Kwa lipi la maana alilolifanya Lowassa hadi apewe nchi?
Kuna sababu nyingi za kusema Lowassa hafai kuwa rais wa nchi hii licha ya kuwa mgonjwa wa macho na mgongo pia ni mmoja wa watu 11 waliotajwa kuwa ni mafisadi.
Amefanya nini la maana hadi tumpe nchi? Unamkumbuka kwa lipi zaidi ya kujiuzulu?
Pesa zake sio tiketi kuwepo ulazima wa kuingia ikulu. Kama anatafuta umaarufu,umaarufu sio kwa mazuri tu hata ufisadi na kujiuzulu napo aljulikana ndani na nje ya nchi.
Sababu zipi za kunishawishi kumpigia kura Lowassa awe Rais wa awamu ya tano?
He is the hope YOU deserve and NOT THE HOPE WE DESERVE!!
unaposema "we" unamaanisha wewe na nani?
afadhali apewe, maana kwa miaka 9 sasa nchi ipo auto pilot! hakuna wa kuamua jambo! kila mtu analalamika! bora aje atuibie lakini awe na maamuzi endelevu!
Hujui unachokisema wewe.
nimejikuta nacheka tu ! Eti Bora mwizi anayezuia wengine kuiba , inakatisha tamaa sana .
Hivi hatuwezi kupata mwenye maamuzi endelevu asiyekuwa mwizi?
Kila mwenye uraia wa tanzania
Hahahahahaha! Misukule ya mzee mamvi inatia huruma!
siwezi kutaja jina la mtu bali nataja sifa za mtu anayefaa kuwa rais wa nchi hii.
1. Awe mwadilifu na mzalendo
2. Awe na uwezo wa kutatua matatizo ya kiuchumi,kisiasa na kiutamaduni
3. Awe ni mtu anayejali watu wake hususani wanyonge
4. Awe ni mtu anayeweza kulinda rasimali zetu kama madini,wanyama nk
4. Awe na uwezo wa kushughulikia wahujumu uchumi
Unaambiwa tangu azaliwe hajawahi kukemea wizi wowote , yaani hata wa njiwa !