Kwa lipi Lowassa apewe nchi?

Kwa lipi Lowassa apewe nchi?

Mwacheni Lowassa augue vyema, mtu hata kula hawezi sembuse urais?
 
Natamani utengamano wa nchi za AFRIKA uwe kama ule wa Umoja wa Ulaya ili Mzee wetu huyu akichukia nchi sisi waona karibu tuhamie DRC.
 
Nchi imekuwa ikiongozwa kama social sports and entertainment orgnization huku jk akiwa kama mc asiyependa kumbugudhi yeyote anaekula good tym, walio nje ya organization, not his problem. Lowasa ana trait za kutoleta mzaha wala kumchekea yoyote anaeharibu kazi, pia huwa misimamo yake ipo wazi, sio muumini wa huu ni upepo tu, utapita kama mengine yalivyopita. Kwa Lowassa ni action Now.
 
Lowasa anakosa vigezo vyote vinavyotumika na ccm kupata mgombea.

1) haijawahi tokea na wala haitatokea Ccm ikachagua mtu ambaye sio waziri. CCM ina desturi ya kuchagua mrithi ndani ya wale minute 12.

2) Pinda akigombea anawameza Sumaye na Lowasa ambao wangefikiriwa kwa nyazifa za uwaziri mkuu.

3) Afya ya Lowasa inatosha kuacha kujadili jana lake. Parkinson na dementia ukiachia mail alcoholism ni magonjwa hatari maana yanaathiri ubongo kitengo cha matendo ya hiari na kumbukumbu.

4) CCM haitapenda iwe na wakati mgumu kumnadi kiongozi aliyekumbwa na kashifa hadi kujiuzuru. Lowasa inabidi awe kwenye defensive mode badala ya offensive wakati wa kampeni za ndani na nje.

Mwenye macho na asome na aweke kwenye kumbukumbu.
 
hivi wewe upo dunia ya ngapi.Katika kipindi cha miaka 2 aliyokaa madarakani bwana EL kajenga shule za kata kibao,chuo cha dodoma na mradi wa maji wa ziwa victoria kupeleka mikoa ambayo haikua na maji ya shinyanga,simiyu na Geita.Sasa unvosema hajafanya kitu mie nakushangaa sana na kuhusu ufisadi ile hela walipiga watu wengi sana ila yeye ndiye aliyekua mbuzi wa kafara.
Watz tujifunze kuelewa concept jamani..hizi shule za kata kajenga wapi Lowassa?? mie kijijini kwangu nilishiriki kuijenga wala sikumuona Lowassa wala hela yake.ila lilikuwa ni tamko la serikali ambalo lilianzia kwenye mmem na likaingia kwenye mmes na tayari idea ilishakuwaepo toka awamu ya mkapa..
kama mnataka kumpa nchi mpeni lakini hakuna haja ku-exagerate vitu..yee aombe urais kwa ahadi ya kufanyia watz kazi za maendeleo n sio kuchukua ujiko kwenye mambo yaliyopita. cheap politics hazijengi umaarufu.
 
hivi wewe upo dunia ya ngapi.Katika kipindi cha miaka 2 aliyokaa madarakani bwana EL kajenga shule za kata kibao,chuo cha dodoma na mradi wa maji wa ziwa victoria kupeleka mikoa ambayo haikua na maji ya shinyanga,simiyu na Geita.Sasa unvosema hajafanya kitu mie nakushangaa sana na kuhusu ufisadi ile hela walipiga watu wengi sana ila yeye ndiye aliyekua mbuzi wa kafara.

una mtetea mwizi,ccm kumsimamisha lowasa ni kukosa watu
 
Ningetamani sana rais wa awamu ya tano asitokee CCM kwani hakuna msafi hata mtoto mdogo aliyezaliwa kwenye familia ya mwanachama wa CCM.
Wote ndani ya CCM ni tumbili wanakula mahindi ya nchi hii.

Ukisikia tumbili wanagombana usije ukafikiri kwamba wanakemeana wasiibe mahindi bali ujue wanagombania mahindi.

Ikitokea kwa bahati mbaya hii nchi ikabaki chini ya pori la tumbili hawa CCM basi Lowassa anaweza akatumia kushiba kwake na kuwadhibiti tumbili wanaojiandaa kuvamia shamba na njaa zao wakitamani kushiba kama Lowassa.

Fisadi au tumbili mwingine anyeweza ni Pombe Magufuli.Huyu naye ni fisadi mchapa kazi sio kilaza.

