Kwa mambo haya - JK ni Mdini!

Kwa mambo haya - JK ni Mdini!

Status
Not open for further replies.
Jmushi1...unafahamika kwa Udini wako.
Wewe ulitaka JK atoe amri ya Kukamatwa Ponda...kwakuwa hakutoa hio Kauli umesema "Mdini"

Wala hukutaka Kumwambia JK au Serikali ichukue hatua kwa wale waliotoa Takwimu "Feki" Hizi Takwimu Feki even Wizara ya Pinda imetoa Kalenda ikiweka Hizo "Takwimu Feki"

Kwa hili wewe Umemuita JK "Mdini"

Uchaguzi unafahamika Namna Kampeni zilivyofanywa, JK na Wenzake walikuwa hawaamini the so called "UDINI" hadi mlipoanza Kampeni "Makanisani" hadi wengine "kutengwa" Mkadai "elimu ya Uraia mnaitoa"
Wakati CUF wanaitwa Wadini Hamkusema chochote...Hadi post nyingi hapa JF zinaonesha hivyo...ila Mkiitwa nyie Chadema wadini mnakuja juu kutafuta visingizio!!!

Huyu JK amefanya mengi kuwafavor wakristo kuliko waislam...Hizi kelele mnazoendelea kuzipiga ili mzidi kupewa nafasi zaid...!!! Maana mshazoea tangu huko nyuma waislam wasiipinge Serikali, wakiipinga basi wakalale "JELA" hapo mtakunywa sana Pombe zenu kwa "furaha"

Waislam hawajapata chochote cha Maana kutoka kwa JK, zaid hilo la kusema kutokamatwa shk Ponda....May be kilio chako kitasikilizwa Maana Sensa haijaaisha...so Ponda akikamatwa labda utaweka Post ya Kumpongeza JK...So far wanafamilia wengi wameshaanza kukamatwa hadi watoto kisa baba zao Hawapo ktk "kuhesabiwa"...Labda hizi taarifa za kukamatwa wanafamilia wa kiislam kwasababu za sensa zitakuridhisha kiasi...Maana wenzako washaweka mada kwanini wanaopinga sensa "wasikamatwe" Halafu unataka Amani au Kujenga Nchi mmoja wakati unamuombea Mabaya mwezio yamkute...!!!

Twendeni...JK ataondoka litakuja "chaguo Lenu"
HELL HELL HELL!! mlitaka kupata nini zaidi?? KIPI kingine?? zaidi ya mnavyoreap bila kupanda? Je mnajua BAKWATA ina Bajeti kutoka serikalini? Je mnajua mahakama ya kadhi inagharamiwa na serikali kinyemela!??
Hamtakiwi kulalamika baada ya kumruhusu kumchakachua muislamu msomi Salim Ahmed Salim. Kwa ule ubaguzi aliofanya yeye na mtandao ule wa kishetani kwa Salim laana ya ubaguzi itamla yeye na serikali yake hadi mwisho. Hata wale wanaokubali kutumika kama wewe hawataweza kuzuia!! Ona sasa dalili zote za utawala uliofitinika zi wazi. Mitandao inagongana!! Haponi!!
 
Mkuu chama,
Tafsiri ya Udini ni Uslam ukiwa Mkristo uwezi kuwa mdini muhasisi wa Chadema Edwin Mtei, alitoa kauli kuhoji uwiano wa dini wakati Rais JK, alivyowateuwa wajumbe wa tume ya katiba lakini kwa Wakiristo kwa hilo sio udini wanasema Mtei alikuwa sahihi kutoa hiyo kauli, jana nimeanzisha thread kutaja kauli ya Mtei, hatimaye thread yangu imepotezwa imechanganywa na JK mdini, mkuu chama, hivi kweli Wakiristo Tanzania wanaweza kweli kulalamika wakati keki ya taifa wanakula wao, Wizara zote za serikali taasisi zote za umma kote huko wamejaa wao...tunapoelekea ni kubaya kuna siku tutapigana mitutu sisi kwa sisi.
 
Last edited by a moderator:
CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kimesema kuwa kutokana na kujirudiarudia kwa mauaji yanayofanywa na vyombo vya dola, Rais Jakaya Kikwete, anapaswa kuingilia kati kuunda tume huru ili kuwezesha uchunguzi wa kina.

