Kwa mambo haya - JK ni Mdini!

Kwa mambo haya - JK ni Mdini!

Status
Not open for further replies.
pengine Mtei aliuona udini wa Jk kabla yangu.Hakuna aliyejuwa JK ni mdini mwanzoni,rangi zake zimejionyesha na taifa linakwenda kombo.Kama miye ndo mdini nimesababisha hayo,then una hoja.Otherwise rudi kwenye hoja mkuu,mimi si rais wa nchi ati.Tafadhali jadili hoja si mimi.Unataka kufanya character assasination kwasababu umeudhika sana,hilo huwezi coz im nobody,hoja zinajisimamia zenyewe,pitia hii mada toka mwanzo,kuna waru wametoa maoni safi sana.

Una kazi kubwa ya kufanya kumtetea fisadi mdini,kwasababu matokeo yake ni wewe kuonekajna na nia moja,yani kutumia udini kulinda ama kuwakingia kifua mafisadi.Thats the truth.

Hakuna ambacho sijakujibu, labda kama hutaki kuelewa.....au unataka nikujibu kila kipengele peke yake?! Tuanze basi na wewe utoe hoja za ku-support madai yako!
1. Umesema: "Kinachonifanya niamini ni JK,ni kwasababu hao wanaopinga kasi ya upinzani,wanapoijibia serikali ya ccm,basi wanaoonyesha chuki za wazi kabisa za kidini.Ule udugu tuliokuwa nao wakitanzania haupo tena,na sijui utarudi kwa njia gani."
Sasa hapa unataka nijibu nini wakati hamna hoja ya kuijibu?! Labda nikuulize wewe: ni akina nani hao wanaoijibia serikali na waliijibia nini kinachoonesha chuki za wazi za udini?! NAOMBA UNIJIBU hapa otherwise hakuna hoja ya maana hapo uliyoieleza!

2. Aidha ukasema:"
Kuna habari kuwa hata mtu na mke wake wanataka kutoana roho kwasbabu hizo hizo.Sheick Ponda alipotoa kauli kinyume na yakwake kuhusu sensa,kaliachia na gazeti lenye kusambaza sumu hizo huku akilifungia lenye kusema ukweli(mwanahalisi)"
Hapo pia nikakupa changamoto kwamba wenzako wanasema aliyelifungia Mwanahalisi ni Membe kwa ajili ya kumlinda mtuhumiwa namba moja kwenye makala ya Mwanahalisi ambae wanasema ni swahiba wa Membe hivyo nimeshangaa kusikia kumbe aliyelifungia Mwanahalisi kwa mujibu wako ni JK. But all in all, nikakuuliza, kwani kazi ya kufungia magazeti ni ya Rais hadi ulalamike ni kwanini hayafungii hayo magazeti yanayosambaza sumu...!!!! Nikakupa hadi mfano wa Mwakyembe na Kagasheki ambao wamechukua hatua bila kuingiliwa na Rais...sasa kwanini usimlaumu Waziri wa Habari kwa kutoyachukulia hatua hayo magazeti yanayomwaga sumu?! Nimekukumbusha kwamba Mwakyembe alitamka wazi, tena hadharani kwamba si kweli kwamba Mawaziri hawana mamlaka ya kuchukua hatua.....labda hapo ubadilishe mada kwamba Waziri wa habari alitaka kuyafungia magazeti yanayomwaga sumu lakini JK akakataza kwa sababu ni magazeti ya Kiislamu!! Kama huna hoja ya ku-support hayo basi nitaona hiyo nayo ni hoja isiyo na chembe ya mashiko!!!!

3. Vile vile ukachomekea hili: "
Kama JK ni mdini,tufanyeje?Ni wazi anapenda haya yaendelee kuwepo kwasababu ni kama anauwa ndege wawili kwa jiwe moja,yani kwasababu yeye ni fisadi na mdini,basi issue za ufisadi wake anazifukia kwa kupenyeza sentiments za kidini kwasababu anajuwa the issue is extremely sensitive."
Hapa pia nimekuuliza.....hivi kashfa za ufisadi za nchi hii ni dhidi ya Waislamu pekee?! Ni kashfa ipi ya ufisadi ambayo hatimae JK akapenyeza UDINI ili kuficha tuhuma hizo dhidi yake na labda hao mafisadi wenzake?! Nitajie moja tu;hoja ya ufisadi ikafinyangwafinyangwa baada ya JK kuchomkea udini! Kama huna ya kuitaja basi nayo ni hoja nyingine nyepesi isiyo na mashiko yoyote kwa kuwa haiakisi unachokiubiri!!!