Watanzania tusirubunike ndani ya CCM hakuna cha mlokole wala ustadhi wote lao ni moja, kula na kuiba mali za Umma tu huku ubunifu wao ukiwa ziro.
 
hivi wewe upo dunia ya ngapi.Katika kipindi cha miaka 2 aliyokaa madarakani bwana EL kajenga shule za kata kibao,chuo cha dodoma na mradi wa maji wa ziwa victoria kupeleka mikoa ambayo haikua na maji ya shinyanga,simiyu na Geita.Sasa unvosema hajafanya kitu mie nakushangaa sana na kuhusu ufisadi ile hela walipiga watu wengi sana ila yeye ndiye aliyekua mbuzi wa kafara.

Alijenga shule za kata? Lete ushahidi hapa wa kitakwimu alichangia sh.ngapi hizo shule zikajengwa?
 
Alijenga shule za kata? Lete ushahidi hapa wa kitakwimu alichangia sh.ngapi hizo shule zikajengwa?

cha kuongezea tu kwani alitoa pesa yake mfukoni? Si alitumia kodi za wananchi,angekuwa katumia pesa zake sawa!
 
cha kuongezea tu kwani alitoa pesa yake mfukoni? Si alitumia kodi za wananchi,angekuwa katumia pesa zake sawa!

Namshauri ipumzike tu anatafuta kashifa nyingine kubwa zaidi. Rais mzuri ni yule anayechapa kazi na kukubalika kwa wananchi bila kuwashawishi kwa pesa. Huyu Lowasa hasafishiki makonda alikwisha mmaliza.
 
Kwa lipi la maana alilolifanya lowasa hadi apewe nchi? Kuna sababu nyingi za kusema Lowasa hafai kuwa rais wa nchi hii,licha ya kuwa mgonjwa wa macho na mgongo pia ni mmoja wa watu 11 waliotajwa kuwa ni mafisadi.
Amefanya nini la maana hadi tumpe nchi? Unamkumbuka kwa lipi zaidi ya kujiuzulu? Pesa zake sio tiketi kuwepo ulazima wa kuingia ikulu. Kama anatafuta umaarufu,umaarufu sio kwa mazuri tu hata ufisadi na kujiuzulu napo aljulikana ndani na nje ya nchi.
Sababu zipi za kunishawishi kumpigia kura Lowasa awe rais wa awamu ya tano?

Hivi ni lini katangaza kugombea urais! Hajatangaza nia unaaza kutokwa na povu; akitangaza si utajinyea?? Kama huna hoja ya kupost kaa kimya, pita soma za wengine zenye maana usonge mbele!!! Wewe ni daktari wake hadi ujue anaumwa nini?? Hata km ni daktari ushapoteza sifa maana ni mwiko kutoa siri za wagonjwa!!! Wangapi wagonjwa wa macho/moyo na bado ni viongozi wazuri tu!!??? Jiulize ni wangapi wanavaa miwani tanzania na wangapi nmi viongozi?? au wangapi wanatumia dawa za magonjwa sugu?? Je ni ugonjwa upi haumruhusu mtu kugombea?? Je wewe huna ugonjwa wowote?? Jk alizushiwa magonjwa mangapi na sasa anamalizia kipindi chake?? Ufisadi /wizi upi usiotambuliwa na sheria ambao hatujaona anafikishwa mahakamani??? think twice before you .......
 
Hivi ni lini katangaza kugombea urais! Hajatangaza nia unaaza kutokwa na povu; akitangaza si utajinyea?? Kama huna hoja ya kupost kaa kimya, pita soma za wengine zenye maana usonge mbele!!! Wewe ni daktari wake hadi ujue anaumwa nini?? Hata km ni daktari ushapoteza sifa maana ni mwiko kutoa siri za wagonjwa!!! Wangapi wagonjwa wa macho/moyo na bado ni viongozi wazuri tu!!??? Jiulize ni wangapi wanavaa miwani tanzania na wangapi nmi viongozi?? au wangapi wanatumia dawa za magonjwa sugu?? Je ni ugonjwa upi haumruhusu mtu kugombea?? Je wewe huna ugonjwa wowote?? Jk alizushiwa magonjwa mangapi na sasa anamalizia kipindi chake?? Ufisadi /wizi upi usiotambuliwa na sheria ambao hatujaona anafikishwa mahakamani??? think twice before you .......

nani atmfunga paka kengele?
 
Back
Top Bottom