Mparee2
JF-Expert Member
- Sep 2, 2012
- 2,591
- 4,279
Nimekuwa natafakari hili jambo la kutumia Quran/Biblia kwenye kiapo naona kama halipo sawa; kwani linakosa uhalisia; hii ni kwa sababu zifuatazo;
1. Kile kinacho apiwa hakitumii sheria wala taratibu za dini husika.
2. Kuapa kwa kutumia kitabu kitakatifu na ndani ya muda mfupi mtu aende kinyume Mf: Kudanganya mahakamani ni kutenda kosa la pili kwa mwenyezi Mungu (Kudanganya).
3. Baadhi ya wanao apa hawana elimu yoyote ya dini husika zaidi ya kuitwa jina linalo endana na hiyo dini hivyo ni sawa na kudhalilisha kitabu husika.
5. Baadhi ya wanao apa wangestahili waongozwe na masheikh/wachungaji sala ya toba wamrudie kwanza Mungu kabla ya kushika kitabu kitakatifu na kuapa kitu ambacho hakifanyiki
Kwa sababu hizo, Napendekeza viapo vyote vifanywe kwa kutumia KATIBA ambayo ndiyo Sheria itakayo muhukumu muapaji pale atakapokwenda kinyume na kiapo chake.
1. Kile kinacho apiwa hakitumii sheria wala taratibu za dini husika.
2. Kuapa kwa kutumia kitabu kitakatifu na ndani ya muda mfupi mtu aende kinyume Mf: Kudanganya mahakamani ni kutenda kosa la pili kwa mwenyezi Mungu (Kudanganya).
3. Baadhi ya wanao apa hawana elimu yoyote ya dini husika zaidi ya kuitwa jina linalo endana na hiyo dini hivyo ni sawa na kudhalilisha kitabu husika.
5. Baadhi ya wanao apa wangestahili waongozwe na masheikh/wachungaji sala ya toba wamrudie kwanza Mungu kabla ya kushika kitabu kitakatifu na kuapa kitu ambacho hakifanyiki
Kwa sababu hizo, Napendekeza viapo vyote vifanywe kwa kutumia KATIBA ambayo ndiyo Sheria itakayo muhukumu muapaji pale atakapokwenda kinyume na kiapo chake.