Sella turcica
Senior Member
- Oct 13, 2020
- 103
- 190
Watanzania ni washenzi, nianze kwa kusema hivyo. Tumekabidhi hii nchi mikononi mwa CCM na tumeacha itupeleke kama inavyotaka na hatutaki kuhoji.
Wakati wa uchafuzi mkuu wa 2020 mzee wangu alikuwa anashangilia kwamba wameshinda majimbo yote. Mimi nilimsikiliza tu nikaishia kumsikitikia. Mzee yuko kijijini anashangilia Mbowe kukosa ubunge.
Hivi leo hii Mbowe akiugua ataenda kutibiwa kwenye hospitali ya halmashauri ambayo haina hata gloves? Mtoto wa Mbowe anasoma kwenye shule ya kata ambayo haina walimu wala vifaa vya kujifunzia?
Je, kuna namna yoyote Mbowe anaathirika na hizi tozo tunazolalamikia? Unakuta mtu anasema wapinzani mbona mko kimya kuhusu tozo. Huwa natamani kumtukana huyu mtu, basi tu. Kwenye uchaguzi wawachague kina Mwigulu na Zungu, halafu linapokuja suala la kuwatetea wananchi iwe kazi ya wapinzani, kwa misingi ipi?
Mimi naona wote wanaofanya harakati za kuwatetea watu wanapoteza muda, unless kama kuna malipo kwa ajili ya hiyo kazi. Unamtetea mtu ambaye ukikamatwa anasema una kiherehere. Tundu Lissu alijitoa kusema ukweli tangu mwanzo ambapo mikataba ya kilaghai inasainiwa na kupitishwa na wabunge wa CCM.
Juzi Magufuli anajifanya kusema tunaibiwa ilhali alikuwa bungeni wakati mikataba inapitishwa. Lissu hakuchoka kusema ukweli, leo hii wamekuja kuthibitisha kuwa zile reports za kin prof Osoro zilikuwa professorial rubbish. Cha ajabu Lissu anaitwa msaliti na kuna watu walitamani afe.
Watanzania hawa leo wanaona wabunge wa CCM wanachofanya kule bungeni. Badala ya kuisimamia serikali wao wanasimama na serikali kuwakandamiza wananchi, lakini cha ajabu uchaguzi ukija watawachagua tena.
Watanzania hatujielewi, wacha serikali ya CCM itunyooshe vizuri huenda akili zikatujia. wanaopaza sauti watulie tuli dawa iingie. Dawa ikikolea vizuri wananchi wenyewe watasimama kudai haki zao bila kushawishiwa na mtu. Kama haufadiki directly na harakati bora utulie ufanye mambo yako ya msingi.
Nawasilisha.
Wakati wa uchafuzi mkuu wa 2020 mzee wangu alikuwa anashangilia kwamba wameshinda majimbo yote. Mimi nilimsikiliza tu nikaishia kumsikitikia. Mzee yuko kijijini anashangilia Mbowe kukosa ubunge.
Hivi leo hii Mbowe akiugua ataenda kutibiwa kwenye hospitali ya halmashauri ambayo haina hata gloves? Mtoto wa Mbowe anasoma kwenye shule ya kata ambayo haina walimu wala vifaa vya kujifunzia?
Je, kuna namna yoyote Mbowe anaathirika na hizi tozo tunazolalamikia? Unakuta mtu anasema wapinzani mbona mko kimya kuhusu tozo. Huwa natamani kumtukana huyu mtu, basi tu. Kwenye uchaguzi wawachague kina Mwigulu na Zungu, halafu linapokuja suala la kuwatetea wananchi iwe kazi ya wapinzani, kwa misingi ipi?
Mimi naona wote wanaofanya harakati za kuwatetea watu wanapoteza muda, unless kama kuna malipo kwa ajili ya hiyo kazi. Unamtetea mtu ambaye ukikamatwa anasema una kiherehere. Tundu Lissu alijitoa kusema ukweli tangu mwanzo ambapo mikataba ya kilaghai inasainiwa na kupitishwa na wabunge wa CCM.
Juzi Magufuli anajifanya kusema tunaibiwa ilhali alikuwa bungeni wakati mikataba inapitishwa. Lissu hakuchoka kusema ukweli, leo hii wamekuja kuthibitisha kuwa zile reports za kin prof Osoro zilikuwa professorial rubbish. Cha ajabu Lissu anaitwa msaliti na kuna watu walitamani afe.
Watanzania hawa leo wanaona wabunge wa CCM wanachofanya kule bungeni. Badala ya kuisimamia serikali wao wanasimama na serikali kuwakandamiza wananchi, lakini cha ajabu uchaguzi ukija watawachagua tena.
Watanzania hatujielewi, wacha serikali ya CCM itunyooshe vizuri huenda akili zikatujia. wanaopaza sauti watulie tuli dawa iingie. Dawa ikikolea vizuri wananchi wenyewe watasimama kudai haki zao bila kushawishiwa na mtu. Kama haufadiki directly na harakati bora utulie ufanye mambo yako ya msingi.
Nawasilisha.