Hata hivyo, wakati CHADEMA ikitaka tume huru ya kuchunguza matukio hayo likiwemo lile la kuuawa kwa kijana Ally Hassan Singano maarufu kama Zona katika maadamano yao juzi, Jeshi la Polisi Mkoa wa Morogoro, limejivua lawama za mauaji hayo.

Akizungumza jana jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi wa Habari na Uenezi wa CHADEMA, John Mnyika, alisema wanapinga kauli za serikali, Jeshi la Polisi na CCM zenye kulipotosha taifa kuhusu mashambulizi na mauaji yanayoelezwa kufanywa na askari mkoani Morogoro.

Mnyika ambaye pia ni mbunge wa Ubungo, alisema kuwa kauli zilizotolewa na Waziri wa Mambo ya Ndani juzi, Dk. Emmanuel Nchimbi zina mwelekeo wa kulilinda Jeshi la Polisi, ambalo askari na maofisa wake ni sehemu ya watuhumiwa wa mauaji badala ya kuwezesha ukweli kuthibitika na hatua kuchukuliwa kwa wahusika.

“Ikumbukwe kuwa Agosti 27 mwaka huu, polisi mkoani Morogoro walifyatua risasi za moto na kupiga mabomu ya machozi wananchi na wanachama wa CHADEMA waliokuwa wamejikusanya kwa ajili ya kuelekea kwenye mkutano halali, na kusababisha kifo cha raia mmoja asiye na hatia na kujeruhi wengine wawili,” alisema.

Alisema kwa mauaji hayo na mengine katika maeneo mbalimbali nchini, Serikali ya CCM kupitia vyombo vya dola inaendelea kukiuka ibara ya 14 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambayo inatambua kwamba uhai ni haki ya msingi wa raia wote.

Mnyika alibainisha kuwa, hawakubaliani na hatua zilizochukuliwa na serikali mpaka sasa kuhusu tukio husika pamoja na maelezo yaliyotolewa na Waziri Nchimbi juzi, ambayo alidai kwa sehemu kubwa yametokana na taarifa zisizo za kweli kutoka polisi.

“CHADEMA haina imani na timu iliyoundwa na Mkuu wa Jeshi la Polisi kuchunguza tuhuma za askari kufyatua risasi na mabomu ya machozi na kusababisha mauaji kwa kuwa tayari serikali na jeshi hilo wametoa maelezo yenye kutofautiana kwa kiwango kikubwa,” alisema.

Kwamba wakati serikali na polisi wakisema kuwa marehemu alikutwa umbali wa mita 300 na kupelekwa hospitali na wasamaria wema, mashuhuda wameeleza wazi kuwa askari walifika jirani na eneo lake na ofisa mmoja akaonesha ishara, na ndipo mabomu ya machozi na risasi za moto zikafyatuliwa na mojawapo kumpata na kudondoka.

Mnyika alidai kuwa mashahidi wote waliohojiwa wanaeleza kwamba bunduki ya polisi ndiyo ilielekezwa na kufyatuliwa kwa marehemu, maelezo pekee yanayotofautiana ni kuwa baadhi wameeleza kuwa ni bunduki ya risasi za moto na wengine wameeleza kuwa ni bunduki ya kufyatulia mabomu ya machozi.

Aliongeza kuwa sababu zilizotolewa na serikali kuwa polisi walizuia maandamano ya CHADEMA mkoani Morogoro kwa sababu ya sensa ya watu na makazi si za kweli kwa vile sababu pekee zilizotolewa ni ufinyu wa barabara na kuwa yalipangwa siku ya kazi.

Kwa mujibu wa Mnyika, ushahidi wa suala hili ni barua ya Jeshi la Polisi ya Agosti 23, 2012 yenye Kumb. Na. MOR/A.25/1/VOL.II/202 na kwamba polisi mkoani Morogoro ndio waliacha kuheshimu utawala wa sheria na makubaliano yaliyofikiwa baada ya mazungumzo ya pande zote.

“Kwa kuzingatia utofauti mkubwa baina ya maelezo yanayotolewa na serikali na Jeshi la Polisi kuhusu matukio husika na ukweli halisi ulivyotokea, CHADEMA kinasisitiza kuwa uchunguzi huru ufanyike kwa mujibu wa sheria ya uchunguzi wa vifo sura ya 24 ya sheria za Tanzania,” alisisitiza.

