Kwa lipi Lowassa apewe nchi?

Kwa lipi Lowassa apewe nchi?

Jamani katika canditates naona lowassa is the best kwanza anadare kila mtu Ana mskosa yake hata kwenye ile ishu ya radar hatujui what really hapened lakini hakudare kungangania alijitoa ujue ni kiongozi ambae anaweza akafanya maamuzi magumu kiukweli namkubali lowassa and nimeona pia ni mtu ambae anamkimbilia Mungu ni Mara nyingi nimemuona kwa TB Joshua hamna binadamu aliekamalika hata Kama Ana madhaifu yake but naamini lowassa ni kiongozi ambae hapelekeshwi na mtu let's jamani watanzania tusipelekwe na upepo but tufikirie kwa makini
 
Makelele bila hata mpango ! Umeulizwa swali rahisi mno , apewe urais kwa lipi na hiyo mijikashfa inayomuandama ? Kwanza aliwahi kufanya nini cha kupigiwa mfano ?

Tupe unayemtaka ambaye alishafanya cha kupigiwa mfano....usiropoke tu...wala usimkatae tu kwa maneno ya vijiwe vya wala unga...
 
Tupe unayemtaka ambaye alishafanya cha kupigiwa mfano....usiropoke tu...wala usimkatae tu kwa maneno ya vijiwe vya wala unga...

mwingine huyu ! , haya na wewe weka mazuri ya lowasa ambayo ni ya kuigwa , huna hoja ni bora utulie tu , huyu hata ukimloweka na jiki mwezi mzima hawezi kutakata .
 
Huku Arusha Kuna Vijana Wenzangu Wanaandika Magari Yao Binafsi
TEAM LOWASSA
LOWASSA NEXT PRESIDENT
Mimi Sijajua Malengo Yao
 
Si uwaulize kukimbilia JF wakati walioandika upo karibu nao kutakusaidia nini?
 
Ndugu watanzania msiogope kelele na nderemo za team Lowasa maana serikal haiwez pitisha jina la mtu atakaye leta visas na kupoteza uzalendo wa wana usalama wetu, haijawah tokea nakama imewah tokea ni Misri ila at the end jesh lilichukua nchi na Morsi wanamnjonga. Lowasa hana umaarufu wa mh Mrema hivyo hawez kukisumbua chama na idara za usalama. Wanachokifanya wanakijuwa na muda ukifika wa Tz mtapata kiongoz.
 
  • Thanks
Reactions: gsu
Binafsi namawazo tofauti sana na baadhi ya watu humu JF na hata mitaani!
Sikatai mh.Lowassa kachafuka na labda ni kweli hasafishiki na kashfa aliyonayo ya RICHMOND.
Sikatai mh.Lowassa ni mlafi wa.madaraka.
Sikatai mh.Lowassa akiingia madarakana wengi watalia hasa wabaya wake.
Sikatai mh.Lowassa labda kweli kajilimbikizia mali zisizo halali.
Sikatai mh.lowassa kweli haaminiki na watanzania wengi kwakuwa ya maneno mengi mabaya yasemwayo

Lakiniiiiiii pia sikatai Lowasa.ndio kiongozi anayetakiwa kuitoa nchi hapa ilipo kwenda mbele......
Pia sikatai Lowassa ndiyo mtu mwenye msimamo na mtoa maamuzi yenye tija kwa nchi hata kama ni magumu vipi.
Ni kweli pia tukimpima Lowassa na wagombea wengine wa ndani ya chama chake na nje...anawazidi kwa uwezo!mwenye kubisha na abishe kuhusu hilo!!
Ni kweli pia usiopingika kuwa endepo UKAWA watasimamisha sura mpya kwenye uraisi asiwe mbowe,mbatia,wala slaaa,wala proff. Na wakaanza kumnadi mapema mgombea huyo machoni pa watanzania nitakuwa wakwanza kupanga mstari wa kupiga kura saa 12 asubuhi...
All in all Lowassa is the best option we have right now!!!!(katiba inaniruhusu kutoa mawazo binafsi)
 
Ukifikiria kwa kutumia tumbo,

lazima utakuwa na mawazo kama hayo.

Imagine rais lowasa
PM- karamagi
Nishati- ngeleja
Miundo mbinu- mkigoma
Elimu- chilolo
Hahahaha
 
Hivi Lowassa akiwa rais nani ataongoza nchi? Maana kuongea tena hawezi, Anapoteza kumbukumbu kwa kiasi kikubwa na hawezi kusimama kwa dakika 30! Nyie mnacheza kweli! Lowassa ni mgonjwa mno!
 
