Kwa lipi Lowassa apewe nchi?

Kwa lipi Lowassa apewe nchi?

Mara nyingi umekuwa ni mtu anayetajwa kuhusika na ubadhirifu pia ufisadi mbalimbali unaofanyika ndani ya nchi, ukiwamo richmond ambapo mara zote umekuwa akiwaadaa wananchi kwamba alijiuzulu ili kulinda heshima ya serikali na chama chake jambo ambalo sio kweli, taarifa ya tume ambayo iliundwa na bunge kufuatilia sakata hilo iliweka wazi namna waziri mkuu alivyohusika moja kwa moja katika ubadhirifu huo vikiwamo viambatanisho vya vinote vyake, mawasiliano, na namna jinsi zoezi zima la ugavi ulivyoendeshwa. Lakini pia amehusika na ufisadi katika ujenzi wa jengo la ukumbi wa mikutano ya kimataifa AICC.

Lakini pia watanzania tunakufahamu kama mwenye kutumia vibaya madaraka yake, akiwa waziri mkuu alikuwa ni mtu mkorofi na mwenye maamuzi ya kukurupuka, alikuwa ni mtu mwenye kuwafukuza watu kazi kwa uonevu papo kwa papo bila hata kuwapa haki ya kuwasikiliza (right to be heared au natural justice)hasa wanapokataa kulinda maslahi yako , uliwah kumdhalilisha na kutaka kumfukuza kazi dc aliyekuwa ameteuliwa siku tatu tu na sasa ni mkuu wa mkoa, ndg mongela.

Ametumia madaraka yake vibaya kwa kujilimbikizia mali mbalimbali ikiwamo umiliki wa ardhi mkubwa hasa jijini dar es salaam kwa mfano eneo la peninsula pale masaki ambapo amejipatia viwanja kadhaa na ushahidi amejenga nyumba ya ubalozi wa south africa, AKiwa waziri mkuu alishiriki kuamuru uvunjaji wa ghorofa masaki kwa sababu linaziba nyumba yake kukosa upepo kutoka baharini, huku akidanganya umma kuwa ghorofa lile limejengwa kinyume na utaratibu, amekuwa mtu mbadhirifu wa mali za umma sana kwa kutumia madaraka yake kwa mfano amejimilikisha majengo ya ppf na kumpa mtoto wake.

Ni mtu msanii sana na si mkweli hasa kwa utaratibu wake wa kukwakupua mipango ya serikali na kusema amefanya yeye, akiwaaminisha watu kwamba amekuwa anaisimamia ama kuanzisha yeye jambo ambalo limekuwa likifanywa na serikali kama timu, mara nyingi anazungumzia shule za kata ambazo zimeanza tokea enzi za mkapa wakati wa waziri ndg joseph mungai, pia amekwapua mradi wa maji ziwa victoria akisema ameanzisha yeye jambo ambalo sio kweli kabisa, mradi ule ulisainiwa na ndg benjamini mkapa mwaka 2002 wakati huo waziri wa maji akiwa ndg pius ng'wandu.

lowassa akijinasibu kwa hoja yake ambayo sio nzuri kwake lakini yeye amekuwa akiwadanganya wananchi kwamba ana maamuzi magumu, maamuzi yake hayakuwa magumu bali ni ya kukurupuka na yasiyokuwa makini yaliyolenga kujikampenia uraisi ambayo yamelitia taifa hasara sana, kwa mfano kuvunja mikataba kinyume cha sheria ambayo baadae ameitia hasara serikali kwa kulipa fidia mfano mradi wa maji wa jiji (city water) amevunja majengo masaki ambayo hayo yote serikali ilibidi kutoa kodi za wananchi ili kulipa fidia amelitia hasara taifa, hayo ni kwa ufupi tu lakini yapo mengi sana.
 
Pwani kwetu nakushukuru kwa mchango wako wa kusaidia watanzania wengi kuwafahamu vizuri hawa wanaotaka kutuongoza Si wengi tuna access ya taarifa nyingi nyeti.Isiwe kwa Edward tu iwe kwa wote ili mradi yasiwe majungu.Mungu ibariki Tanzania
 
Lowassa ni fisadi nambari wahedi,yeye na mwenzie mjenzi huru a.k.a nyoka wa makengeza wameleta nuksi sana hapa Tz.
 
Kwa lipi la maana alilolifanya Lowassa hadi apewe nchi?

Kuna sababu nyingi za kusema Lowassa hafai kuwa rais wa nchi hii licha ya kuwa mgonjwa wa macho na mgongo pia ni mmoja wa watu 11 waliotajwa kuwa ni mafisadi.

Amefanya nini la maana hadi tumpe nchi? Unamkumbuka kwa lipi zaidi ya kujiuzulu?

Pesa zake sio tiketi kuwepo ulazima wa kuingia ikulu. Kama anatafuta umaarufu,umaarufu sio kwa mazuri tu hata ufisadi na kujiuzulu napo aljulikana ndani na nje ya nchi.
Anaitwa mtu wa maamuzi magumu,maamuzi yapi? Kujiuzulu ni uwajibikaji sio maamuzi magumu. Maamuzi magumu yapi? Alikuwa anafukuza watumishi wa serikali majukwaani bila hata kuwapa nafasi ya kijitetea(natural justice). Kama sio kuwaonea ni nini? Yeye alikuwa analalamika ooh mh spika,nimeonewa sana,nimesikitika sana hata sijaulizwa juu ya Richmond sijapewa hata nafasi ya kujitetea(natural justice),amesahau kuwa usihukumu usije ukahukumiwa(mathayo 7:1)
wanasema alijenga shule za kata,je,alitumia pesa yake badala ya kodi za watz? Walitaka afanye nn wakati ulikuwa wajibu wake kama mtendaji mkuu wa shughuli za serikali za kila kitu?