Wajitetea Moro
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro, Faustine Shilogile alisema kuwa matokeo ya uchunguzi wa tukio hilo, yalionesha kwamba jeraha lililokuwa kichwani kwa marehemu lilitokana na kugongwa na kitu kizito kilichorushwa na si risasi.

Alisema kuwa uchunguzi huo ulifanywa na madaktari wawili wa mkoani humo pamoja na Dk. Ahmed Makata kutoka jijini Dar es Salaam na kushuhudiwa na mwanasheria wa CHADEMA, Aman Mwaipaya na baadhi ya askari.

Kamanda Shilogile alisema kuwa baada ya matokeo hayo ya daktari, polisi sasa wanaendelea na uchunguzi wa kubaini kitu hicho kilichorushwa na kusababisha kifo cha kijana huyo.

Alisema kuwa baadaye Jeshi la Polisi litachukua hatua za kisheria kwa askari ama mtu mwingine atakayebainika kuwa alirusha kitu hicho, ikiwa ni pamoja na kumkamata kiongozi wa CHADEMA aliyechochea maandamano hayo yaliyozua vurugu.

Kamanda Shilogile alisema kuwa ili kubaini hayo yote, serikali imeunda tume ya kuchunguza na kwamba inayoundwa na askari polisi na watu wengine ambao watasaidia kukamilisha uchunguzi huo.

Aliongeza kuwa tume hiyo ambayo tayari imeshafika mkoani Morogoro itatafuta maelezo na ushahidi kutoka kwa watu mbalimbali walioshuhudia tukio hilo, wakiwemo wanahabari na hivyo kuwaomba wote watakaohitajika kutoa ushirikiano.

Kuhusu majeruhi Hashimu Seif aliyejeruhiwa mguu katika vurugu hizo, Shilogile alisema kuwa uchunguzi umebaini kuwa alijeruhiwa na bomu lililomuangukia mguuni na kwamba anaendelea vizuri ikiwa bado yuko hospitali ya mkoa kwa matibabu zaidi.

Wadaiwa kumtesa mtoto
Katika hatua nyingine jeshi hilo Mkoa wa Manyara, limeingia katika kashfa nzito likidaiwa kumpiga na kumuumiza vibaya mtoto wa kiume, Kadogoo Kalanga (16), ambaye kwa sasa amelazwa katika Hospitali ya Selina kwenye chumba cha uangaliazi maalumu (ICU) akiwa hajitambui.

Mtoto huyo ambaye taarifa za polisi juu ya kilichompata zinatofautiana, yuko mahututi akiwa amevimba sehemu za siri na nyuma ya kichwa (kichogoni).

Kamanda wa Polisi mkoani humo, Akili Mpwapwa alisema kuwa mtoto huyo alipatwa na hali hiyo baada ya kufikishwa kwenye kituo cha polisi cha Orkasumeti wilayani Simanjiro kwa tuhuma za wizi wa mbuzi wawili na kupandisha mori, na hivyo kujipigapiga chini hali iliyomsababishia kupoteza fahamu.
Hata hivyo, maelezo yake yanapingana na polisi waliompeleka mtoto huyo kwenye kituo cha afya Orkasumeti, ambao waliwaeleza madaktari kuwa alipata ajali ya pikipiki.

Daktari aliyempokea mtoto huyo kituoni hapo, aliyejitambilisha kwa jina moja la Ester, alimweleza mwandishi wa habari juzi kwa njia ya simu kuwa, mtoto huyo alifikishwa hapo Jumatatu wiki hii na askari ambao walimweleza kuwa alipata ajali ya pikipiki.
Alisema kuwa walimpa huduma ya kwanza, lakini kutokana na hali aliyokuwa nayo ya kutojitambua, walishindwa kubaini anaumwa wapi, hivyo siku iliyofuata akashaurina na madaktari wenzake wakaamua kumpa rufaa kwenda hospitali yenye vifaa kwa ajili ya vipimo zaidi.

