Andy Burnham aapishwa, tayari kumrithi Keir Starmer

Andy Burnham aapishwa, tayari kumrithi Keir Starmer

Elias Msuya

Platinum Member
Joined
Dec 23, 2011
Posts
235
Reaction score
941


Siku moja baada ya Keir Starmer kutangaza kujiuzulu, mwanasiasa mkongwe wa Chama cha Labour, Andy Burnham, ameapishwa tena kuwa Mbunge wa jimbo la Makerfield, hatua inayotajwa kuwa mwanzo wa safari yake kuelekea kuingia Ikulu ya Downing Street kama Waziri Mkuu mpya wa Uingereza.

Burnham, ambaye kwa miaka mingi amekuwa Meya wa Greater Manchester, anaonekana kuwa mgombea mwenye nguvu zaidi wa kurithi uongozi wa chama hicho baada ya kupata uungwaji mkono kutoka kwa viongozi wakuu wa Labour, akiwemo aliyekuwa Waziri wa Afya, Wes Streeting, ambaye ameamua kutogombea nafasi hiyo.

Kwa mujibu wa ratiba iliyowekwa na chama hicho, mchakato wa kuchagua kiongozi mpya unatarajiwa kuanza Julai, huku Burnham akitajwa kuwa mgombea anayepigiwa upatu kushinda bila kupata upinzani mkubwa. Endapo hali hiyo itatokea, anaweza kuingia rasmi Downing Street katikati ya Julai na kuwa Waziri Mkuu wa saba wa Uingereza ndani ya kipindi cha takribani miaka kumi.

Wachambuzi wa siasa za Uingereza wanaamini Burnham atarithi nchi inayokabiliwa na changamoto kadhaa ikiwemo gharama kubwa za maisha, ukuaji hafifu wa uchumi, migogoro ya huduma za umma na shinikizo la kisiasa kutoka kwa vyama vya upinzani.

Katika kauli zake za awali, Burnham ameahidi kuleta utulivu ndani ya Labour na kuelekeza nguvu katika kukuza uchumi, kuboresha huduma za umma na kuimarisha mamlaka ya serikali za mitaa. Pia amesisitiza kuwa kwa sasa si wakati wa kuzungumzia uchaguzi mkuu mpya bali ni wakati wa kuhakikisha serikali inaendelea kufanya kazi kwa ufanisi.

Burnham, mwenye umri wa miaka 56, si mgeni katika siasa za kitaifa. Aliwahi kuwa Waziri wa Afya, Waziri wa Utamaduni na kushika nyadhifa mbalimbali serikalini kabla ya kuwa Meya wa Greater Manchester mwaka 2017. Umaarufu wake uliongezeka wakati wa janga la COVID-19 alipokuwa akitetea maslahi ya wananchi wa kaskazini mwa Uingereza dhidi ya maamuzi ya serikali kuu.

Iwapo atachaguliwa kuongoza Labour na kuapishwa kuwa Waziri Mkuu, Burnham atakabiliwa na jukumu kubwa la kurejesha imani ya wananchi kwa serikali ya Labour huku akijaribu kuzuia kuongezeka kwa nguvu za vyama vya upinzani kabla ya uchaguzi mkuu ujao.

Hata hivyo, kwa sasa macho ya wengi nchini Uingereza yanaelekezwa kwake huku akionekana kuwa mrithi anayetarajiwa zaidi wa Keir Starmer katika kipindi hiki cha mpito wa kisiasa.
 
hawa nao wapuuzi wakubwa. Wanaondoana kama vile mchezo a kuigiza! Wapuuzi wakubwa
 
View attachment 3613707

Siku moja baada ya Keir Starmer kutangaza kujiuzulu, mwanasiasa mkongwe wa Chama cha Labour, Andy Burnham, ameapishwa tena kuwa Mbunge wa jimbo la Makerfield, hatua inayotajwa kuwa mwanzo wa safari yake kuelekea kuingia Ikulu ya Downing Street kama Waziri Mkuu mpya wa Uingereza.

Burnham, ambaye kwa miaka mingi amekuwa Meya wa Greater Manchester, anaonekana kuwa mgombea mwenye nguvu zaidi wa kurithi uongozi wa chama hicho baada ya kupata uungwaji mkono kutoka kwa viongozi wakuu wa Labour, akiwemo aliyekuwa Waziri wa Afya, Wes Streeting, ambaye ameamua kutogombea nafasi hiyo.

Kwa mujibu wa ratiba iliyowekwa na chama hicho, mchakato wa kuchagua kiongozi mpya unatarajiwa kuanza Julai, huku Burnham akitajwa kuwa mgombea anayepigiwa upatu kushinda bila kupata upinzani mkubwa. Endapo hali hiyo itatokea, anaweza kuingia rasmi Downing Street katikati ya Julai na kuwa Waziri Mkuu wa saba wa Uingereza ndani ya kipindi cha takribani miaka kumi.

Wachambuzi wa siasa za Uingereza wanaamini Burnham atarithi nchi inayokabiliwa na changamoto kadhaa ikiwemo gharama kubwa za maisha, ukuaji hafifu wa uchumi, migogoro ya huduma za umma na shinikizo la kisiasa kutoka kwa vyama vya upinzani.