Sababu zipi za kunishawishi kumpigia kura Lowassa awe Rais wa awamu ya tano?




Hakuna mtu anayepewa nchi hii.
Mtu anapewa kiwanja au shamba.
Hii nchi ni milki ya watanzania mil.45.
Sasa hiyo stori ya kumpa Lowasa nchi inatoka wapi?

Nijuavyo mimi Lowasa haombi kupewa nchi anaomba uongozi wa nafasi ya urais.
Na anajua kuwa wenye ridhaa ya kumpa hiyo nafasi ni watanzania na sio kikundi cha watu kumi.
 
huo ndo ukweli ingawa wapambe hawataki kusikia.
Tusimhukumu mtu kwa kudhaania.tumuhukumu kwa matendo yake.lowassa ana nia ya kweli ya kuleta maendeleo kwa tanzania.tumeona muda mrefu amekuwa akichangia miradi mikubwa ya nchi akiwa MB tu.kwa nini tusimpe ridhaa ya kuongoza taifa hili.apewe.hakuna wa kuzuiya tena mkondo huu wa maji kule unakotaka kuelekea.big up lowassa
 
Hakuna sababu ambayo nimeona tangu niingie humu ndani jf kuona kommet kuhusu mh El

Nimeshangaa sana kuona watu humu wanakuja na sababu za ufisad Mara mgonjwa bado sijaona kama zina mashiko.

Naomba kama mtu anaushahid wa kina kwa wale mnao mchafua atoke hazaran na mbele ya waandish wa habar azungumze maana naona kujiongezea dhambi kama nitaongea kwenye mitandao

Kwa wale mnaomtakia nia lowasa ya kuingia ikulu na tunaona kabisa ndiye mwenye uwezo wa kutufikisha aseme neno
Ndio
au
hapana
tujue humu humu ndan
 
lowasa hana kipaji cha uongozi ila anakipaji cha uongo.
Uwezo wake ni kuongoza ng'ombe sio watu.
Lowasa ni jipu, ukitumbua vibaya utachafuka wewe, linahitaji timing sana
 
Kwa lipi la maana alilolifanya Lowassa hadi apewe nchi?

Kuna sababu nyingi za kusema Lowassa hafai kuwa rais wa nchi hii licha ya kuwa mgonjwa wa macho na mgongo pia ni mmoja wa watu 11 waliotajwa kuwa ni mafisadi.

Amefanya nini la maana hadi tumpe nchi? Unamkumbuka kwa lipi zaidi ya kujiuzulu?

Pesa zake sio tiketi kuwepo ulazima wa kuingia ikulu. Kama anatafuta umaarufu,umaarufu sio kwa mazuri tu hata ufisadi na kujiuzulu napo aljulikana ndani na nje ya nchi.

Anaitwa mtu wa maamuzi magumu,maamuzi yapi? Kujiuzulu ni uwajibikaji sio maamuzi magumu. Maamuzi magumu yapi? Alikuwa anafukuza watumishi wa serikali majukwaani bila hata kuwapa nafasi ya kijitetea(natural justice).

Kama sio kuwaonea ni nini? Yeye alikuwa analalamika ooh mh spika,nimeonewa sana,nimesikitika sana hata sijaulizwa juu ya Richmond sijapewa hata nafasi ya kujitetea(natural justice),amesahau kuwa usihukumu usije ukahukumiwa(mathayo 7:1)

wanasema alijenga shule za kata,je,alitumia pesa yake badala ya kodi za watz? Walitaka afanye nn wakati ulikuwa wajibu wake kama mtendaji mkuu wa shughuli za serikali za kila kitu?

Sababu zipi za kunishawishi kumpigia kura Lowassa awe Rais wa awamu ya tano?

Kwa ufisadi
 
Lowasa ni ovyo kabisa mkuu.
Maamuzi ya kuanzisha shule za kata zisizokuwa na uwezo wa kutoa elimu?

Maamuzi endelevu ya kwenda kutafuta mvua ya kutengeneza?

Maamuzi ya kwenda Niuzilendi ku eti kujifunza kilimo cha vitunguu?

Maamuzi ya kushiriki mikataba ya richmond ya kitapeli huku akijua eti kwa sababu hata kikwete alifahamu?

Analipi la kutuambia huyu Watanzania huyu mtu?

Hatutaki. Unafiki mtupu
 
Nahakika sala zangu zitatimia na sala za wanyonge wote Tanzania hakika #mamviii atakatwaaaaaaaaaaaa tuuuuu,na tuseme amina walala hoi wenzangu
 
Yani hata mfanyeje mi napenda kuwaambia kuwa bila sisi kuomba sana kwa mwenyezi Mungu basi Tanzania itakuwa chini ya freemason na hii ni kweli we ona watu wanavyomkubali lowassa yani tumeshaingiwa na pepo mbaya sasa
 
Back
Top Bottom