Kamanda Mpwapwa alipoelezwa kuwa taarifa yake inatofautiana na ile ya askari wake kwenye kituo cha afya, aliendelea kusisitiza kuwa taarifa anazotoa ni zile alizopewa na Mkuu wa Polisi (OCD) wa Wilaya ya Simanjiro, na kwamba kama inatofautiana na nyingine hilo halimuhusu.

“Maelezo ninayokupa mimi ni yale niliyopewa na OCD wangu, kama kuna “contradiction” (mkanganyiko) kati ya taarifa niliyopewa na ambayo imetolewa mahali pengine hilo si tatizo langu,” alisema.
Naye mama wa mtoto huyo, Paulina Kalanga, aliwaeleza waandishi wakati akisubiri mtoto wake apatiwe matibabu kwenye hospitali ya Selian kuwa, alipata taarifa kwamba Kadogoo yuko kituo cha afya saa tano asubuhi ya Jumatatu na alipofuatilia alimkuta akiwa hajitambui.

Alisema madaktari walimweleza kuwa mtoto huyo alipelekwa hapo na askari polisi watatu na alipomkagua akishirikiana na ndugu zake, walibaini kuwa ameumizwa vibaya sehemu za siri ambazo zimechubuka na kuvimba, huku kaptula aliyokuwa ameivaa ikiwa imelowa mkojo na kuchanika eneo la katikati.

Paulina aliongeza kuwa, tangu wakati huo hadi jana asubuhi mtoto huyo hajaongea zaidi ya kuzungusha kichwa sana wakati fulani, hali inayomlazimu amsaidie kukishikilia kuepuka asijiumize.

Alisema kuwa mtoto huyo anaonekana kuumia kila anapoguswa maeneo ya nyuma ya kichwa, kwenye mbavu na kwamba anahisi mfumo wake wa haja ndogo huenda umepata tatizo kwani tangu Jumatatu hapati choo kidogo licha ya kuwekewa chupa kadhaa za maji ya kumwongeza nguvu mwilini.

Kadogoo alilazimika kuhamishiwa katika Hospitali ya Agha Khan ya mjini Arusha kwa kutumia gari la wagonjwa la Halmashauri ya Wilaya ya Simanjiro lenye namba za usajili SM 5004 ili kufanyiwa kipimo cha kichwa, CIT SCAN.

Mama mzazi wa mtoto huyo pamoja na ndugu wengine waliokusanyika hospitalini hapo, walieleza masikitiko yao juu ya kitendo hicho cha kinyama wakidai mpaka sasa polisi imeshindwa kuwapa namba ya taarifa iliyofunguliwa kwao (RB) kuhusu kosa linalomkabili Kadodoo.



[TD="bgcolor: #ffffff"]
Ngoma nzito Polisi
• Wadaiwa kumfanyia mtoto unyama wa kutisha Manyara

na Waandishi wetu
Tanzania Daima



[/TD]
[TD="width: 140, bgcolor: #ffffff"] [/TD]
 
Umeyaona ya shekh PONDA tu, ya maasikofu hujayaona kweli wewe huiwezi siasa!!Waislam wanahaki ya kudai kipengele cha dini ktk sensa.kwanini wadai tembelea web hizi upate reference
1) www.wikipedia.com/tanzania
2) www.arc.com/tanzania

web zote hzo zinatoa idadi ya watanzania kwa mujibu wa dini yao wakati tangu 1967 watanzania hatuja hesabiwa kwa mjibu,wa dini zetu.swali hawa WA RC Takwim hz wanazitoa wapi????
unajua makanisani kuna utaratibu mzuri wea kufahamiana kwa mafano wakristu wote huwa wanabatizwa na vyeti ivyo hutunzwa makanisani ambavyo ni sawa na vyeti vya kuzaliwa...vilevile makanisa yana utaratibu wa jumuiya ndogondogo za kikristo ambapo watu wa mtaa mmoja hukusanyika kusali pamoja na idadi yao huwekwa kwenye kumbukumbu za jumiya husika hivyo ni rahisi kupata idadi yao kutumia kumbukumbu hizo
 
Nimeshavgunduwa,waislam nyie ni ndugu zetu,hamkupata mwakilishi mzuri kuwa rais.Ni muhimu tushirikiane ili makosa yasijirudie.Asante.