Katika kauli zake za awali, Burnham ameahidi kuleta utulivu ndani ya Labour na kuelekeza nguvu katika kukuza uchumi, kuboresha huduma za umma na kuimarisha mamlaka ya serikali za mitaa. Pia amesisitiza kuwa kwa sasa si wakati wa kuzungumzia uchaguzi mkuu mpya bali ni wakati wa kuhakikisha serikali inaendelea kufanya kazi kwa ufanisi.

Burnham, mwenye umri wa miaka 56, si mgeni katika siasa za kitaifa. Aliwahi kuwa Waziri wa Afya, Waziri wa Utamaduni na kushika nyadhifa mbalimbali serikalini kabla ya kuwa Meya wa Greater Manchester mwaka 2017. Umaarufu wake uliongezeka wakati wa janga la COVID-19 alipokuwa akitetea maslahi ya wananchi wa kaskazini mwa Uingereza dhidi ya maamuzi ya serikali kuu.

Iwapo atachaguliwa kuongoza Labour na kuapishwa kuwa Waziri Mkuu, Burnham atakabiliwa na jukumu kubwa la kurejesha imani ya wananchi kwa serikali ya Labour huku akijaribu kuzuia kuongezeka kwa nguvu za vyama vya upinzani kabla ya uchaguzi mkuu ujao.

Hata hivyo, kwa sasa macho ya wengi nchini Uingereza yanaelekezwa kwake huku akionekana kuwa mrithi anayetarajiwa zaidi wa Keir Starmer katika kipindi hiki cha mpito wa kisiasa.
kujiuzulu ni udhaifu na tabia mbaya sana ya kukimbia tatizo.

inaonekana hawa jamaa hawapendagi changamoto kabisa, wakikumbana nazo wanatoka nduki kiulaini 🐒
 
Mmezoea kung’ang’ania madaraka, hata kwa gharama ya kumwaga damu za watu wasiokuwa na hatia!
uzoefu wa kukimbia matatizo ni uzembe wa kiwango kibaya sana gentleman,
hayo mengine ni porojo za kutafuta public sympathy tu, ni kitu useless.

UK waache tabia mbaya ya kukimbia matatizo yao wenyewe, bali wasimame imara na kuyayatatua na sio kuyakimbia na kurithishana kama kipaji vile 🐒
 
kujiuzulu ni udhaifu na tabia mbaya sana ya kukimbia tatizo.

inaonekana hawa jamaa hawapendagi changamoto kabisa, wakikumbana nazo wanatoka nduki kiulaini 🐒
Una akili kama za huyo tumbili ulimweka hapo kwenye ishu ya demokrasia
 
Una akili kama za huyo tumbili ulimweka hapo kwenye ishu ya demokrasia
na watu wa aina yao hata kwenye ndoa na familia zao wako hivyo hivyo.

akipata changamoto tu kidogo wanaachana. Hiyo ni nonsense.

watu wanapewa nafasi za uongozi ili kwenda kutatua changamoto na sio kukimbia changamoto gentleman

huna haja ya kua na mihemko nonsense kwenye ukweli huu gentleman 🐒
 
na watu wa aina yao hata kwenye ndoa na familia zao wako hivyo hivyo.

akipata changamoto tu kidogo wanaachana. Hiyo ni nonsense.

watu wanapewa nafasi za uongozi ili kwenda kutatua changamoto na sio kukimbia changamoto gentleman

huna haja ya kua na mihemko nonsense kwenye ukweli huu gentleman 🐒
Tofautisha familia na serekali wewe
Jinga
Ndo maana mnapewa uongozi mnataka kuendesha wananchi kama familia zenu pumbavu
 
Tofautisha familia na serekali wewe
Jinga
Ndo maana mnapewa uongozi mnataka kuendesha wananchi kama familia zenu pumbavu
kwahiyo mihemko na mambo yako binafsi au ya familia yako ndio unakuja nayo kuharibu miundombinu ya umma, right?🐒
 
Demokrasia upuuzi. Hivi toka Brexit wamepita mawaziri wakuu wangapi?
 
Sijajua bado kwanini yule wazir mwanamama kajiuzuru,lakini utaratibu wao kujiuzuru ni mzuri sana,inaonyesha wanawajibika kwa makosa au kushindwa kwao kutimiza majukumu fulani lengo fulani.

Kujiuzuru ni heshima kubwa sana,hata Marehemu Raisi Mwinyi naye alijiuzur alipokuwa waziri wa mambo ya ndani,kwa maana aliwajibika kwa makosa ya wizara yake,baadae akaja kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Binafsi naupenda sana utaratibu wa waingereza
 
hawa nao wapuuzi wakubwa. Wanaondoana kama vile mchezo a kuigiza! Wapuuzi wakubwa
Imefika wakati hata huyu aliondoka jana nilikuwa simfahamu, wakati fulani Italy walikuwa kama hawa Waingereza lakini sasa naona wametulia kijiti wamechukua Uingereza.
 
Back
Top Bottom