Ukweli kaka tunakoelekea na udini ni kubaya tusipopata viongozi wa kutuongoza kuondokana na janga hili kama wananchi tutashindwa kujiongoza wenyewe. Kaka kuna kitu kilinisikitisha sana kilitokea UDOM mwaka jana kama sikosei, kuna mdahalo uliandaliwa na waislamu pale chuoni na kichokuwa kikijadiliwa na UDINI mtupu na mikakati ya ajabu ya kidini na kupandikiza chuki dhidi ya ukristo, walienda mbali na kudai watakwenda Butiama kumsomea hukumu baba wa Taifa kwa makosa aliyowafanyia waislamu. wakajadili na mikakati ya kuendelea kukaa ikulu eti wakidai kanisa haliwezi kuruhusu kibaragashia kuendelea tena miaka kumi pale white house, hivyo wamejipanga vema na kamili kwa mapambano mwaka 2015! ni kikao ambacho katika nchi isiyo kuwa na dili kama yetu kuruhusiwa kuandaliwa na tena wanaojfanya mjadala ni walimu wa vyuo. kwa kweli ni hatari sana kaka! na kwa haya siju JK amajiandaa kwa legacy ipi atakapo toka madarakani!
ni kikao kilichoendeshwa kwa siri kubwa lakini kama unavyojua kuna watu wanaelimu kuliko yao ya kukariri madrasa tulipata tape bila wao kujua! wakawa wanadai eti mabinti wa kiislamu kuolewa au kuchukuliwa na wakristo ni fadhaa kubwa kwao hivyo wasidhubutu kufanya hivyo. Na cha ajabu waislamu kwa sasa wanafanya vitu kama wanavyotaka bila hata onyo lolote kutoka serikalin. Wanafunzi wa UDOM mwaka jana kwenye uchaguzi walikuwepo wagombea wawili binti mkristo na jamaa wa kiislamu, jamaa wakaweka mabango kuwa ni MOHAMMED V JESUS. bahati nzuri wakapigwa chini kwenye kura. kweli ni hatari.
Hakuna kitu kibaya kama UNAFIKI na UZANDIKI.....waswahili wanasema wazi kwamba, MUNGU HAMFICHI MNAFIKI......hapo juu unadai kulikuwa na MDAHALO, ghafla unabadilika na kusema kilikuwa ni KIKAO CHA SIRI! Aibu sana, kama huko vyuo vikuu kuna watu staili yako ambao damu yao imejaa UDINI wa kutisha basi ni hatari kubwa kwa taifa hili. Yaani maandiko yako yanaonesha jinsi ulivyo mdini wa kutisha, na bahati mzuri haupo hodari kama alivyo jmushi1 katika kuficha udini wenu. Binafsi, wala sitafuni maneno, jmushi1 ni mdini sana lakini hana confidence ya kudhirisha udini wake....huwa anajitahidi sana kujificha lakini huwa inatokea mara moja moja anajisahau na kuishia kujivua nguo.....!!!