Kwauzushi wako na chuki ulonayo juu yawaislam hutapata muislam atakaeungana nawe ilo sahau....bs nanyinyi fanyeni CDM Kama ccm Kama ulivyoelezea huko nyuma sasa ivi zamu ya muislam kwa urais CDM au iyo ngumu kumeza?
 
Nimeshavgunduwa,waislam nyie ni ndugu zetu,hamkupata mwakilishi mzuri kuwa rais.Ni muhimu tushirikiane ili makosa yasijirudie.Asante.
Tuleteeni bs muwakilishi mzuri wa kislamu kutoka CDM 2015
 
Yeye kaukuza zaidi ndio maana tumefika hapa tulipo!

kwanza kabisa napenda kukufahamisha kuwa jk sio mdini kama unavyofikiri japokuwa nakubaliana na wewe kwamba udini upo.na huo udini haukuanza katika kipindi hiki cha jk,bali ulianza tangu kipindi cha awamu ya kwanza ya mwalimu nyerere,na kisha kushika kasi kubwa kipindi cha mkapa.na siku zote pale ambapo waislam watasimama ktk kudai au hata kuhoji tu kuhusu haki zao mbalimbali basi neno udini huingizwa.nakupa mifano miwili tu miongoni mwa mifano mingi.mfano wa kwanza;kulikuwa na nini hasa zaidi hata serikali kuingia mkataba wa siri na kanisa katoliki na kuridhia kutoa mabilioni ya shilingi kulisaidia kanisa kila mwaka[1992 hadi 2090],hali ya kuwa kuna dini nyigine pia?huo sio udini?jambo la pili ajira na nafasi mbalimbali za utawala.ni watu wa dini fulani ndio waliojaa huko[lifanyie utafiti mdogo tu kulitambua]je huo sio udini?
jambo la kufanya ili kuweka mambo sawa ni kuondoa dhulma hizo nilizotaja na nyiginezo na kuleta usawa katika masuala mbalimbali yanayohusu jamii nzima ya watanzania.
 
Na imeletwa na campaign manager wa udini na ukabila humu jamvini wa CCM

Kuna thread humu inasema "kashfa ya chadema na kanisa katoliki"imeletwa na wafuasi wa JK!mbona sioni "Kashfa ya ccm na kanisa katoliki" kwenye issue ya malalamiko ya Mou?Huo ndo udini wenyewe sasa.Ni vyema viongozi muwapime kutokana na matendo kwa nchi ya kimaendeleo na si kwa kutizama ni dini gani!
 
Unaye mtetea ni jk wa tz au una jk wako mwingine?

udini wa jk ulikuja baada ya kuanza kuwapa nafasi Muslim serikali Hilo liliwakera sana inajulikana tafuta jingine nitamuhukumu jk kwa mengine bt udini nichuki mlizopandikiza nyinyi wakristo lakini tumeshawastukia na Kama unataka kumtoa jk kabla ya 2015 siuazie mtaani kwako unapokaa hamasisha na jiranizako muende na mtaa wa pili na watatu anza usiku huu bila kuchelewa si unauchungu na nchi yako
 
THE BEST PRESIDENT AMBAE HAJAWAHI TOKEA TANZANIA.Ukweli ndo huo.

Sijui kama hapo kwenye red umekosea au vipi?
Ila mimi naona JK ni 'the worst president' ambaye hajawahi tokea.
Kwa nini? Kwa sababu zifuatazo:-
  • Hakujawahi tokea serikali ta Tanzania kuanguka kwa sababu ya kashfa ya rushwa. Ila imetokea kwa JK.
  • Haijawahi tokea nchi ikawa na 'ugonjwa' mbaya sana wa ufisadi na rushwa. Ila imetokea kwa JK.
  • Haijawahi tokea nchi ikawa na ubaguzi wa kidini wa hali ya juu sana. Imetokea kwa JK.
...
... Ongezea nyingine hapa ...
 
kweli huyu jamaa ni mdini, angalia wizara ya mambo ya nje wafanyakazi wengi hasa wa kipind chake ni wakina salama leikum!
 
Unaye mtetea ni jk wa tz au una jk wako mwingine?

