Kuwa first born sometimes ni shida

Kuwa first born sometimes ni shida

Amebaki dogo mmoja yuko mwaka wa pili huu dah ananiumiza kichwa sana. Chuo private, ada mil 3.2 plus gharama zingine zote. Sasa hivi sina laptop karibia mwaka sasa, aliichukua yeye asomee.

Najiona kabisa saa hizi namiliki hiki na hiki ila ndio hivyo pesa inaenda kwake. Acha amalize nile bata.
Mimi juzi dogo anaingia six wamefungua shule mwezi wa saba Ada hamna na anadaiwa ya term iliyoisha. Mshahara ulipoingia nilitoa Kama ulivyo nikamtumia, Yani tuseme nasurvive kwa nguvu za muumba.
 
Hongera kama wazazi wameweza kukutegemea japo kipato hakitoshi. Ni vita kubwa ya kiroho wamepambana nawe pia umepambana bila kujijua maybe hadi wewe umefika hapo.
Kuna wazazi wengi watoto zao wa kwanza hawawezi hata kuwategemea kwa ushauri maana mshale wa dira upo kusini badala ya kaskazini yaani kama ni dish la kiroho lilishaaguka kabisa no chanel.

Maan mtoto wa kwanza ni vuno bora linalotafutwa na Muumba pamoja na ibirisi. Wote hao wanakuwinda wachukue hesabu yako kwako.. Ibilisi anapiga kichwa cha familia/first born ili familia iivurugike na Mungu anataka akiongeze kichwa cha familia ili familia isipalanganyike. Kama mzazi au mzaliwa wa kwanza usipojitambua utaishia kubaya.
Hongera sana kwa hilo maana tambua kwamba Mafanikio yako si ajili yako bali kwa ajili ya wae walio nyuma yako. Siku moja kidogo hicho kitaongezeka usivunjike moyo
Tembea na kanuni hii... Family- Duty- and Honor

Family always come first
mzee do you believe in spirituality?
 
Mimi juzi dogo anaingia six wamefungua shule mwezi wa sita Ada hamna na anadaiwa ya term iliyoisha. Mshahara ulipoingia nilitoa Kama ulivyo nikamtumia, Yani tuseme nasurvive kwa nguvu za muumba.
damn!!! halafu unasikia kafanya ujinga kafeli
 
Kwetu mzaliwa wa kwanza aliipata, yote aliyabeba yeye hadi kuweka umeme maji na vyote.

Ajabu wifi yangu anamwita... nyundo.. eti ni mbahili.

Wazaliwa wa kwanza Mungu awatie nguvu.
 
Wadogo zangu wawili wananielewa vema sana nipoje

Huwa sicheki nao kabisaaaa, ukiomba hela ya shule unatakiwa kuja na maendeleo yako ya shule kama huwezi kajitafutie

Kwenye maswala ya shule sicheki na kima yoyote

Na nimewaambia mkishindwa kila mtu akatafutr pa kukaa sio kwenda kusumbua wazee
kama amefeli inakuaje?
 
Nilikutana na mtu mmoja wa kanda fulani akaniambia, jamii nyingi kwenye familia wanatumia mtoto wa kwanza kutanya matambiko yao ambayo huwaathiri wao na maisha yao.
Akaniambia nichunguze mafanikio ya first born wengi na mikasa ya maisha wanayokutana nayo.
Nilikuwa mnyonge sana japo sijui ukweli wa hili.

Lakini Mungu ndiye anaamua hatma ya maisha ya kila kiumbe.

Sent from my Nokia 3.1 using JamiiForums mobile app
First Born wanapitia mengi
 
Hii inanihusu sana, sina uhusiano mazuri na babaangu japo nampenda....
Mzee wangu alidakwa na Malaya kabla ya kustaafu Kazi wakala mafao na bidada mpya, mama akafa kwa presha bado inaniuma sana
duh!! hatari sana
 
Habari zenu wakuu,

Jamani maFirst born hasa tuliozaliwa kwenye hizi familia zetu za kipato cha kawaida nadhani msoto wa kukabidhiwa majukumu kabla ya wakati mnaujua.

Yani umepata kibarua Chako hata we mwenyewe hujimudu vizuri, unakabidhiwa mdogo wako umsomeshe na majukumu mengine ya nyumbani usaidie. Yani wadogo zako wao slope tu, kitu kidogo mtafuteni kaka/dada Yani ushatwikwa majukumu Kama yote.

maFirst born mliobeba majukumu ya mzazi popote mlipo hongera zenu.
Mkuu tupo!
 
Hii ni kweli

Mi nasererekaa na slope/kitonga kwa bro zangu

Full kuwapa majukumu

Kuzaliwa wa kwanza noma sana
 
1st born mna raha hasa kipindi mnasoma.
Mahitaji yote muhimu mnapewa ,yaani macho yote yanakuwa kwenu.
Wasaidieni wazazi kutusomesha.

Sent using Jamii Forums mobile app
Yaan first born anapewaga privilege kubwa sana...

Na ndio maana na mimi nawatwisha mizigo, maana utotoni wametupokonya haki zetu
 
Habari zenu wakuu,

Jamani maFirst born hasa tuliozaliwa kwenye hizi familia zetu za kipato cha kawaida nadhani msoto wa kukabidhiwa majukumu kabla ya wakati mnaujua.

Yani umepata kibarua Chako hata we mwenyewe hujimudu vizuri, unakabidhiwa mdogo wako umsomeshe na majukumu mengine ya nyumbani usaidie. Yani wadogo zako wao slope tu, kitu kidogo mtafuteni kaka/dada Yani ushatwikwa majukumu Kama yote.

maFirst born mliobeba majukumu ya mzazi popote mlipo hongera zenu.

Mkuu uzao wa kwanza ni baraka, umepewa pendeleo hilo ili uwe dira ya wale watakaozaliwa nyuma yako, kumsaidia mtu haitaji kuwa na mali nyingi bali ni roho ya kusaidia, mfano ikiwa utamchukuwa ndugu yako ukaa naye hata kama kula yenu ni ya kuhausle ni kwa mbinde huyo ndugu yako utaona hilo na atakuombea ufanikiwe ili iwe nafuu kwakwe, Karma husaidia mwenye kusafia wengine sio tofauti na hapo
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom