Maswala ya mimi kumpenda Zitto hadi nikalale naye unayaona mazuri sana na matamu, wengine wasiseme lolote juu yako wewe. Alaa unapofungua milango anaruhusu mambo haya na wala mimi siandiki kitu kama hujaelekea kuacha hoja unanifuata mimi. Hakuna hoja yako hata moja umezingatia Hoja iliyopo isipokuwa Mkandara na Zittto mbona miye sisemei Freeland na Slaa au Mbowe!
Bila shaka nilichoandika ndicho nilichokisoma ni hoja yangu kwamba mngetumia akili japo kidogo msingeendeleza hizi siasa za Utengano ambazo sisi wengine zimetutoa Chadema na UKAWA sitoiunga mkono hata kwa nini na nipo hapa kuipiga vita. Naamini na nitaendelea kuamini Chadema niloijua mimi baada ya 2010 ingeweza kabisa kuchukua majimbo mengi kuliko UKAWA na ingeweza kuwa chama pinzani kuua vyama vyote vingnevyo kama chama kingekubali mabadiliko ( Changes) kutenganisha Uongozi wa chama na Serikali na kutumikia sheria na kanuni walozweka ili kuonyesha mfano bora.
Udini umewaingia kiasi kwamba mmesahau kuwa Chadema haikuanza hivi mnakuwa kama CUF ya kabla ya uchaguzi wa 2010 mnajitangaza na Ukristu wenu sana halafu mkiambiwa mnakataa, sisi wengine sio mazuzu kiasi hicho. Siasa za separation athari zake ndio hizi na inawabidi muwe tayari kuzipokea..