Kwa hili Wamarekani wanatudharau

Kwa hili Wamarekani wanatudharau

Wakati Kikwete alikuwa akienda Marekani na kuishia kupiga picha na Boyz 2 Men na UB40 ni Magufuli alikuwa ameharibu siasa?


Ni hivi ukiwa kibaraka na cheap kwa wazungu na wao wanakutreat hivyo hivyo.

Ulishaona Rais wa Nchi yeyote kampigia simu samia kumkaribisha atembelee nchi yake?

Lakini Chancellor wa Ujerumani alimpigia Rais Magufuli simu na kumkaribusha Germany na mwamba hakwenda.

Huyu wa kujitembeza bure hana value. Kwanza wanakudharau tu.
Ni hivyo sio? Rais wa nchi uingie kwenye nchi nyingine mwenyeji wako asikutambue?
Bado Kuna uchafu wa siasa za Magufuli alizozifanya haujaondolewa kwenye taswira ya nchi kimataifa
Nchi bado inanuka
Huwa dhambi inaondolewa kwa Toba haitoki yenyewe
Asanteni.
 
Ni hivyo sio? Rais wa nchi uingie kwenye nchi nyingine mwenyeji wako asikutambue?
Bado Kuna uchafu wa siasa za Magufuli alizozifanya haujaondolewa kwenye taswira ya nchi kimataifa
Nchi bado inanuka
Huwa dhambi inaondolewa kwa Toba haitoki yenyewe
Asanteni.
Hapana, ni ka vile hatuwezi kupima mtu ambaye hayopo kujitetetea, ila ukweli ni kwamba iwapo Magufuli angekwenda Marekani angepokelewa kwa heshima kubwa hasa kwa vile ujio wake ungevuta vyombo vya habari vingi sana. Mama yuko Marekani, hakuna vyombo vya habari vinavyotilia uzito ziara yake.
 
Hapana, ni ka vile hatuwezi kupima mtu ambaye hayopo kujitetetea, ila ukweli ni kwamba iwapo Magufuli angekwenda Marekani angepokelewa kwa heshima kubwa hasa kwa vile ujio wake ungevuta vyombo vya habari vingi sana. Mama yuko Marekani, hakuna vyombo vya habari vinavyotilia uzito ziara yake.

..vyombo vingi vya habari vingemfuatilia Jpm kwasababu alikuwa ana sifa mbaya ya udikteta.

..pia vingemfuatilia kwasababu alikuwa ni covid denier, hivyo vyombo vingi vya habari vingependa kukutana naye na kum-challenge.

..Rais Ssh amesema anataka kurudisha heshima ya Tz kidiplomasia kama ilivyokuwa wakati wa Mwalimu Nyerere.
 
..vyombo vingi vya habari vingemfuatilia Jpm kwasababu alikuwa ana sifa mbaya ya udikteta.

..pia vingemfuatilia kwasababu alikuwa ni covid denier, hivyo vyombo vingi vya habari vingependa kukutana naye na kum-challenge.

..Rais Ssh amesema anataka kurudisha heshima ya Tz kidiplomasia kama ilivyokuwa wakati wa Mwalimu Nyerere.
Hata angekwenda kabla ya Covid mambo yangekuwa yale yale. Covid ni kosa pekee na kubwa sana alilofanya kwenye mwaka wa mwisho wa utawala wake, lakini kabla ya hapo alikuwa akisikika sana kwa mamabo mengi mazuri tu.
 
Hata angekwenda kabla ya Covid mambo yangekuwa yale yale. Covid ni kosa pekee na kubwa sana alilofanya kwenye mwaka wa mwisho wa utawala wake, lakini kabla ya hapo alikuwa akisikika sana kwa mamabo mengi mazuri tu.

..alikuwa akisikika kwa udikteta na ukatili.

..Jpm alifanya ukatili ambao Watz hatukutegemea kwamba unaweza kufanyika nchini kwetu.
 
..alikuwa akisikika kwa udikteta na ukatili.

..Jpm alifanya ukatili ambao Watz hatukutegemea kwamba unaweza kufanyika nchini kwetu.
Hakuwa katili, alifanya kazi yake vizuri sana ila watanzania walikuwa wamezowea rais asiyefanya kazi ndiyo maana wakamwona yeye ni katili. Rais ni lazima asimamie sheria mbalimbali za nchi, sasa kwa vile sheria ni msumeno, na waswahili tulikuwa tumezowea kuishi kama vile hakuna sheria, tukaona machungu. Sasa hivi tunaishi tena kama vile hakuna sheria
 
Tanzania haina political stability kama Kenya ndio maana unaona Uhuru Kenyatta alipokelewa na Biden wakati mama alipokewa na diaspora!
Kitu kingine uchumi wa kenya ni mkubwa, kiasi kwamba rais wao anaheshimika na mabeberu...........kenya wanajitegemea kwa bajeti kwa karibu asilimia 97.........
 