Uyouyo anaezungumzwa hapa ...Ndio maana WAislam hawataipigia kura ilo lichama lenu sijui mtashinda vipi .hata mkisimamisha muislam hataivyo haiwezekani kumsimamisha kwa udini wenu
 
BAK, nakubaliana na wewe kuwa hizi vurugu zinazoendelea zinazidi kupanda mbegu ya chuki.

Je hudhani kama kuna namna ambayo tunaweza kujisahihisha kabla mauaji haya hayajafikia hatua kubwa zaidi??

Je, vyombo vya habari havina nafasi katika hili????

Huwa najiuliza sana sipati majibu, kwa nini vyombo vya habari na au wanahabari wanakubali kutumiwa??
Tena wakati mwingine, wanatumia wazi kabisa pasipo kificho, je tufanye nini?? Au tujirekebisheje?? Uzalendo urudishweje kwa wanahabari??

Katika nchi changa kama TZ ambayo ukomavu/uelewa wa wanachi wake kwa asilimia kadhaa bado ni 'simama dede', mie huwa sipuuzii nafasi ya wanahabari. Natamani tuwe na wanahabari wanaoweza ku-take lead katika hili. Ila wasianze finger pointing maana hapo hatutafikia muafaka.

Kuna umuhimu wa kuundwa chombo/kamati/task force au sijui nini kwa ajili ya kuchunguza kwa kina wapi tulipo katika suala zima la amani ya nchi. Na chombo hiki kisisimamiwe wala kujihusisha na serikali bali kiwe cha wananchi wenyewe na makundi ya dini zote. Nafasi ya serikali ni kukitambua na kukipa uhuru chombo hiki ili kiweze fanya kazi zake. Hapa tunaongea zaidi kwa kuona viashiria kama vya mauaji, lakini tunahitaji uchunguzi zaidi wa wapi tulijikwaa.

Na kingine, pande zote inabidi tuvuke mpaka fulani tuliojiwekea ili tuwe tayari kupokea ukweli mgumu 'bitter truth' utaopatikana baada ya uchunguzi na kuwajibika kama timu moja. Nachohofia au nachokiona ni kuwa, hata tukiamua kama taifa kushighulikia hili suala, tuko tayari kupokea ukweli kama ukweli mtupu bila kusema hawa wanatuonea au hawa walipendelewa au hawa vile.

Bila kujua tulijikwaa wapi na kukubali kweli itakuwa ngumu ku-move forward.

Thank you very very much for this post.Hakika it is extremely useful!

Kweli wewe dada una akili!Anyways,nadhani wachangiaji kama ni kweli wanapenda umoja wa kitaifa uendelee,basi wanahitaji mawazo kama haya.Mawazo ambayo yamepelekea jukwaa hili na forum kuitwa "The home of great thinkers"

Nashukuru sana kwa mchango wako huu,na hopefully members watakaochangia,watakuwa na mwelekeo kama huu.Thread hii si ya kutugawa watanzania.

Bali ni ya kuangalia ni wapi tumejikwaa,ili tulimalize tatizo hili kabla haijawa too late.Mawazo kama haya na ushauri pamoja na nasaha hizi ni muhimu kuliko vile ambavyo maneno yangu yangeweza kuelezea.

Tuko pamoja!country first!adui ni ccm na JK wenye kueneza udini kwa kutumia mgongo wa watanzania.
 
Last edited by a moderator:
Udini utatumaliza. Yuliozaliwa katika familia mchanganyiko za kidini tunaona watu wana-complicate sana maisha!
 
JK kusema kweli ni mtu ambaye alikuwa anataka tu awe RAIS BASI! hakuwa na ajenda nyingine kichwan mwake zaidi ya kupata urais na kutimiza yale anayoona kwake ni ya manufaa, si zaidi ya hapo! JK amekuwa ni rais anaependa watanzania kugawanyika ki makundi makundi hasa ya udini. Mungu tuepushe na balaa hili lililoletwa na JK!
 