4. Hatimae ukamalizia: "
Je kama taifa tutapona dhidi ya udini huu wa JK?je kukitokea mapigano,nani atakuwa responsible?Je nini kifanyike kukomesha udin8I hu?ama tumeridhika?!...."
Hebu hapa nipe jambo moja la msingi la udini wa JK!!! Wala usiniambie habari za akina Ponda na magazeti ya SAUTI simply because vipo vyombo husika vinavyotakiwa kuchukuwa hatua! Ipo Wizara Ya Mambo ya Ndani, Ipo Wizara ya Habari na mamlaka nyngine zenye meno ya kutosha kuchukua maamuzi dhidi ya hao akina Ponda! Kama hapo napo huna cha kuthibitisha, basi nitalazimika ku-conclude kwa mara nyingine kwamba wewe ndie mdini kwa kuwa umeshindwa kuthibitisha tuhuma za udini unazodai kuwapo!

Pamoja na yote, kwenye post zangu nimeshazungumza kwamba wakati wa kampeni JK alikuwa anakemea sana suala la udini, lakini watu wa ajabu ajabu wakadai nchi hii haina udini hivyo mdini ni huyo JK anayekemea kitu kisichokuwepo na hivyo anaweza kusababisha kupandikiza mbegu za udini!!!


 
Hapa tz kama kuna udini basi nyerere ndo muasisi. Yeye alikuwa amelibeba kanisa bila woga na kutuminyi sisi waislamu. Kupitia redio imani na vyombo vingine vya kiislamu. Kwa dhuluma mlotufanyia sasa basi tumewastukia elementi za udini mnatengeneza nyie alafu mnasema waislamu ni wadini acheni udini nyie. Redio imani inawaumbua sasa kwa data za ukweli ndo mana mnaichukia mnaomba ifungwe bila sababu za msingi. Siku zote mtu akisema ukweli anaonekana mkorofi. Hapa duniani ukisema ukweli watu wanakutoa roho kwa redio imani mmechemka. Mchafueni huyohuyo jk wenu mlomuweka madarakani na mkamwita chaguo la mungu leo imekuwaje tena ? Au mungu kabatilisha chuguo ? Au kagusa maslai yenu leo ndo mnamwita mdini ? Hacheni propaganda chafu
 
By Jacobus Mie hupendelea kuisikiliza radio Imani ya Morogoro, ukweli radio hii haina jema kwa taifa letu. Mtu makini utatarajia chombo cha habari cha kidini kazi yake ni kuwaelimisha/kuwakumbusha kuhusu imani ya dini hiyo, lakini radio hiyo imejikita kuwafanya waumini/wasikilizaji wake wajione wananyanyaswa, kudhurumiwa na kila unyonge wa mwanadamu hapa duniani hufanyiwa lakini watawala wetu wanaona sawa tu na kulifungia gazeti. Nachelea kuamini kuwa labda vita ya kidini inaandaliwa.

Hembu thibitisha kwamba vitendo vyenye kutiwa rangi nyekundu havitokei dhidi ya kundi husika au na wewe ni sehemu ya mkakati husika wa unyanyasaji?
 
Sijadiliani na wadini,we huna mpango wala huna haja ya kujibu posti yangu,changanya masaburi najuwa unamtetea baba yako.Kuna thread nyingi tu,peleka masaburi kwenye ile ya Zomba.

Mkuu wangu Kongosho,

Nadhani umemsoma vizuri jamaa anavyoporomosha matusi dhidi yangu halafu ananiambia mie na domo chafu, mie hata siku moja siwezi kumvunjia heshima mzazi wa mwenzangu humu JF...mtu wa hivi anaekutukana anajumuisha na wazazi mie wa nini kujadiliana nae.
 
