Kutoka Bungeni: 2006 - 2010

Kutoka Bungeni: 2006 - 2010

Mradi upi wa Umeme? kwa ninavyo jua Stiggler Gorge kwa wakati ule ulikuwa mradi mkubwa saana kwetu na hizo Megawatts 3,000 tulikuwa hatuna mahali pa kuzitumia, lakini sasa ni wakati muuafaka. Reli iliondolewa au kungolewa kwa sababu ya kuanguka kwa zao la karanga kama sikosei etc, lakini pia ungeonyesha mwenyewe need ya kuwepo Reli huko kwa kuwepo production fulani ambayo wakati ule wa Mwl ulikwazwa kutokana na kutokuwepo kwa Reli infact Reli yenyewe ilikuwa inatoka Nachingwe kwenda bandarini Mtwara/Lindi kama sikosei.
Unajua wewe GT ni msomi , kwa hiyo muono wako unatakiwa kulenga huko kuliko kila kitu Mwalimu Mwalimu etc etc inakuwa kama una Personnal Vandetta nae, kwa mfano jana uliingiza mambo ya ufuska wa Slaa mahali pasipo pake, hivyo unapoteza maana zima ya suala unaloongelea hata kama uko sawa, tatizo ni mahali pa ku-advocate hilo suala, ni sawa unaulizwa hesabu ya kutoa wewe unajibu kwa kugawanya. (- unaifanya /)
Hata hapa tunaweza kuongelea mambo mengi ya kusini mfano huo wa Muhidhiri, lakini ni vizuri uka-stick to that point badala ya kuchanganya Pilau na Maharage na vyakula ambavyo haviendani pamoja. Mimi mwenyewe niko concern kwanini hatutumia nafasi tulizo nazo kujenga kusini kwa sasa huko nyuma na alot of theories ambazo zinaweza kuwa kweli au uongo, mfano vita ya Msumbiji mpaka 1975, uwezo wa nchi wakati ule, na vichocheo vingine vya investment, kama rasilimali watu, etc Usafiri wa watu etc. hata kaja Mkapa wa kwetu na ameshindwa kukamilisha vizuri hiyo barabara, kaamua kuka Ushoto.

Ni mawazo mazuri sana , yanayo attract comments.
1 Steiglers Gorge yenye potential ya kuzalisha 3000MW kwa wakati huo
ingekuwa uwekezaji mzuri sana wa kimaendeleo.Msumbiji walijenga Dam
la aina hiyo(wakoloni wa wakati huo) na hata leo wanauza sana umeme
Kusini.Lazima tukubali kuwa wakati huo upeo wa uwekezaji bado ulikuwa
mdogo.

2 Mradi wa Karanga (Ground Nut Scheme) ilikuwa mradi wa kikoloni ambao
ukaja onekana kuwa not feasible.Reli hiyo toka Nachingwea hadi Mtwara (160km) ilikuwa kwa ajili ya mradi wa Karanga Nachingwea(OFC-Overseas Food Corporation).Mradi ulifeli hivyo ile economic use yake kutokuwa na manufaa.Pengine tungekuwa matariri wakati huo isingeng'olewa na kupelekwa Tanga line

3 Hat hivyo ni watu wachache wanaofika Mtwara /Lindi lakini leo ukiacha 60km za Ikwiriri(Mkapa Bridge) Hadi Somanga barabara ni lami tupu.Kuna maendelezo mazuri kuelekea Unity bridge kwa mradi wa ufadhili wa Japan unaoendelea.

Siku za watu wa Mtwara /Lindi kulalamika zimehesabika na hatimae kuisha kabisa
 
Fahamuni kwamba tuhuma za Mudhihiri ni mwanzo tu
Kuna matatizomengi sana ya chinichini huyu mama waziri anayasababisha bilakujali.

.

Sasa hapa mwananchi mbona wanasema Membe kajitokeza kusema aliyesemwa ni yeye? soma hapa wala si huyo mama.

Kombora la Mbunge Mudhihir lamtikisa Waziri Membe
membe.jpg
*Ajitetea anamheshimu, atajibu kwenye vyombo vya mkoa

Na Ramadhan Semtawa

MBUNGE wa Mchinga, Mudhihir Mudhihir hakutaja jina la waziri aliyemfananisha na "nyoka wa mdimu", lakini akasema kondoo wa manyoya atazizima mwenyewe na kujitokeza hadharani.

Jana Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernad Membe alijitokeza na kusema kuwa amepigiwa simu na watu wengine waliomwambia kuwa makombora hayo ya Mudhihir yanaelekezwa kwake na hivyo atachukua hatua kwa kulifikisha suala hilo kwenye vikao vya chama na serikali vya wilaya na mkoa.

Mudhihir, mmoja wa wabunge wenye kupenda kutumia misemo na methali huku akinukuu wanafalsa na vitabu mbalimbali, juzi alimlaumu mtu huyo kuwa ndiye anayetaka kiwanda cha saruji kijengwe kilomita 35 kutoka eneo lenye malighafi ambalo ni Mchinga.