Kweli, natamani kuwe na task force ya kitaifa
Inayojumuisha makundi mbali mbali hasa ya kiimani, kila kundi kwa hiari yao
Na kuwe na wanahabari wenye uzalendo
Tuweze kuwa hata na slogani za 'Utaifa kwanza'
Na ziwe nyingi ambazo wanahabari wanasaidia kuzipenyeza kwa watu

Serikali wala viongozi wasijihusishe maana wanaweza wakaingiza interest zao
Kisikubali kutumiwa na kundi lolote la kisiasa

Bottom line, lazima tufanye jambo fulani kabla hatujachelewa kwa ajili ya nchi hii

Msinisahau haya ujumbe tu (joking 🙂 )

Ha ha ha, asante kwa kutambua post yangu, siku zote huwa niko 'confused' hapo red pamenitia moyo

Thank you very very much for this post.Hakika it is extremely useful!

Kweli wewe dada una akili!Anyways,nadhani wachangiaji kama ni kweli wanapenda umoja wa kitaifa uendelee,basi wanahitaji mawazo kama haya.Mawazo ambayo yamepelekea jukwaa hili na forum kuitwa "The home of great thinkers"

Nashukuru sana kwa mchango wako huu,na hopefully members watakaochangia,watakuwa na mwelekeo kama huu.Thread hii si ya kutugawa watanzania.

Bali ni ya kuangalia ni wapi tumejikwaa,ili tulimalize tatizo hili kabla haijawa too late.Mawazo kama haya na ushauri pamoja na nasaha hizi ni muhimu kuliko vile ambavyo maneno yangu yangeweza kuelezea.

Tuko pamoja!country first!adui ni ccm na JK wenye kueneza udini kwa kutumia mgongo wa watanzania.
 
Nchi ilipofikia,credits huwa anapewa rais na serikali yake,kwahili la udini,hakuna ubishi umeshaota mizizi.Na sijawahi kusikia kauli ama vitendo kutoka kwa JK vya kukemea haya mambo ya udini.

Kinachonifanya niamini ni JK,ni kwasababu hao wanaopinga kasi ya upinzani,wanapoijibia serikali ya ccm,basi wanaoonyesha chuki za wazi kabisa za kidini.Ule udugu tuliokuwa nao wakitanzania haupo tena,na sijui utarudi kwa njia gani.

Kuna habari kuwa hata mtu na mke wake wanataka kutoana roho kwasbabu hizo hizo.Sheick Ponda alipotoa kauli kinyume na yakwake kuhusu sensa,kaliachia na gazeti lenye kusambaza sumu hizo huku akilifungia lenye kusema ukweli(mwanahalisi)

Ninamini kabisa kuwa tulipofikia,uwezekano wa kuingia kwenye vurugu na mapigano ya kidini ni mkubwa kuliko wakati wowote ule kwenye historia ya Tz toka tupate uhuru.

Kama JK ni mdini,tufanyeje?Ni wazi anapenda haya yaendelee kuwepo kwasababu ni kama anauwa ndege wawili kwa jiwe moja,yani kwasababu yeye ni fisadi na mdini,basi issue za ufisadi wake anazifukia kwa kupenyeza sentiments za kidini kwasababu anajuwa the issue is extremely sensitive.

Je kama taifa tutapona dhidi ya udini huu wa JK?je kukitokea mapigano,nani atakuwa responsible?Je nini kifanyike kukomesha udin8I hu?ama tumeridhika?!....

Ukweli kaka tunakoelekea na udini ni kubaya tusipopata viongozi wa kutuongoza kuondokana na janga hili kama wananchi tutashindwa kujiongoza wenyewe. Kaka kuna kitu kilinisikitisha sana kilitokea UDOM mwaka jana kama sikosei, kuna mdahalo uliandaliwa na waislamu pale chuoni na kichokuwa kikijadiliwa na UDINI mtupu na mikakati ya ajabu ya kidini na kupandikiza chuki dhidi ya ukristo, walienda mbali na kudai watakwenda Butiama kumsomea hukumu baba wa Taifa kwa makosa aliyowafanyia waislamu. wakajadili na mikakati ya kuendelea kukaa ikulu eti wakidai kanisa haliwezi kuruhusu kibaragashia kuendelea tena miaka kumi pale white house, hivyo wamejipanga vema na kamili kwa mapambano mwaka 2015! ni kikao ambacho katika nchi isiyo kuwa na dili kama yetu kuruhusiwa kuandaliwa na tena wanaojfanya mjadala ni walimu wa vyuo. kwa kweli ni hatari sana kaka! na kwa haya siju JK amajiandaa kwa legacy ipi atakapo toka madarakani!
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom