Kutumia Dola ni kukosa hoja?

Kutumia Dola ni kukosa hoja?

Mimi ninachojua ,Bashiru alikuwa anaiongelea dola(serikali) na sio vyombo vya dola (polisi n.k). Mafanikio ya serikali ndio uhakika Wa chama chenye madaraka kuendelea kutawala kwa kuwa serikali ndio dola inayochaguliwa na watu.
Kwahiyo mafanikio ya serikali si yanaelezewa kwa hoja? Ama unadhani alichokisema katibu mkuu hakitokei? Unataka kusema ccm inatumia serikali dhidi ya upinzani na polisi wanawatumiaje?

Dola ni serikali na siyo polisi? Are you serious?
 
Midahalo inapima uwezo wa kujieleza kwa kiongozi anayekusudia kuomba nafasi kubwa za uongozi,na lengo ni kujua na kutambua uwezo wa huyo kiongozi tarajiwa kwenye mambo mbalimbali ya kidunia ili ikitokea amepewa nafasi ya kuongea kwenye mikutano ya kimataifa asibabaike au kuogopa mikutano ya kimataifa. Ni aibu kwa nchi kuwa na kiongozi parochial kwenye mambo ya kidunia maana Rais ni nembo ya Taifa akiwa empty minded ni sawa na kuwa nchi na wananchi wake ni empty minded pia
Well said mkuu!
cc MsemajiUkweli
 
Kwa hiyo ili msalie Madarakani mnategemea dola..?
Bila Dola ni wepesi kweli kweli. Ccm ni chama dola. Kinaiongoza nchi yetu kifashisti. Ukiona chama kinaweza kuleta watu wanaoonekana kama vichaa ujuwe kuna tatizo pahala.

Kuna mambo yanayofanywa na ccm kwa kupitia hao viongozi wao kwa kutumia dola, ambayo yanafanya mtu ujiulize utimamu wao wa akili.

Mdahalo utasaidia sana kufahamu mapungufu mengi. Mfano marekani, huwezi kuwa rais kama huwezi kujieleza mbele ya umma na kujenga hoja.
 
Unataka kusema ccm siyo chama cha siasa bali ndiyo dola yenyewe siyo ?

Hivi ccm bado kinaweza kusimamia hoja ipi kwa sasa na kikawashawishi wananchi ?

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu ccm ni dola na dola ni ccm! It is reciprocal! Ndo maana unaona wanajeshi na mapolisi, sambamba na viongozi wengine kwenye majeshi yetu, kufadhiliwa na kupewa vyeo na serikali ya ccm mara baada ya kustaafu. Wengine wanaingizwa kwenye nafasi za kiutendaji serikalini, mfano ukuu wa mkoa nk.

Kuna “quid pro quo” kwenye huu mfumo hasi. Yani nipe nikupe.
Tusipopambana sasa hivi, tutakuja kushangaa kwa kutokuona utofauti kati ya ccm na majeshi yetu ya ulinzi ambayo yanatakiwa kuwa neutral inapokuja kwenye siasa na utendaji wao.
 
CCM imechokwa hata kijenge barabara zilizinakshiwa kwa Dhahabu bado Wananchi wanataka mabadiliko

CCM hawawezi kushindana na wakati nyakati zimebadilika sana sana

Chama hiki cha kukomunisti hata kikija na mbinu gani bado kitang'oka tu

View attachment 1379053
Hiki chama hakifai tena. Ni vyema kikafa tuanze upya. Au kuwepo na katiba mpya. Chini ya mfumo huu tutakuja kujuta sana huko mbeleni. Kama tukiponea kuingia kwenye full dictatorship tushukuru sana. Lakini huu ndo wakati ambao mapungufu karibia yote ya mfumo huu yanaonekana na kufahamika na walio wengi.

Ni kweli ccm imejisahau kama kupe, ambaye kuanzia ng’ombe anapochinjwa yeye hana habari, ngozi inaanikwa hadi inakuja kuwambwa anafia humo!

Nyakati hizi ni za tofauti. Hatuwezi kuendelea na mfumo wa “ukomunisti uchwara”
 
Kwa ujumla katibu mkuu wa CCM amekuwa mkweli. Vyama mbadala vitumie uelewa huo kupanga mikakati mbadala. Kwa mfano kutafisiri sheria na kuzikomalia kwa nguvu ya umma. Wasisahau kutakuwa na gharama hadi ya maisha ya watu.
 
Mimi nadhani hamkuelewa kauli ya katibu na tatizo letu watanzania kila kauli kutoka ccm uwa tunaichukulia kipinzani naomba ukasikilize tena maana Juma kaparatu aliomba katibu aweke sawa maelezo na aliongea vizur usipotoshe uma


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwa ujumla katibu mkuu wa ccm amekuwa mkweli. Vyama mbadala vitumie uelewa huo kupanga mikakati mbadala. Kwa mfano kutafisiri sheria na kuzikomalia kwa nguvu ya umma. Wasisahau kutakuwa na gharama hadi ya maisha ya watu.
Hapa kwa kifupi umesema kwamba ccm haiwezi kuacha kutumia dola dhidi ya wapinzani wa kisiasa.

Pia nimekuelewa kwamba wapinzani watumie nguvu ya umma dhidi ya dola inapotumwa na ccm.

Huko binafsi ninaombea tusifike, kwasababu inaweza kusabanisha “civil strifes”, kwasababu ccm ni chama dola lakini si kina wanachama mtaani ambao pia wanatumika wakisaidiwa na dola? Mfano mkutano wa juzi wa Mbowe na pia Alphonce Mawazo na wengine wengi tu.
 
