Hivi umejisoma vizuri mkuu wangu. Kama tume imerasimisha utengano ulokuwepo utasemaje tume hiyo imeunda serikali 3 za Muungano wa kweli na sio Utengano wa kweli? Mimi nawashangaa sana mnapotumia ati S3 ni kuudumisha muungano ilihali mnajua mnachokifanya ni kutenganisha kile mnachoamini kimesha kuwa na Utengano basi bora Tutengane. Na ndivyo navyowasoma miye siku zote..Mkandara utengano umekuwapo siku zote na umeendelea kuwa mkubwa baada ya Mwalimu kufariki. Mapendekezo ya iliyokuwa tume ya kabadiliko ya katiba yalikuwa kurasimisha utangano huo. Muungano wa kweli utapatikana ktk serikali tatu na si vinyinevyo kwa mujibu wa maoni ya wananchi.
Ukawa utasimamia serikali tatu na yeyote atakayetaka kujiunga awe tayari kukubaliana na hilo.
Kwa nini UKAWA msiwe wakweli muwaambie wananchi tunagenganisha - Zanzibar Kivyao na Tanganyika Kivyao halafu tuone kama wananchi watakuwa nanyi katika mbiu hiyo badala ya kutumia lugha za ulaghai..Semeni wazi tunataka UTENGANO maana upo siku zote tunarasimisha hakuna sababu ya kukataa kilichokuwepo.