Hakuwa katili, alifanya kazi yake vizuri sana ila watanzania walikuwa wameazowea rais asiyefany kazi ndiyo maana wakamwona yeye ni katiri. Rais ni lazima asimamie sheria mbalimbali za nchi, sasa kwa vile sheria ni msumeno, na waswahili tulikuwa tumezowea kuishi kama vile hakuna sheria, tukaona machungu. Sasa hivi tunaishi tena kama vile hakuna sheria

..alikuwa anajali sheria ikiwa inam-favour yeye.

..sheria ikiwa iko upande asioupenda haifuati.

..tatizo hilo alikuwa nalo tangu akiwa Waziri na alipopata Uraisi likawa tatizo kubwa zaidi.

..hivi kwa mfano suala la kukataza mikutano ya hadhara ya vyama vya siasa unaamini Jpm alikuwa anafuata sheria.

..au makesi mabaya-baya yaliyowakabili viongozi na wafuasi wa vyama vya upinzani unaamini serikali ya awamu ya 5 ilikuwa sahihi?

..Kwamba huko nyuma wapinzani walizoea kufanya siasa kinyume na sheria alipoingia Jpm ndio akaanza kusimamia sheria ya vyama vya siasa?
 
Rais hajaenda Marekani kwa ziara ya kiserikali (official state visit), ameenda kwa shughuli tofauti ambayo haihusiani kukutana na Rais

Kuna protokali za Marais kukutana sio tu kwa sababu ameenda kwenye nchi yao

Ameenda kufanya nini? Either ni Ziara rasmi au kula bata.

Kuzindua filamu ni siku moja tu.
 
Rais wetu anakaribia kufunga wiki nchini mwao lakini mwenyeji wake ambaye ndiye mkuu wa nchi hajakutana na mgeni wake(Mh. Rais wetu)

Hii ni dharau...ifike mahali tuwe masikini jeuri, hivi Mh. Biden angefanya ziara nchini Tanzania, kweli Mhe. Rais wetu angekuwa bize na mambo mengine na kuicha hiyo shughuli kwa waandamizi wake?

Ifike mahali wizara ya mambo ya nje wajitafakari pia katika hili.
Tatizo la rais wetu anamsikiliza sana rais wetu kilaza wa miaka ya nyuma (JK)....yule jamaa alishindwa kabisa kuwa rais wetu ila alijipa utalii wa dunia usiyo na malipo angani.
 
Tatizo la rais wetu anamsikiliza sana rais wetu kilaza wa miaka ya nyuma (JK)....yule jamaa alishindwa kabisa kuwa rais wetu ila alijipa utalii wa dunia usiyo na malipo angani.
Huyu SSH anawasikiliza wapuuzi, wabinafsi ndio washauri wake wakuu.

Uzalendo kwake ni sifuri. Kujali issue za Watanganyika, hajali kitu ni kutumbua tu pesa zao.
 
Huyu SSH anawasikiliza wapuuzi, wabinafsi ndio washauri wake wakuu.
Ndiyo maana watu wanamdharau maana anajitakia mwenyewe. Angalia kwenye taasisi za serikali, siku hizi ule ujinga wa enzi za JK umerudi tena, nobody works na Mama mwenyewe anaikimbia nchi yake.
 
Ndiyo maana watu wanamdharau maana anajitakia mwenyewe. Angalia kwenye taasisi za serikali, siku hizi ule ujinga wa enzi za JK umerudi tena, nobody works na Mama mwenyewe anaikimbia nchi yake.
Upuuzi mtupu. Wanasema ni demokrasia kuwajaza wezi serikalini.
 
..vyombo vingi vya habari vingemfuatilia Jpm kwasababu alikuwa ana sifa mbaya ya udikteta.

..pia vingemfuatilia kwasababu alikuwa ni covid denier, hivyo vyombo vingi vya habari vingependa kukutana naye na kum-challenge.

..Rais Ssh amesema anataka kurudisha heshima ya Tz kidiplomasia kama ilivyokuwa wakati wa Mwalimu Nyerere.
Heshima gani unayoizungumzia hapa!
 
Una maana gani na "political stability"?

Unachanganya mambo kwa kutumia lugha usiyofahamu maanha yake.

Ungesema, Kenya ni "Strategic partner" ndio maana kiongozi wa huko hupokelewa White House na mwenyeji wake hapo ungeeleweka.

Lakini hata kama ungesema hivyo, bado ningekuwa na mashaka kama unaelewa maana ya kuwa "strategic partner" ni nini.

Huyu hupewa majukumu maalum katika eneo fulani, na kuna ujira maalum anaopewa kila mwaka siyo chini ya Bilioni moja, ndiyo, bilioni moja ya hard currency kila mwaka, pamoja na marupurupu mengine chungu nzima.

Sasa huwezi ukalinganisha partner huyo na huyu kapuku mwingine anayejisomba na yeye apewe upendeleo.

Na hadi hapa, kama bado huelewi, basi kuna tatizo sehemu fulani. Jaribu kujichunguza uliondoe tatizo hilo.
Acha ushamba wewe mataga unajua maaana ya political stability kwanza!
 
Back
Top Bottom