Alisema mtu huyo, ambaye alimuelezea kuwa atawania urais katika uchaguzi wa mwaka 2015 anafanya hivyo kwa roho mbaya kwa kuwa hatanufaika lolote na msimamo wake kuhusu kujengwa kwa kiwanda hicho na kumfananisha na nyoka anayeishi kwenye mti wa ndimu ambaye hali majani yake wala ndimu, lakini mtu anayekwenda kuchuma ndimu kwenye mti huo humng'ata.

"Unajua nyoka wa mdimu ana hila sana; anapenda kukaa kwenye mdimu, lakini hali ndimu, ila akija mtu anayetaka kuchuma ndimu humshambulia, sasa yeye kiwanda kinataka kujengwa Mchinga, lakini anakizuia," alisema Mudhihir juzi.

Mudhihir, ambaye alikuwa akitumia mafumbo kwa kunukuu wanafalsafa mbalimbali, alitetea uamuzi wake wa kueleza bayana suala hilo alipotumia mfano wa mwendawazimu ambaye anatembea huku akizungumza kwa sauti na mtu mwingine ambaye anatembea akiwaza akilini masuala tofauti.

"Wote ni sawa, tofauti yake ni kwamba mmoja anazungumza kwa sauti na mwingine anazungumza kimyakimya," alisema mbunge huyo ambaye ni mwanafasihi.


Mudhihir pia alimnukuu mwanafalsafa ambaye alisema mtu ambaye hatumii akili yake, mambo humgeuka na akili huanza kumtumia yeye.

Wakati akitoa hoja na mifano yake, Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Bunge, Sera na Uratibu), Philip Marmo aliingilia kati na kutaka wachangiaji wawe wanataja majina ya mawaziri wanaowatuhumu badala ya kutoa tuhuma za jumla. Alidai kuwa tabia hiyo imeanza kukomaa tangu mbunge wa Nzega, Lucas Selelii alipolituhumu baraza zima la mawaziri na kuliombea laana.

Hata hivyo, Spika Samuel Sitta alimtetea akisema hawezi kumlazimisha kila mchangiaji amtaje waziri anayemtuhumu, na badala yake akashauri wachangiaji waeleze kuwa wataliwasilisha jina la waziri anayetuhumiwa kwa Waziri Mkuu Pinda.


Alipoulizwa na Mwananchi jana, Waziri Membe alisema, tayari pia alishapata simu nyingi kutoka Lindi na watu wengine ambao walimwambia kuwa ndiye alikuwa akitajwa na Mudhihir.

"Sikusikia hiyo hotuba, lakini nimepata simu nyingi kutoka Lindi zikinieleza kwamba, mimi ndiye nilikuwa nikitajwa," alikiri Membe.

Membe jana alisema baada ya kupata simu hizo kutoka Lindi, ameamua kujiandaa kulitolea suala hilo ufafanuzi katika vikao vya chama na serikali ngazi za wilaya na mkoa ili lieleweke vema na kuondoa hisia za uadui na chuki kwa watu ambao wanatoka katika mkoa mmoja na wanaoheshimiana.


"Nimeamua kulitolea ufafanuzi (halmashauri kuu ya CCM) NEC wilaya, kikao cha baraza la ushauri la mkoa. Haya ni mambo ya aibu hatuwezi kulipuana hadharani," alifafanua Membe.

Membe, ambaye ni mmoja wa wabunge wanaotokea mkoa wa Lindi, aliongeza kusema: "Nisingependa kufanya malumbano na ndugu yangu Mudhihir."

Alisema anamheshimu Mudhihir kwa muda mrefu na ni ndugu yake, hivyo ni vema jambo hilo akalizungumzia kwenye vikao hivyo ili kuondoa malumbano zaidi hadharani.

"Niko tayari kwenda Mchinga. Nitazungumza na wananchi wa kule ili waweze kuelewa vema suala hili," aliongeza.

Waziri huyo aliongeza kwamba yeye ni mtu wa maadili hivyo asingependa kukaa na kuzungumza mambo ya aibu hadharani bila kufuata maadili.

"Unajua katika kazi kuna mambo ya ethics (maadili), sasa sitaki kuanza kukaa na kuvunja maadili hayo, mimi ni mtu ambaye najiheshimu na nafanya kazi kwa misingi na miiko ya kazi," alifafanua.

Alipoulizwa iwapo anahisi matamshi ya Mudhihir yana msukumo wa maadui wake kisiasa ambao wanahisi anaweza kugombea urais 2015, Membe alisema kwa vyovyote itakuwa hivyo.

"Bila shaka ... bila shaka. Mudhihiri ninayemfahamu mimi asingeweza kutoa matamshi ya aina ile, lakini nasema sihitaji kulumbana naye namheshimu sana," alisisitiza Membe.

