EDWARD LOWASSA THE HOPE WE DESERVE...
Ikiwa imesalia miezi michache kuanza kwa mchakato wa kuchukua form Za Kugombea URAIS kwa chama cha Mapinduzi (CCM),yapo Majina mengi yanayotajwa Nani atakaye mrithi Rais anayemaliza Muda wake Dr Jakaya Mrisho kikwete ,katika kukiwakilishaa chama katika MBIO Za URAIS hapo mwakani 2015, Mh Edward Ngoyai Lowassa ,
mmbunge wa monduli anaonekana na anatajwa sana na vyombo mbalimbali vya habari ndani na nje ya nchi pia wachambuzi na wataalam tofauti wa kisiasa pamoja na wananchi wa rika mbalimbali Kuwa ni kiongozi mwenye mvuto mkubwa ndani ya chama na pia nje ya chama (ana sifa ya kuuzika kwa wananchi),endapo Halmashauri kuu ya Chama itapitisha jina lake Kama mgombea wa nafasi ya URAIS mwaka 2015 kupitia CCM ..kutokana na sifa zake kiutendaji pamoja na uadilifu wake Kama kiongozi ambaye anatamani kuleta usawa miongoni mwa watanzania Wote ikiwa ni moja ya ajenda zake kuu .
Kwa mtazamo Edward Lowassa ana upeo wa Hali ya juu katika kufanya maamuzi katika utendaji na ni mtu makini mwenye uwezo wa kudhibiti mambo na kuhakikisha wananchi Wa Hali ya chini hawaumizwi na mfumo uliopo ,hupenda Kuilinda haki kwa watu Wote.
Ni kiongozi anayeumizwa na umaskini wa watanzania ,nnaweza kusema anauchukia umaskini : ni adui mkubwa wa maendeleo ya nchi yetu, asilimia kubwa ya watanzania ni maskini Kama akiwa Rais anapendelea kuubadili mfumo uliopo na kuhakikisha wananchi wa tabaka la chini wanapata ELIMU bora yenye ufanisi ambayo itawakomboa kutoka katika umasikini ,ni Lazima tuufute ujinga unaoleta umaskini kwa kutoa elimu Bora kwa Wote yenye tija katika kuleta maendeleo ya Taifa letu.
Asilimia 80% ya watanzania ni wakulima ,Lazima waelimishwe Kwanza ndipo tuweze kufanya mapinduzi ya kilimo Kama mkulima hatapewa elimu Bora ni sawa na kazi Bure .
Edward lowassa ni mwenye matumaini zaidi ,na mwepesi kujaribu yote yameonekana na kujitokeza katika nafasi mbalimbali alizokwisha kuzitumikia na anazozitumikia ,Tanzania ni nchi yenye utajiri wa rasilimali ,kiongozi aina ya Lowassa anahitajika kuzisimamia kuleta ubunifu kwa manufaa ya watanzania Wote , watanzania waonyeshe bidii na kufikiri na kuufanyia kazi huu utajiri wetu.
Hakatishwi tamaa na mikono michafu na faulo anazochezewa juu yake ,ikumbukwe mwaka (2008) alijiuzulu kutoka na siasa chafu na kushindwa kuwajibika kwa watendaji waliopo chini yake, hata ripoti ndefu ya mwakyembye iliyokuwa na sintofahamu haikuwahi kumuhoji kuhusiana na usainishwaji wa mkataba ule katika wizara ya Nishati ,Aliyajali maslahi ya umma Wala hakuyumbishwa na yeyote Ila aliamini anawajibika kutokana na fitina zilizotengenezwa juu yake .
Edward Ngoyai Lowassa aliyezaliwa kijiji cha ngarashi ,hapendi upambe kwasababu wapambe ni wabaya anaamini Ndiyo huingiza nchi katika Rushwa ,ndiyo watakaoiyumbisha nchi kwasababu ni watu Wenye kujali maslahi binafsi ,wasiojali juu ya athari zinazoikumba jamii.
Mwingi wa uvumilivu na kiongozi asiye na chuki Wala kisasi Hapa tunampa sifa watoto wa mjini wanamwita mwanaume wa shoka..basi usalitibhaukuanza Leo upo tangu zama Za yesu ,waliompiga made wapo huru mitaani na lowassa pia anaishi Wala si mwenye kisasi juu yao ,huibeba sifa ya huvumilivu Kama kiongozi
Vilevile ana maadili sifa ya kupendwa na kuheshimiwa na Wote ni kiongozi hupendelea kujadiliana mezani ,Kama tulivyoona hapo mwanzo sio mgovi ni msikivu na mwerevu sifa hizi huonekana hata pale anapongea ni mtu wa adili njema ana sifa ya kuheshimu DINI Zote na mwenye kusaidia wengine Wenye Shida
"Kama tunataka kubadilisha maisha ya wananchi Lazima tuwapatie mazingira sahihi yatakayowapelekea kujenga Taifa imara lenye nguvu"
Edward Ngoyai Lowassa ni kiongozi anayefikiria zaidi kuijenga Tanzania imara yenye inayokuwa kwa kasi kiuchumi kivitendo na Wala si kinadharia (hizi)kwa kufufua viwanda viliyokuwepo pamoja na vipya vitakavyoanzishwa ili kuweza kupanua soko la AJIRA Hapa nchi yapo mambo mengi ya msingi ya kuzingatia ili kuweza kuleta ufanisi katika ukuaji wa uchumi.
Lowassa ni kiongozi mwenye majibu juu ya matatizo ya watu yanayowakabili ana maono mapya katika safari yake ya matumaini ,hutamani Kuwa mtetezi wa wanyonge na kufuta vilio vya maisha fini wanayoishi watanzania
Lipo Tumaini kwa Watanzania juu ya EDWARD NGOYAI LOWASSA a.k.a LEIGWANAN ni mcha mungu anayeamini hatima ya maisha yake Ipo mikononi mwa mungu ,kwani hekima ,busara ,pamoja na maarifa yake Edward lowassa yametokana na ucha mungu wake...