BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,769
- 288,287
@Kongosho vita haiko mbali. Haya mauaji yanayoendelea kufanywa na polisi magamba ni dalili tosha kwamba vita vya wenyewe kwa wenyewe vinainyemelea Tanzania kwa karibu sana. Angalia mauaji yanavyozidi kutokea katika sehemu mbali mbali nchini na hakuna hata wa kukemea mauaji hayo. Kikwete yuko kimyaaa yule Pinda naye yuko kimyaaa wanaacha mbegu ya chuki nchini izidi kushamiri kila kukicha.
Halafu mie kinanishangaza sana kuona wale Viongozi wastaafu kama akina Mwinyi, SAS, Warioba na wengine wengi ambao bado wanaheshimika na wananchi wengi nao pia wako kimya kabisa. Wanayaona na kuyasikia matukio ya kutisha nchini yakishamiri siku hadi siku lakini wanaangalia pembeni kama vile hayawahusu lakini vita hii ikitokea utakuwa ni kama mtego wa panya wataingia waliokuwemo na wasiokuwemo.
Wapumbavu kama akina Mwigulu na magamba wengine wanaachiwa kupandikiza mbegu ya chuki nchini kila kukicha kwa sababu tu ya kutaka kutimiza ndoto yao ya magamba kuitawala Tanzania milele bila kuangalia athari kubwa za chuki wanazozipandikiza kila kukicha.
Amani imeshapotea nchini miaka mingi sasa na hali inazidi kuwa mbaya kila siku iendayo kwa Mungu. Wananchi wamechoshwa kuona Watanzania wenzao wanauwawa na polisi magamba bila hatua zozote kuchukuliwa na Serikali sasa watakapoanza kurudisha mapigo hapo ndio nchi itawaka moto na hakutakuwa na msalie mtume.
NB: Uwe unakuja huku mara nyingi badala ya kuishia kule nanihii
Halafu mie kinanishangaza sana kuona wale Viongozi wastaafu kama akina Mwinyi, SAS, Warioba na wengine wengi ambao bado wanaheshimika na wananchi wengi nao pia wako kimya kabisa. Wanayaona na kuyasikia matukio ya kutisha nchini yakishamiri siku hadi siku lakini wanaangalia pembeni kama vile hayawahusu lakini vita hii ikitokea utakuwa ni kama mtego wa panya wataingia waliokuwemo na wasiokuwemo.
Wapumbavu kama akina Mwigulu na magamba wengine wanaachiwa kupandikiza mbegu ya chuki nchini kila kukicha kwa sababu tu ya kutaka kutimiza ndoto yao ya magamba kuitawala Tanzania milele bila kuangalia athari kubwa za chuki wanazozipandikiza kila kukicha.
Amani imeshapotea nchini miaka mingi sasa na hali inazidi kuwa mbaya kila siku iendayo kwa Mungu. Wananchi wamechoshwa kuona Watanzania wenzao wanauwawa na polisi magamba bila hatua zozote kuchukuliwa na Serikali sasa watakapoanza kurudisha mapigo hapo ndio nchi itawaka moto na hakutakuwa na msalie mtume.
NB: Uwe unakuja huku mara nyingi badala ya kuishia kule nanihii
tutajipamba hapa kwa maneno, lakini ikitokea vita, tutakaoathirika hasa ni sie tusokuwa na uwezo wa kugharimia familia zetu kwenda kuishi nje.
Wao utakuta familia zote ziko nje.