Last edited by a moderator:
Kwa hilo la kwanza. Mimi nina shangazi yangu yupo Mwanza. Ni mkatoliki kama mimi ila yeye ni CCM damudamu. Alinisimulia mwenyewe kwamba wakati wa uchaguzi 2010, alipata msukosuko kidogo kwa kujifanya mwana ccm. Wenzake walikuwa wampanga wakipigie kura chama cha upinzani lakini yeye akagoma. Na ilikuwa bado kidogo tu atengwe. Ninachosema hapa ni kwamba. Wapo baadhi ya wakatoliki wadini. Baadhi ya walutheri wadini, baadhi ya waislam wadini nk. Naomba uondoe hicho kitu ulichokisema eti "lakini hapa mnachomaanisha hakemei waislamu".
Tunachomanisha hapa ni viongozi wa serikali na Kikwete kama kiongozi mkuu wamefanya nini kukemea huu udini tunaouona ukishamiri? Hapa haijalishi ni waislam ama ni wakristu. Wamefanya nini viongozi wetu?

Hilo la Mtei mimi msimamo wangu unajulikana na unaweza ukafuatilia post kule. Hata hiyo tume ya katiba ingekuwa na waislam wote, kwangu mimi haina tatizo as long as ni watu waadilifu.

LABDA unachomaanisha wewe lakini sio jmushi1! Ni mpuuzi tu ndie ambae anaweza kupinga kwamba nchi hii haina udini.....ninachopinga mimi ni hoja ya kudhihirisha udini wa JK kwa sababu tu Ponda amebishana na serikali lakini hajachukuliwa hatua yoyote, kwamba gazeti la SAUTI(binafsi wala silifahamu) linamwaga sumu, lakini haijachukuliwa hatua yoyote.....haya yanahusishwa na Uislamu wa JK jambo ambalo nasema sio sahihi kwani wapo wenye mamlaka wa kuweza kuchukua hatua....na ndio maana nikatoa mfano wa Mwakyembe! Hoja ya mtoa hoja si kwamba serikali inalea choko choko za kidini bali JK ni mdini!!! Kama JK ni mdini, na yeye ni Mwislamu basi maana yake ni kwamba anaupendelea Uislamu na Waislamu na kuukandamiza Ukristo na Wakristo...huo ndio udini ambao unaweza kufanywa na kiongozi wa nchi!!!.kama ingekuwa ndiyo hoja yake ni kushamiri kwa udini nchini, hapo tungeenda pamoja!
 


Pamoja na yote, kwenye post zangu nimeshazungumza kwamba wakati wa kampeni JK alikuwa anakemea sana suala la udini, lakini watu wa ajabu ajabu wakadai nchi hii haina udini hivyo mdini ni huyo JK anayekemea kitu kisichokuwepo na hivyo anaweza kusababisha kupandikiza mbegu za udini!!!
Ni kweli hii kitu umeirudia sana, lakini haijibu kitu chochote. Unachotaka kusema hapa ni kwamba kwa sababu kikwete alilisema hili la udini kwenye kampeni zake na watu wakampuuzia, basi, kwa hiyo sasa hivi tusimhoji jinsi anavyokemea udini au una maana gani?
 
@Kongosho vita haiko mbali. Haya mauaji yanayoendelea kufanywa na polisi magamba ni dalili tosha kwamba vita vya wenyewe kwa wenyewe vinainyemelea Tanzania kwa karibu sana. Angalia mauaji yanavyozidi kutokea katika sehemu mbali mbali nchini na hakuna hata wa kukemea mauaji hayo. Kikwete yuko kimyaaa yule Pinda naye yuko kimyaaa wanaacha mbegu ya chuki nchini izidi kushamiri kila kukicha.

Halafu mie kinanishangaza sana kuona wale Viongozi wastaafu kama akina Mwinyi, SAS, Warioba na wengine wengi ambao bado wanaheshimika na wananchi wengi nao pia wako kimya kabisa. Wanayaona na kuyasikia matukio ya kutisha nchini yakishamiri siku hadi siku lakini wanaangalia pembeni kama vile hayawahusu lakini vita hii ikitokea utakuwa ni kama mtego wa panya wataingia waliokuwemo na wasiokuwemo.

