Sifa za kuoa au kuolewa

Mwl Mwakujonga

JF-Expert Member
Jun 29, 2023
286
582
Utangulizi
Nimekua nikisoma habari mbalimbali katika mitandao ya kijamii, katika Jambo ambalo linanipa maswali ni mabadiliko ya vigezo vya kuoa au kuolewa

Wakati nikiwa kijana mdogo kuna maswali yalinisumbua sana, mana mtaa ambao nilikuwa naishi ulikuwa na nyumba za watumishi WA umma (magorofa ya TBA) na kwa sehemu kubwa walikuwepo wanasheria na watumishi WA idara zingine za serikali

Marafiki zangu Kwa sehemu kubwa Baba Zao walikuwa wanasheria na mama Zao walikuwa walimu na wachache walikuwa mama WA nyumbani.

Wakati nikiwa katika harakati za kuoa maswali mengi yalikuwa kichwani mwangu juu ya wale wazazi wa rafiki zangu na wazazi wengine ambao nilikuwa nawafahamu.

Kwakweli Kwa sehemu kubwa kulikuwa na ufanano na ndoa hizo sina uhakika Sana juu ya migogoro iliyokuwako kwenye hizo ndoa , nachojua zilitulea na kutufikisha hapa tulipo.

Wakati nataka kuoa niliwaza Sana ni kigezo gani kiwe cha Kwanza na muhimu kwa binti ambaye atakuwa mke wangu?

Kigezo cha Kwanza ambacho kilikuwa moyoni mwangu ni

A. Mwenye Hofu ya Mungu 60%

Kuna tofauti ya kwenda kusali na kuwa na Hofu ya Mungu , kipindi cha kuoa au kuolewa kila mmoja anakwenda kanisani Kwa tumaini la kumpata mweza ndio maana lazime UWE makini, sio kila MTU anayekwenda kanisani ana Hofu ya Mungu

Biblia inasema MTU Mwenye Hofu ya Mungu ni Yule anayeskia neno la Mungu na kutetemeka , unashangaa uko kwenye mahusiano na binti tena ni MTU wa ibada Sana lakini haigopi uzinzi ! Ujue huyo MTU Hana Hofu ya Mungu.

Umesoma habari ya Yusufu alipolazimishwa na mke wa potifa kufanya nae mapenzi ,akakataa akiogopa kumtenda Mungu dhambi.

Leo hii vijana wanapotaka kuoana wanataka Kwanza kufanya ngono Kwanza wajuane Kwanza , ndio maana ndoa nyingi za Leo zina pata shida

B. Mama wa Watoto wangu 30%
Nilijiuliza maswali Huyu binti ambaye nakwenda kumwoa ndiye atakaye kuwa mama wa Watoto wangu?

Kuna kitu ambacho watu wengi Hawajui , tumbo la mwanamke limewekwa na Mungu kupitisha agano la Mungu Kwa mwanadamu

Mungu alisema na Ibrahimu akamwambia utapata mtoto wakiume Kwa Sarah Kwa sababu kwenye tumbo la Sarah Ndiko kuna agano ambalo Mungu alifunga na Ibrahimu ndio maana licha ya Ibrahimu kuwa na watoto wengi lakini ni Isack Tu ndiye aliyepewa urithi wakiagano na Mungu

Kwa hiyo unapochagua binti wakuoa ni lazima ujue anafaa kuwa mama wa Watoto wako?

Kuna tofauti ya kuwa na binti kama girlfriend na binti kama mama WA familia

C. Mwenye kujishughulisha

Ni kweli biblia inatoa maagizo kwamba Baba ndiye ataleta chakula Kwa ajili ya familia, lakini biblia hiyo hiyo inasema mke Mwema ni Yule anayejishughulisha Kwa kazi ya mikono

Leo hii mabinti wengi wanafanya kazi nzuri Tu lakini bado wanategemea fedha Zao kuzitumia Kwa matumizi ya mapambo na hanasa za Dunia lakini za mume ndio zitumuke kwenye familia

D. Na vigezo vingine ambavyo 10%

Vigezo vya Karne ya 21

A. Mwenye Shape au Elimu na fedha 60%

Kitu ambacho kinanisikitisha ni habari za ndoa za SASA watu kuachana hata mwezi hawajafikisha? Umetumia gharama zote za sherehe kubwa lakini ndoa hazidumu Kwa sababu umeangalia kitu kidogo Sana , shape inakwisha, Elimu sio maarifa na fedha zinamabawa Leo ziko kesho haziko, vitu vya nje haviwezi kutunza ndoa
 
Vigezo vya kuoa na kuolewa wanavyo waoanaji wenyewe.

Wengine wanataka ujichubue,wengine uwe na kitambi, wengine uwe maskini wengine uwe tajiri wengine uwe mrefu wengine uwe mfupi, wengine uwe na dini wengine hawataki wa kanisani au msikitini, wengine wanakutana baa ila wakioana mmoja anamkataza mwenzie asiende anataka kwenda mwenyewe. Yaani ilimradi vurugutu mkuu

Usichanganywe kama unataka mbilikimo funga nae ndoa. Kama umempata mwenye kibiongo mnapendana usisikilize kelele. Kama umempata bubu jipange usiogope mtu.

USIKILIZE MOYO WAKO KWANI HAKUNA JAMBO GUMU KAMA KUSHINDA, KULALA NA KUKESHA NA MTU AMBAYE MOYO HAUJAMKUBALI
 
Kumpata mtu sahihi ni kupima roho na damu yake hivi pekee haviongopi.
Roho inabeba tabia na tabia inakaa kwenye damu.
 
