi; kama hamna kifo, basi suala la mali linategemea na actual contribution ya mali husika kwa wanandoa. Hapa kuna uwezekano kwamba mali yote ikawa ya mke peke yake au ya mume peke yake au yao kwa pamoja kulingana na actual contribution ya kila mmoja! Lakini wakati mali ikiwa ni ya mwanamke kwa 100% basi halazimiki kutoa hata senti kumi kwa mtalaka wake; kwa mwanaume hata kama mali ni yake kwa 100% basi analazimishwa na Utamaduni wa Kiislamu kukata sehemu na kumpa mtalaka wake!! Hata kama mke ni Gavana wa BOT na mume ni mwalimu wa shule za kata; kwa mujibu wa Uislamu mwanaume huyu ana wajibu wa kutunza familia na mwanamke wala habanwi na sheria.....na mke huyu pamoja na ukwasi(utajiri) wake wote alionao bado ana haki ya kumpeleka mumewe huyu masikini kwenye mahakama ya kadhi kwamba mumewe haudumii familia! Mwanaume huyu maskini wala hana haki ya kumpeleka mkewe tajiri kwenye mahakama ya kadhi na kusema kwamba ingawaje mkewe ana pesa za kutosha lakini hatoi hata senti moja kwa ajili ya familia....huo si wajibu wake na akifanya hivyo ni kwa upendeleo wake tu huyo mwanamke na pindi anapofanya hivyo(kuhudumia familia); mwenyezi mungu anageuza mchango huo moja kwa moja kuwa sadaka! Hata hivyo, hapo haimaanishi kwamba Mwanamke akiwa na uwezo asihudumie familia; la hasha....busara inasema ahudumie tu na atapata malipo yake ya sadaka lakini halazimi na wala hatapata dhambi asipofanya hayo! So, mambo complicated kama hayo hayawezi kuwa handled na circular courts! Na kuwepo na sheria za kiislamu pasipo na mahakama za kadhi ni sawa na kuwa na graduates wa sheria pasi na kuwa na taasisi za ku-enforce sheria hizo!
Umegusia suala la mahakama za kadhi kuanzishwa na misikiti!!! This's very wrong mkuu wangu! Msikiti ni nyumba ya ibada na sio sehemu ya kutolea hukumu!! Msikiti utabaki msikiti na mahakama ya kadhi itabaki kuwa mahakama ya kadhi.....hivi vitu ni tofauti! Hata mimi naweza kusalisha msikitini; lakini sina weledi wa japo 10% wa kuwa hakimu wa mahakama ya kadhi!
Kwa kuchelea post hii kuwa ndefu na kuwa boring to read, niishie hapo tu!