Mimi nadhani hamkuelewa kauli ya katibu na tatizo letu watanzania kila kauli kutoka ccm uwa tunaichukulia kipinzani naomba ukasikilize tena maana Juma kaparatu aliomba katibu aweke sawa maelezo na aliongea vizur usipotoshe uma


Sent using Jamii Forums mobile app
Ebu weka hiyo kauli hapa tuione. Kwani wewe umeelewa vipi? Sina nia ya upotoshaji.
 
jmushi1,
Hiki Chama kinajieleza kuwa kinawatetea wakulima na wafanyakazi ukiangalia vizuri wakulima wanamaisha duni ya kutisha na wanazidi kuwa masikini hali kadhalika wafanyakazi mishahara haiongezwi mifuko yao ya pensheni inakombwa na kuporwa fedha na CCM

CCM kinatetea matumbo yao na kwa mujibu wa Katibu wake mpya anasema kuwa Chama hakitakabidhi madaraka kwa Watanzania hiyo ni kauli ya kushindwa.
 
Hiki Chama kinajieleza kuwa kinawatetea wakulima na wafanyakazi ukiangalia vizuri wakulima wanamaisha duni ya kutisha na wanazidi kuwa masikini hali kadhalika wafanyakazi mishahara haiongezwi mifuko yao ya pensheni inakombwa na kuporwa fedha na CCM

CCM kinatetea matumbo yao na kwa mujibu wa Katibu wake mpya anasema kuwa Chama hakitakabidhi madaraka kwa Watanzania hiyo ni kauli ya kushindwa.
Asilimia zaidi ya tisini ya wananchi wa Tanzania ni wakulima. Badala ya kuwaeleza wakulima utawasaidia vipi, wewe unachagua kutumia dola na wala huna haja ya kutumia hoja kwasababu wananchi hawajitambui? Wanachokifanya ccm kinaonyedha dharau kubwa sana kwa wananchi na ni sawa na kuutukana ufahamu wetu!

ccm ingewasaidia wakulima kidogo tu bila kujali matumbo yao nchi ungekuta iko mbali sana! Kwanza hivyo viwanda ungekuta vina uhitaji bila kulazimishiwa. Wao wamebakia na bombadia na hawataki kuhojiwa na huku wanachokifanya ni kuzitolea maamuzi pesa zetu wananchi bila ya kutushirikisha. Mfano kungekuwepo na midahalo ingesaidia sana! Na mfumo huu utakufa ccm ikifa.
 
Halafu wengine wanamtetea eti tumemuelewa vibaya...msomi kama yeye anawezaje kusema vitu halafu hadhira isielewe..??
Jinsi wanavyojitetea, ndivyo wanavyozidi kujifunga! Madai yao yangekuwa na ukweli wowote, basi tusingeona hila na unyanyasaji dhidi ya wapinzani.

Kizuri chajiuza, kibaya chajitembeza.
 
Huna lolote upeasant tu umekujaa, unafananisha vitu visivyo fanana.
Hoja yake ni mfu, eti anadai kuwa ccm kutumia dola na taasisi nyingine za umma ndiko kumeleta amani nchini. Hao ni wale waliokunywa maji ya bendera ya chama cha kifashisti.

ccm ni lazima ivunjwe. Au ifumuliwe kabisa. Mfumo wake ni kama wa Ba’ath Party kile cha Saddam Hussein wa Iraq.
 
Policeccm ndio wanawabeba,ndio mana police n traffic awamu hii wanachukua rushwa hadharani mana wanajua meko anawategemea wao kutawala

Sent using Jamii Forums mobile app

Uko sahihi sana, tena huko tuendako viongozi wa vyombo vya dola watachukua madaraka maana wataona mbona wao ndio wanawalinda raia ambao wanakaa madarakani bila kupitia njia ya kura?
 
Asilimia zaidi ya tisini ya wananchi wa Tanzania ni wakulima. Badala ya kuwaeleza wakulima utawasaidia vipi, wewe unachagua kutumia dola na wala huna haja ya kutumia hoja kwasababu wananchi hawajitambui? Wanachokifanya ccm kinaonyedha dharau kubwa sana kwa wananchi na ni sawa na kuutukana ufahamu wetu!

ccm ingewasaidia wakulima kidogo tu bila kujali matumbo yao nchi ungekuta iko mbali sana! Kwanza hivyo viwanda ungekuta vina uhitaji bila kulazimishiwa. Wao wamebakia na bombadia na hawataki kuhojiwa na huku wanachokifanya ni kuzitolea maamuzi pesa zetu wananchi bila ya kutushirikisha. Mfano kungekuwepo na midahalo ingesaidia sana! Na mfumo huu utakufa ccm ikifa.
Chama kilichowekwa madarakani kwa ahadi ya kuwakomboa watanzania sasa kimekuwa Chama cha wababe kinatawala kimabavu na kufikia kuuwa watanzania wanaokikosoa hata wenye kuhoji Phd ya kiongozi wanaishia kwenye Chainsaw CCM kimekosa uhalali wa kuiongoza nchi hii sasa kinatumia Polisi na vyombo vingine katika kuliteketeza taifa

Busara zimetoweka badala yake amri matamko na mizengwe ndio imekuwa sera mpya

Wakuu wa mikoa ambao hawajachaguliwa na Watanzania ndio wanapewa fimbo za kukomoa na kuwatisha wananchi
 
Back
Top Bottom