jmushi1 ugumu unao wewe kwa kuwa unataka kupindisha mada....inawezekana ulikuwa na hoja ya msingi lakini ulikosa weledi wa kuiwasilisha ili ionekane ni yenye kutetea utaifa. Kutokana na huko kukosa weledi, ukaileta kiudini udini! Kimsingi, nimemwelewa sana Sweke34; sincerely, hoja yake ipo tofauti kabisa na yako, bila shaka ulitakiwa kuiwasilisha kama ambavyo Sweke anavyoilelezea! Lakini kwavile hoja ya msingi ni yako, na ndio maana unakuta nakazania pale pale kwenye msingi wako wewe coz' nafahamu ni hatari!
Kuhusu Nyerere, nimesema wazi kwamba he's a very honest person lakini watendaji wake walikuwa tatizo! Underline hapo! Na ndipo nikasema, as far as Mwalimu alikuwa ndie head of state basi hawezi kukwepa lawama za ubovu wa watendaji wake! In contrast, tuhuma zako wewe ni kwamba JK mwenyewe ndie MDINI....compare na hapo nilipokushauri u-underline(kwenye RED)! Yaani JK ni mdini kwavile "hamchukulii" hatua Ponda na vyombo vya habari vya kiislamu ingawaje yote hayo yapo kwenye mamlaka yasiyo na shaka yoyote ya watendaji husika na sio JK! Suala la Nyerere lilikuwa ni la kisera na hili la akina Ponda si la kisera! Kama Azimio la Arusha au Ujamaa havikuwa sahihi huwezi kumlaumu DC, RC, OCD au yeyote sawa na hao....lakini ikiwa Ponda anastahili kuchukuliwa hatua basi wanaostahili kubeba lawama ni watendaji sawa na hao niliokutajia unless uniambie na kunithibitishia (ingawaje nafahamu huwa hutaki kuthibitisha hoja) kwamba JK anawazuia wahusika kuchukua hatua! Nikakupa hadi mfano wa akina Mwakyembe; lakini hutaki kabisa kuelewa....kulikoni?! Tatizo lako unataka kuchanganya DINI na SIASA za CHADEMA na ndio maana ulimshngaa Mkandara kwanini hakuungi mkono ikiwa anajinadi nae ni CHADEMA....tht's ur STRONGEST weakness!!