Wapumbavu kama akina Mwigulu na magamba wengine wanaachiwa kupandikiza mbegu ya chuki nchini kila kukicha kwa sababu tu ya kutaka kutimiza ndoto yao ya magamba kuitawala Tanzania milele bila kuangalia athari kubwa za chuki wanazozipandikiza kila kukicha.

Amani imeshapotea nchini miaka mingi sasa na hali inazidi kuwa mbaya kila siku iendayo kwa Mungu. Wananchi wamechoshwa kuona Watanzania wenzao wanauwawa na polisi magamba bila hatua zozote kuchukuliwa na Serikali sasa watakapoanza kurudisha mapigo hapo ndio nchi itawaka moto na hakutakuwa na msalie mtume.


NB: Uwe unakuja huku mara nyingi badala ya kuishia kule nanihii

yani hilo li rahisi lenu ninalichukia natamani kungekuwa na uchaguzi wa dharura, liondoke mapema hawez kujenga hoja hana dira wala hajui anafanya nini ikulu huyu ndio JK THE NEW VASCO DA GAMA
 
LABDA unachomaanisha wewe lakini sio jmushi1! Ni mpuuzi tu ndie ambae anaweza kupinga kwamba nchi hii haina udini.....ninachopinga mimi ni hoja ya kudhihirisha udini wa JK kwa sababu tu Ponda amebishana na serikali lakini hajachukuliwa hatua yoyote, kwamba gazeti la SAUTI(binafsi wala silifahamu) linamwaga sumu, lakini haijachukuliwa hatua yoyote.....haya yanahusishwa na Uislamu wa JK jambo ambalo nasema sio sahihi kwani wapo wenye mamlaka wa kuweza kuchukua hatua....na ndio maana nikatoa mfano wa Mwakyembe! Hoja ya mtoa hoja si kwamba serikali inalea choko choko za kidini bali JK ni mdini!!! Kama JK ni mdini, na yeye ni Mwislamu basi maana yake ni kwamba anaupendelea Uislamu na Waislamu na kuukandamiza Ukristo na Wakristo...huo ndio udini ambao unaweza kufanywa na kiongozi wa nchi!!!.kama ingekuwa ndiyo hoja yake ni kushamiri kwa udini nchini, hapo tungeenda pamoja!
Hao wenye mamlaka ya kuchukua hatua wakishindwa kuchukua hatua Kikwete anatakiwa afanye nini kama Kiongozi mwenye mamlaka ya juu? Kama anawaaangalia tu utakataa tukimuita dhaifu au kwa namna moja au nyingine ananufaika na hii hali ya kutokuchukuliwa hatua yeyote!?
 
Mkuu wangu Kongosho,

Nadhani umemsoma vizuri jamaa anavyoporomosha matusi dhidi yangu halafu ananiambia mie na domo chafu, mie hata siku moja siwezi kumvunjia heshima mzazi wa mwenzangu humu JF...mtu wa hivi anaekutukana anajumuisha na wazazi mie wa nini kujadiliana nae.
Kumbe ni kweli wewe ni Ridhiwani?inatosha tuache mjadala uendelee,taifa liko pabaya.Na kama wewe ndiye ritz1,basi fikisha salam kwa mzee.
 
Last edited by a moderator:
Kumbe ni kweli wewe ni Ridhiwani?inatosha tuache mjadala uendelee,taifa liko pabaya.Na kama wewe ndiye ritz1,basi fikisha salam kwa mzee.
Yote unayasema wewe mie nikisema utaniambia na mdomo mchafu...nadhani jamaa yako Kongosho kukusoma...wewe niite upendavyo hakuna shida.
 
Last edited by a moderator:
Ritz na jmushi1, mjadala huu utasaidia kurudisha ile heshima iliyopotea labda bila kujua.

Na nyie mtatusaidia kuwa pioneers wa majadala sensitive kama huu kwa hoja.