Binafsi namawazo tofauti sana na baadhi ya watu humu JF na hata mitaani!
Sikatai mh.Lowassa kachafuka na labda ni kweli hasafishiki na kashfa aliyonayo ya RICHMOND.
Sikatai mh.Lowassa ni mlafi wa.madaraka.
Sikatai mh.Lowassa akiingia madarakana wengi watalia hasa wabaya wake.
Sikatai mh.Lowassa labda kweli kajilimbikizia mali zisizo halali.
Sikatai mh.lowassa kweli haaminiki na watanzania wengi kwakuwa ya maneno mengi mabaya yasemwayo

Lakiniiiiiii pia sikatai Lowasa.ndio kiongozi anayetakiwa kuitoa nchi hapa ilipo kwenda mbele......
Pia sikatai Lowassa ndiyo mtu mwenye msimamo na mtoa maamuzi yenye tija kwa nchi hata kama ni magumu vipi.
Ni kweli pia tukimpima Lowassa na wagombea wengine wa ndani ya chama chake na nje...anawazidi kwa uwezo!mwenye kubisha na abishe kuhusu hilo!!
Ni kweli pia usiopingika kuwa endepo UKAWA watasimamisha sura mpya kwenye uraisi asiwe mbowe,mbatia,wala slaaa,wala proff. Na wakaanza kumnadi mapema mgombea huyo machoni pa watanzania nitakuwa wakwanza kupanga mstari wa kupiga kura saa 12 asubuhi...
All in all Lowassa is the best option we have right now!!!!(katiba inaniruhusu kutoa mawazo binafsi)

Who's we?
 
Mwalimu Nyerere alisema 'Hapa hatumchagui mtu maarufu ,tunamchagua mtu safi na huyu si safi ambaye hapo alimlenga Lowasa.Kama unapenda sura yake basi nenda kanywe naye chai.Wengine wanasema aah ni tuhuma tu.
Samueli Sitta]Yusufu Makamba ]mnasisima hapa mnasema ni tuhuma ,tuhuma tu.Lakini mtakumbuka mke wa kaisari alipotuhumiwa kwa ugoni Kaisari akaagiza uchunguzi ufanyike .Uchunguzi ukafanyika ikabainika kwamba sio kweli.Lakini Kaisari bado akamuacha ,akasema mke wa kaisari hapaswi hata kutuhumiwa .
Na sisi hapa mgombea wetu hapaswi hata kutuhumiwa .wakati wapo wengine safi ambao hawana tuhuma.
Kama mkimteua huyo mimi sitapiga kampeni .Siko tayari kumsafisha mtu matope ndio nimuombee kura
Hapana kabisa.Huyu mimi namjua si msafi na nchi nzima inajua siyo msafi.hafai kuwa mgombea wetu'Mwl.Juliasi Nyerere NEC dodoma ,Juni 1995.
Nimeona niandike hayo maneno hapa kwani yana faida kubwa sana kwa watanzania wanaiotakia mema nchi yetu .Nyerere hayupo duniani tena lakini maneno yake na wosia wake utaendelea kudumu daima.
CCM lazima mtambue IKULU SIYO PANGO LA MAFISADI .
CCM lazima mtambue IKULU SIYO WODI YA WAGONJWA.
CCM lazima mtambue Mwalimu Nyerere aliwahi kusema watanzania wanataka mabadiliko wakiyakosa ndani ya ccm watayatafuta nje ya ccm sasa ni wakati muafaka kwa watanzania kutafuta mabadiliko nje ya ccm.
 
Hivi Lowassa akiwa rais nani ataongoza nchi? Maana kuongea tena hawezi, Anapoteza kumbukumbu kwa kiasi kikubwa na hawezi kusimama kwa dakika 30! Nyie mnacheza kweli! Lowassa ni mgonjwa mno!

Hata ukiweka pembeni ugonjwa wake na udhaifu mkubwa wa kujieleza na kutojua kwake kiingereza....HUYU NI JAMBAZI SUGU NA FISADI PAPA AMBAYE KAMWE HAWEZI KUWA RAIS WA TZ
 
Hivi Lowassa akiwa rais nani ataongoza nchi? Maana kuongea tena hawezi, Anapoteza kumbukumbu kwa kiasi kikubwa na hawezi kusimama kwa dakika 30! Nyie mnacheza kweli! Lowassa ni mgonjwa mno!

huo ndo ukweli ingawa wapambe hawataki kusikia.
 
Back
Top Bottom