Kwa lipi Lowassa apewe nchi?

Kwa lipi Lowassa apewe nchi?

LOWASSA mwizi sana, SLAA hana recodi yoyote ya kujivunia mpaka aitwe mkombozi wa taifa, tuache kupamabana kijinga mitandaoni

Umeandika point ya maana lakn umetumia lugha ambayo kwa hali ya kawaida inakera
 
Hivi kumbe yupo kwenye chati!!? sijaiona hiyo chati!
 
Lowasa ni ufisadi wake na akili ndogo za watz
Nakubaliana na wewe Mkuu. Ufisadi wa Liwasa unawafanya aadhi ya watu ambao hapo awali walikuwa na akili leo wanaonekana ni misukule yake
 
Hivi kumbe yupo kwenye chati!!? sijaiona hiyo chati!

lowassa kila siku unamsikia kwenye media, na unafanyiwa na utafiti ya kuwa yeye ndio raisi wa awamu ya tano, hafu wewe unasema hayumo kwenye chati
 
Sijawahi wala kusikia Lowasa akikemea ufisadi na maadili ya uongozi katika taifa hili. Akiwa rais atapata wapi ujasiri wa kuwanyoshea vidole wengine? Hii ndio inayomkumba mzee wa tezi dume kuwa ameshindwa kuwanyoshea vidole wenzie kwa sababu anajua nafasi yake katika ufisadi
 
LOWASSA ni mtu mwenye maamuzi na anayethubutu,si wa kulialia kama wanavyolia na kulalamika viongozi wa sasa,haijulikani mwananchi ni nani na mwenye maamuzi ni nani
Maamuzi yapi?
 
Maamuzi ya kuanzisha shule za kata zisizokuwa na uwezo wa kutoa elimu?

Maamuzi endelevu ya kwenda kutafuta mvua ya kutengeneza?

Maamuzi ya kwenda Niuzilendi ku eti kujifunza kilimo cha vitunguu?

Maamuzi ya kushiriki mikataba ya richmond ya kitapeli huku akijua eti kwa sababu hata kikwete alifahamu?

Analipi la kutuambia huyu Watanzania huyu mtu?

Hatutaki. Unafiki mtupu


CCM, Lowasa kawaweka kwenye kona ........................... bado tu hajaanza kuwashambulia!!
 
Edward Lowasa toka aanze kufanya shughuli za kijamii baada ya kujiuzuru uwaziri mkuu. Baadhi yetu tumekuwa na woga naye sijui kwa sababu gani waliyo iyona kwake ya kuwatisha. Kila umuulizaye atakwambia ni fisadi ukitaka athibitishe madai hayo hilo linakuwa kwake ni swali la dola milion moja. Nimejifunza kwa watu wenye hekima na busara nyingi tena wenye upeo wa hali ya juu. Ya kuwa ukimuona mtu wanamjadili ujue anakubalka. E. Lowasa sasa ni jibu la watanzania ktk uchaguzi wa 2015. Na nyie mnamuogopa E Lowasa kwanini hasa.?
 
...kwa Tanzania ukiwa wewe ni kiongozi, ukaona waliochini yako au unaowaongoza wanakupenda elewa kuwa wewe ni kiongozi DHAIFU, au kwa lugha tulioizoea "hana tofauti na nyoka wa Kibisa ambaye hana madhara pindi anapokuwa nacheza na binadamu". Kupendwa na watu haiwezi kuwa sifa nzuri ya uongozi' yaani unakuwa wewe ni kiongozi MSHIKAJI, asiyekuwa na madhara kwa wale unaowaongoza!
"Lowassa alikuwa kiongozi MCHAPA KAZI, NA ANEYE MWAJIBISHA MOJA KWA MOJA MTENDAJI ALIYE CHINI YAKE".

Kwahiyo ndiyo maana watendaji wengi ndani ya ccccm wanamwogopa, kwa sababu ya MUAAMUZI yake ya hapo kwa papo!.
 
EL Ni Fisadi Na Wewe Mtoa Mada Ni Mfaidika Wa Ufisadi Wake.
 
....karibia ccccm weto wamechafuka!
Na nukuu maswali ya Lowassa aliyomuuliza Kikwete:
“Yule bwana (Lowassa) alimuuliza Kikwete, hivi,
mnataka kunipa barua kwa kosa lipi?
Nimefanya nini? Nini ambacho wewe
hukifahamu,”


"ina maana katika ufisadi wa Lowassa aliokuwa anafanya' kwanza alikuwa ni lazima upate baraka za Kikwete"
 
Lowasa ndiye raisi wa nchi hii 2015 na kwenye hili sakata la Escrow ndio Mungu anamuinua sasa.
 
el ni mtu wa maamuzi sio mchezo. kumbuka jinsi wazungu waliobinafsishiwa maji dar alivyowatimua baada ya wao kujidai ujanja. kampuni ilirejeshwa kwa umma wazungu wakatimuliwa kwa escort airport. kesi ya fidia waliofungua ulaya wakashindwa. linganisha na epa richmond na iptl. watu wanapasiana nchi itachunwa hadi vitukuu. mara huyu kamuuzia huyu ooh wenyewe wanagombana wako mahakamani..wizi mtupu.
 
Back
Top Bottom