Huoni kama itakuwa changamoto kwenu kukaa sred moja na kujadili hoja kwa hoja??

Mtatupa na sie hamasa ya kujadili kwa hoja pia.

Hayo mloambiana awali, tuyadelete tuanze upya.
 
Last edited by a moderator:
Yote unayasema wewe mie nikisema utaniambia na mdomo mchafu...nadhani jamaa yako Kongosho kukusoma...wewe niite upendavyo hakuna shida.

Mwambie mzee akemee udini nchi iko pabaya!Halafu kusema utabeba mtutu eti Padri akiwa raisi ndo udini namba moja.Tuachane na haya.Taifa liko pabaya.Shida yangu na wewe ni unapoingiza udini hata kama ni issueinayohusu ufisadi. Akihoji Slaa utatukana eti padri,mara kanisa,nakwambia msipokuwa makini mtakuja kuwa held responsible na wazalendo wa nchi hii.
 
Last edited by a moderator:
Ni kweli hii kitu umeirudia sana, lakini haijibu kitu chochote. Unachotaka kusema hapa ni kwamba kwa sababu kikwete alilisema hili la udini kwenye kampeni zake na watu wakampuuzia, basi, kwa hiyo sasa hivi tusimhoji jinsi anavyokemea udini au una maana gani?

Nimesema hakuna ambacho sijajibu kinachostahili kujibiwa....si kila kinachoandikwa lazima kijibiwe!!! Likewise, hilo la JK na kampeni ni kuonesha kwamba pale anapowajibika kulizungumzia la udini anafanya hivyo na kwamba si kweli kuwa hakemei....hiyo ndo hoja yangu! Wapuuzi wa nchi hii, wakati JK anakemea UDINI wakati wa uchaguzi wakafanya ionekane kwamba anawaambia Waislamu wasimchague Dr Slaa kwavile ni Mristo na ndio maana wakaishia kusema kwamba JK kuzungumzia udini ndo anapandikiza udini! It was one of the stupid arguments ambazo zimepata kutolewa nchi hii!

Hayo ya akina Ponda na magazeti ya SAUTI wapo wa kuyafanyia kazi vinginevyo hakuna sababu za kuwa na taasisi mbalimbali nchini na badala yake angeachwa tu Rais awe ndie mtendaji wa kila jambo! Nchimbi si yupo, yeye anafanya nini?! Kule habari si kuna m2, yeye anafanya nini hadi Rais aitishe Press Conference kwa ajili ya Ponda....hivi nchi haina ma-DC, RC, OCD, RPC?! Juzi wakati (JK) anahojiwa baada ya kujiandikisha sensa, kuna mwandishi alimuuliza ni hatua gani watachukuliwa wanaokaidi zoezi la sensa....yeye akasema, na ndivyo ilivyokuwa amefanya kwamba, ameshatoa agizo! Na in fact, wala hapakutakiwa kuwa na agizo kwavile watendaji wanafahamu wajibu wao! Hivyo, hoja yangu inabaki pale pale kwamba si sahihi kuhusisha yanayotokea na Uislamu wa JK.....huo ndio UDINI wenyewe! Nisingekuwa na tatizo endapo labda yanayotokewa yangehusishwa na udhaifu wa serikali, lakini ni upuuzi kuhusisha dini ya mtu!!! Ni aibu kwa kizazi kinachojifanya kinapinga ubaguzi wa dini kudai Ponda anachekelewa kv JK ni Muislamu....ni aibu kwa kizazi kinachojifanya kinatetea haki kudai JK analeta UDINI kwenye ufisadi.....kudai gazeti gani sijui linaachiwa kv Rais ni Mwislamu!!
 
Ritz na jmushi1, mjadala huu utasaidia kurudisha ile heshima iliyopotea labda bila kujua.

Na nyie mtatusaidia kuwa pioneers wa majadala sensitive kama huu kwa hoja.

Huoni kama itakuwa changamoto kwenu kukaa sred moja na kujadili hoja kwa hoja??

Mtatupa na sie hamasa ya kujadili kwa hoja pia.

Hayo mloambiana awali, tuyadelete tuanze upya.
I second this...
 