Nasoma sasa kitabu cha PR. PAUL SEMBA kinaitwa UFUNGUO WA NDOA.
Mtunzi wa kitabu anasema kama kijana wa kiume au wa kike hawezi kujihudumia mahitaji yake ya msinginya kila siku yeye mwenyewe basi hatoshi kabisa kuowa wala kuolewa hadi atakapoweza kujihudumia mwenyewe.

Kwa paragraph hiii PR PAUL SEMBA amawatangazia mabinti wengi wa kitanzania kwamba hawafai kuolewa
 
Utangulizi
Nimekua nikisoma habari mbalimbali katika mitandao ya kijamii, katika Jambo ambalo linanipa maswali ni mabadiliko ya vigezo vya kuoa au kuolewa

Wakati nikiwa kijana mdogo kuna maswali yalinisumbua sana, mana mtaa ambao nilikuwa naishi ulikuwa na nyumba za watumishi WA umma (magorofa ya TBA) na kwa sehemu kubwa walikuwepo wanasheria na watumishi WA idara zingine za serikali

Marafiki zangu Kwa sehemu kubwa Baba Zao walikuwa wanasheria na mama Zao walikuwa walimu na wachache walikuwa mama WA nyumbani.

Wakati nikiwa katika harakati za kuoa maswali mengi yalikuwa kichwani mwangu juu ya wale wazazi wa rafiki zangu na wazazi wengine ambao nilikuwa nawafahamu.

Kwakweli Kwa sehemu kubwa kulikuwa na ufanano na ndoa hizo sina uhakika Sana juu ya migogoro iliyokuwako kwenye hizo ndoa , nachojua zilitulea na kutufikisha hapa tulipo.

Wakati nataka kuoa niliwaza Sana ni kigezo gani kiwe cha Kwanza na muhimu kwa binti ambaye atakuwa mke wangu?

Kigezo cha Kwanza ambacho kilikuwa moyoni mwangu ni

A. Mwenye Hofu ya Mungu 60%

Kuna tofauti ya kwenda kusali na kuwa na Hofu ya Mungu , kipindi cha kuoa au kuolewa kila mmoja anakwenda kanisani Kwa tumaini la kumpata mweza ndio maana lazime UWE makini, sio kila MTU anayekwenda kanisani ana Hofu ya Mungu

Biblia inasema MTU Mwenye Hofu ya Mungu ni Yule anayeskia neno la Mungu na kutetemeka , unashangaa uko kwenye mahusiano na binti tena ni MTU wa ibada Sana lakini haigopi uzinzi ! Ujue huyo MTU Hana Hofu ya Mungu.

Umesoma habari ya Yusufu alipolazimishwa na mke wa potifa kufanya nae mapenzi ,akakataa akiogopa kumtenda Mungu dhambi.

Leo hii vijana wanapotaka kuoana wanataka Kwanza kufanya ngono Kwanza wajuane Kwanza , ndio maana ndoa nyingi za Leo zina pata shida

B. Mama wa Watoto wangu 30%
Nilijiuliza maswali Huyu binti ambaye nakwenda kumwoa ndiye atakaye kuwa mama wa Watoto wangu?

Kuna kitu ambacho watu wengi Hawajui , tumbo la mwanamke limewekwa na Mungu kupitisha agano la Mungu Kwa mwanadamu

Mungu alisema na Ibrahimu akamwambia utapata mtoto wakiume Kwa Sarah Kwa sababu kwenye tumbo la Sarah Ndiko kuna agano ambalo Mungu alifunga na Ibrahimu ndio maana licha ya Ibrahimu kuwa na watoto wengi lakini ni Isack Tu ndiye aliyepewa urithi wakiagano na Mungu

Kwa hiyo unapochagua binti wakuoa ni lazima ujue anafaa kuwa mama wa Watoto wako?

Kuna tofauti ya kuwa na binti kama girlfriend na binti kama mama WA familia

C. Mwenye kujishughulisha

Ni kweli biblia inatoa maagizo kwamba Baba ndiye ataleta chakula Kwa ajili ya familia, lakini biblia hiyo hiyo inasema mke Mwema ni Yule anayejishughulisha Kwa kazi ya mikono

Leo hii mabinti wengi wanafanya kazi nzuri Tu lakini bado wanategemea fedha Zao kuzitumia Kwa matumizi ya mapambo na hanasa za Dunia lakini za mume ndio zitumuke kwenye familia

D. Na vigezo vingine ambavyo 10%

Vigezo vya Karne ya 21

A. Mwenye Shape au Elimu na fedha 60%

Kitu ambacho kinanisikitisha ni habari za ndoa za SASA watu kuachana hata mwezi hawajafikisha? Umetumia gharama zote za sherehe kubwa lakini ndoa hazidumu Kwa sababu umeangalia kitu kidogo Sana , shape inakwisha, Elimu sio maarifa na fedha zinamabawa Leo ziko kesho haziko, vitu vya nje haviwezi kutunza ndoa
Hivi kweli kuwa na hofu ya Mungu inaweza kusaidia ndoa?

Nikipata muda nitapenda kujadili hii hoja.
 
Waolewaji wanataka mrefu mweusi, mwembamba flani hivi na mwenye vindevu vya hapa.... alafu baadae wanakuja kujikuta single maza ila sisi waoaji hizo sifa hatuna kabisa kabisa
 
Back
Top Bottom