peno hasegawa
JF-Expert Member
- Feb 24, 2016
- 12,829
- 21,460
Kutoka Kiaraka, Magegeni, Bagamoyo mkoa wa Pwani, kumetokea utata juu kuzikwa kwa mwili wa marehemu Massawe ambapo upande wa mke wanataka mwili usafirishwe na upande wa mume na majirani wakitaka marehemu azikwe nyumbani kwake Kiaraka walipojenga na mke wake.
Kutokana na utata huo mke amewasilisha maombi mahakamani kupinga mwili usitoke hospitali na kuzikwa nyumbani kwakwe bali usafirishwe kama yeye na ndugu zake wanavyotaka.