Last edited by a moderator:
Kongosho,

Mie sina tatizo na mtu nadhani umeona nani anayemtolea mwenzake lugha ambazo sio za kiungwana najuwa huwezi kumwambia swaiba wako umetumia ukongwe kufikisha ujumbe...ngoja mie nijitoe kwenye hii thread tabaki kuwa msomaji.
 
Last edited by a moderator:
Mkuu leo inakuwaje? Mbona wewe ni mchangiaji makini sana humu jamvini!
Mbona watu tunataka kujua vitu rahisi kabisa lakini unatuzungusha?
Viongozi wa serikali na Kikwete mwenyewe wamefanya nini kukemea udini unaonea kama alivyosema mtukufu rais mwenyewe wakati wa uzinduzi wa bunge 2010?

mleta thread ametuambia hapa tunajadili udini wa kikwete na si vinginevyo...! naona ameshapandisha jazba na kuanza kutukana simply " hana hoja yenye mshiko kuonesha udini wa JK upo wapi"

sasa udhaifu unaonyeshwa na watendaje wake wa chini unamfanya kikwete awe mdini! ... swake34 i beg you please nipe mifano hai hata miwili kuonesha udini alioufanya JK!...

mtoa mada amezunguka na kugotea kwenye sensa .. nimarangapi JK aliongelea sensa na waislam kugoma.?! au milihitaji afanye nini zaidi..?

mwisho - udini ni nini...?! maana naona sikuhizi kiongozi mwislam akifanya jambo lolote anaitwa mdini..!? hivi udini umekuwa = uislam..?!
 
Hao wenye mamlaka ya kuchukua hatua wakishindwa kuchukua hatua Kikwete anatakiwa afanye nini kama Kiongozi mwenye mamlaka ya juu? Kama anawaaangalia tu utakataa tukimuita dhaifu au kwa namna moja au nyingine ananufaika na hii hali ya kutokuchukuliwa hatua yeyote!?

Kwa bahati mbaya sana bado unapita mule mule ambamo tayari nimeshazungumza kabla.......nilishasema labda, mtoa mada alete hoja ya udhaifu wa serikali na sio UDINI....the topic under question ni UDINI therefore, hata kama itabainika beyond reasonable doubt kwamba anashindwa kuwachukulia hatua wahusika, basi bado hoja haiwezi kuwa udini coz' good enough, at least for now, Mawaziri wenye dhamana ktk hayo wote ni Wakristo kwahiyo itakuwa ni kichekesho kwa Mdini Mwislamu amtetee na kumlinda Mkristo!!!
 
Mwambie mzee akemee udini nchi iko pabaya!Halafu kusema utabeba mtutu eti Padri akiwa raisi ndo udini namba moja.Tuachane na haya.Taifa liko pabaya.Shida yangu na wewe ni unapoingiza udini hata kama ni issueinayohusu ufisadi. Akihoji Slaa utatukana eti padri,mara kanisa,nakwambia msipokuwa makini mtakuja kuwa held responsible na wazalendo wa nchi hii.

Kabla sijaondoka kwenye thread nataka niweke sawa Kongosho jamaa yako Mnafiki sana ana PhD ya majungu aisee..

Uzuri wa JF kuna Hansard za kila member namuomba aweke hayo maneno niliyosema Padri akiwa rais nitabeba mtutu...ukiweka najitoa JF na usipoweka wewe ni mnafiki na mzandiki wa kwanza humu JF usipoweka takuwa nakuiata Mzandiki.
 
Last edited by a moderator:
Kabla sijaondoka kwenye thread nataka niweke sawa Kongosho jamaa yako Mnafiki sana ana PhD ya majungu aisee..

Uzuri wa JF kuna Hansard za kila member namuomba aweke hayo maneno niliyosema Padri akiwa rais nitabeba mtutu...ukiweka najitoa JF na usipoweka wewe ni mnafiki na mzandiki wa kwanza humu JF usipoweka takuwa nakuiata Mzandiki.
Nani ana muda huo,we wahi tu.Endelea na shughuli fisadi mdini.Nikapitie posti zako si ntatapika?
 
Last edited by a moderator:
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom