Kwa lipi Lowassa apewe nchi?

Kwa lipi Lowassa apewe nchi?

Tuna heshimu mawazo yako hata kama hayana mantiki, Nchi hii inahitaji Rais ambaye anaijua nchi vizuri, awe na maamuzi magumu yenye maslahi na watu wake. We need development not democracy without development. Tumechoka bla bla mingi. unakaribishwa kwenye kuapishwa kwake baada ya uchaguzi. My opinion!
 
Domo fereji..huyo,amepanic, hiv huyu jamaa anataka kutuaminisha upuuz wake, na kiuhalisia katika watiania ya urais hakuna anayemfikia lowassa kwa ujasiri,uwezo na historia chanya ya kulitumikia taifa la tanzania
 
Afadhali huyu yeye katibiwa, sawa EL matibabu sijui kama yapo, angekuwa ameshakwenda
Wewe mimi sizungumzii ugonjwa wa Tezi Dume - Kama unakumbuka historia miaka 9 ilyopita jamaa akiwa anagombea uraisi watu walisema jamaa anaumwa na nini?
 
1. Alituhumiwa na Nyerere kuwa utajiri wake una utata, haiji kichwani eti Nyerere hakuwa informed sawa sawa
Nyerere alizaliwa masikini na alikufa masikini - Kwa taarifa yako hatutaki Raisi ajaye awe masikini!
 
wapinga lowasa nyimbo zenu zimechuja tafuteni nyingine

kila kukicha mambo Yale Yale Mara Nyerere alimktaa mara fisadi etc hakuna kipya


RAis anachaguliwa na watu kma ww humpend losawa
ni bora kutumia muda huu kumnadi mgombea wako sio kuchafua Lowasa

hizi kendembwe dhidi ya Lowasa zinadhirihisha kua jamaa yuko step ahead sasa badala ya kukimbia mmkute mnajaribu mpunguza kasi
 
Nyerere alizaliwa masikini na alikufa masikini - Kwa taarifa yako hatutaki Raisi ajaye awe masikini!

Kama watu ni maskini rais wa watu atatoka wapi kama sio maskini mwenzao? Tajiri aende kugombea Marekani kama ataweza kwa matajiri wenzake
 
Kwa lipi la maana alilolifanya Lowassa hadi apewe nchi?

Kuna sababu nyingi za kusema Lowassa hafai kuwa rais wa nchi hii licha ya kuwa mgonjwa wa macho na mgongo pia ni mmoja wa watu 11 waliotajwa kuwa ni mafisadi.

Amefanya nini la maana hadi tumpe nchi? Unamkumbuka kwa lipi zaidi ya kujiuzulu?

Pesa zake sio tiketi kuwepo ulazima wa kuingia ikulu. Kama anatafuta umaarufu,umaarufu sio kwa mazuri tu hata ufisadi na kujiuzulu napo aljulikana ndani na nje ya nchi.

Sababu zipi za kunishawishi kumpigia kura Lowassa awe Rais wa awamu ya tano?

Habari za Lowasa fisadi sasa zinakera, hebu jengeni hoja alifisadi nini? kumbuka hata wewe jirani yako anaweza kusema wewe ni fisadi au hata mchawi wenye akili watahitaji ushahidi ili kujua ukweli.

Kujiuzuru!!! mbona hata Rais wa awamu ya pili Mzee wetu Ally Hassan Mwinyi alijiuzuru na baadaye akawa rais!

Kwa nchi ambazo viongozi wanachaguliwa kwa majority ikiwemo hapaTZ, mtabakia hapa JM mkiponda na akifikia point ya kupigiwa kura atachaguliwa awe mgombea ndani ya CCM yao na hata baadae na Wananchi na kuwa rais.
 
Big up kamanda,umeeleza vyema.
Mambo ni mengi lakini hebu tuangalie haya kwa uchache wake:

1. Alituhumiwa na Nyerere kuwa utajiri wake una utata, haiji kichwani eti Nyerere hakuwa informed sawa sawa

2. Ndiye alikuwa Shwaiba wa JK, JK alichotufanyia watz, hata watoto wanajua HAIKUBALIKI

3. Alipatwa kashfa ya ufisadi na wizi wa mali za umma kwa mikataba mibovu, ukiiba uko waziri mkuu utaacha ukiwa RAIS?

4. Afya yake as we write sio nzuri

5. Ni Mbunge ambaye kwa kipindi cha miaka 8 hajawahi kuchangia bungeni hoja yoyote, maana yake ni nikilaza sana, maana huwezi sema hakuna matatizo kwa namna yoyote ile Tanzania ambayo yanamgusa au hata jimboni kwake tu. Bubu ataongoza nchi??

6. Wakati anajihuzuru alisema anafanya hivyo kwa maslahi ya CCM na Serikali, hakika ndo maana amekaaa kimya kusema ukweli wote maana hakufanya kwa maslahi ya wananchi, leo wananchi wampigie kura tapeli wa kisiasa huyu??? wananchi wa wapi TZ hii ambayo maisha magumu kila siku? HAIWEZEKANI

Ushauri ili kutimiza ndoto yake, aanzishe benki/chuo ili awe rais wa benki/chuo

Naomba kuwasilisha
 
Maamuzi magumu,yapi? Yatajeni sio kubwabwaja tu.
Tuna heshimu mawazo yako hata kama hayana mantiki, Nchi hii inahitaji Rais ambaye anaijua nchi vizuri, awe na maamuzi magumu yenye maslahi na watu wake. We need development not democracy without development. Tumechoka bla bla mingi. unakaribishwa kwenye kuapishwa kwake baada ya uchaguzi. My opinion!
 
Ufisadi sio fashion,kama ni fashion anza wewe kujiita fisadi.
Habari za Lowasa fisadi sasa zinakera, hebu jengeni hoja alifisadi nini? kumbuka hata wewe jirani yako anaweza kusema wewe ni fisadi au hata mchawi wenye akili watahitaji ushahidi ili kujua ukweli.

Kujiuzuru!!! mbona hata Rais wa awamu ya pili Mzee wetu Ally Hassan Mwinyi alijiuzuru na baadaye akawa rais!

Kwa nchi ambazo viongozi wanachaguliwa kwa majority ikiwemo hapaTZ, mtabakia hapa JM mkiponda na akifikia point ya kupigiwa kura atachaguliwa awe mgombea ndani ya CCM yao na hata baadae na Wananchi na kuwa rais.
 
Ufisadi sio fashion,kama ni fashion anza wewe kujiita fisadi.

Kwa hiyo mnaosemasema Lowasa ni fisadi it means mnasema kama Fasion tu.

Ukweli ni kwamba sio fisadi ndio maana ni mbunge,ni mwenyekiti wa kamati nyeti ya bunge. Cha msingi zaidi hajawahi sio tu kuhukumiwa mahakama lakini pia hana kesi yoyote polisi wala mahakamani au baraza la maadili.
 
Nani wa kumfunga paka kengele?
Kwa hiyo mnaosemasema Lowasa ni fisadi it means mnasema kama Fasion tu.

Ukweli ni kwamba sio fisadi ndio maana ni mbunge,ni mwenyekiti wa kamati nyeti ya bunge. Cha msingi zaidi hajawahi sio tu kuhukumiwa mahakama lakini pia hana kesi yoyote polisi wala mahakamani au baraza la maadili.
 
Hakuna chadema isyompenda lowasa na wafuasi wa vyama vyote wanampenda lowasa!

Mimi mwanzo nilikuwa mfuasi wa chama cha democrasia na maendeleo lakni nimekihama rasmi kwa kumfuata Edward lowassa ccm¨

Nampenda mheshimiwa huyu maana anakuja na suluhisho la bomu la vijana tusio na ajira na tunamkubali maana hajawai
kuahidi uwongo hata kule
jimboni kwake.

Ushauri kwa vijana wataifa hili
tumchagua Edward Lowassa maana
ana suluhisho la ajira zetu

Pia nawashauri watanzania kwa
ujumla kuwa suluhisho la matatizo yetu na mwenye maamuzi sahihi bila yakumtegemea mtu au kumwogopa Ni Edward Lowassa tu the president to be.
 
Hakuna chadema isyompenda lowasa na wafuasi wa vyama vyote wanampenda lowasa!

Mimi mwanzo nilikuwa mfuasi wa chama cha democrasia na maendeleo lakni nimekihama rasmi kwa kumfuata Edward lowassa ccm¨

Nampenda mheshimiwa huyu maana anakuja na suluhisho la bomu la vijana tusio na ajira na tunamkubali maana hajawai
kuahidi uwongo hata kule
jimboni kwake.

Ushauri kwa vijana wataifa hili
tumchagua Edward Lowassa maana
ana suluhisho la ajira zetu

Pia nawashauri watanzania kwa
ujumla kuwa suluhisho la matatizo yetu na mwenye maamuzi sahihi bila yakumtegemea mtu au kumwogopa Ni Edward Lowassa tu the president to be.

Unajua kwa nini huu uzi wako umeletwa huku? Kwa sababu heading ilikuwa haiendani na kilichopo ndani
 
Back
Top Bottom