Membe aliongeza kwamba yeye si kampuni inayofanya mradi huo, hivyo hata akituhumiwa inakuwa ngumu kuelewa na hivyo kulimaliza suala hilo ataliripoti kwenye vikao husika.

"Kwa unyenyekevu mkubwa, nitalifafanua hili ili kuondoa haya malumbano ya aibu," alisema.

Alipoulizwa jana, Mudhihir, ambaye aliwahi kuwa naibu waziri kwenye Wizara ya Elimu na Utamaduni, alijibu: "Mtu niliyemtaja ni kondoo wa manyoya ambaye ni yeyote atakayezizima."

Alipokuwa akisisitiza hoja hiyo awali, Mudhihir aliapa kwamba waziri huyo ambaye anataka urais mwaka 2015, hata akiwa rais hakuna malighafi itakayochukuliwa kutoka Mchinga.

Tangu kuanza kwa bunge la bajeti, kumekuwa na makombora mbalimbali ya wabunge dhidi ya mawaziri na baraza zima la mawaziri.

Mbunge wa kwanza kuanza kulipua mawaziri alikuwa Selelii ambaye alililaani baraza hilo akisema limejaa watu wenye roho mbaya na wanaotaka kukwamisha baadhi ya wabunge majimboni kwao. Wengine waliotoa shutuma nzito kwa mawaziri ni mbunge wa Maswa, John Shibuda, aliyehoji kipimo cha uzalendo cha baraza hilo, huku akilituhumu kuwa ndilo linalobariki mikataba ya kifisadi.
 
kwa kifupi alisema ni waziri wa kusini huko kwao...ina mana aidha membe au hawa ghasia...so Mwandosya hapa ni out of question..pls mzee wa pwani usichanganyane mchanga na kitumbua ...
 
Huyu ndio Nyerere GT anayedai alikwanza na anaendelea kukwaza maendeleo ya KusiniKombora la Mbunge Mudhihir lamtikisa Waziri Membe
membe.jpg
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernad Membe, ametikiswa na kombora la Mbunge Mudhihir Mudhihir .
broken-heart.jpg
*Ajitetea anamheshimu, atajibu kwenye vyombo vya mkoa

Na Ramadhan Semtawa

MBUNGE wa Mchinga, Mudhihir Mudhihir hakutaja jina la waziri aliyemfananisha na "nyoka wa mdimu", lakini akasema kondoo wa manyoya atazizima mwenyewe na kujitokeza hadharani.

Jana Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernad Membe alijitokeza na kusema kuwa amepigiwa simu na watu wengine waliomwambia kuwa makombora hayo ya Mudhihir yanaelekezwa kwake na hivyo atachukua hatua kwa kulifikisha suala hilo kwenye vikao vya chama na serikali vya wilaya na mkoa.

Mudhihir, mmoja wa wabunge wenye kupenda kutumia misemo na methali huku akinukuu wanafalsa na vitabu mbalimbali, juzi alimlaumu mtu huyo kuwa ndiye anayetaka kiwanda cha saruji kijengwe kilomita 35 kutoka eneo lenye malighafi ambalo ni Mchinga.

Alisema mtu huyo, ambaye alimuelezea kuwa atawania urais katika uchaguzi wa mwaka 2015 anafanya hivyo kwa roho mbaya kwa kuwa hatanufaika lolote na msimamo wake kuhusu kujengwa kwa kiwanda hicho na kumfananisha na nyoka anayeishi kwenye mti wa ndimu ambaye hali majani yake wala ndimu, lakini mtu anayekwenda kuchuma ndimu kwenye mti huo humng'ata.

"Unajua nyoka wa mdimu ana hila sana; anapenda kukaa kwenye mdimu, lakini hali ndimu, ila akija mtu anayetaka kuchuma ndimu humshambulia, sasa yeye kiwanda kinataka kujengwa Mchinga, lakini anakizuia," alisema Mudhihir juzi.

Mudhihir, ambaye alikuwa akitumia mafumbo kwa kunukuu wanafalsafa mbalimbali, alitetea uamuzi wake wa kueleza bayana suala hilo alipotumia mfano wa mwendawazimu ambaye anatembea huku akizungumza kwa sauti na mtu mwingine ambaye anatembea akiwaza akilini masuala tofauti.

"Wote ni sawa, tofauti yake ni kwamba mmoja anazungumza kwa sauti na mwingine anazungumza kimyakimya," alisema mbunge huyo ambaye ni mwanafasihi.

Mudhihir pia alimnukuu mwanafalsafa ambaye alisema mtu ambaye hatumii akili yake, mambo humgeuka na akili huanza kumtumia yeye.

Wakati akitoa hoja na mifano yake, Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Bunge, Sera na Uratibu), Philip Marmo aliingilia kati na kutaka wachangiaji wawe wanataja majina ya mawaziri wanaowatuhumu badala ya kutoa tuhuma za jumla. Alidai kuwa tabia hiyo imeanza kukomaa tangu mbunge wa Nzega, Lucas Selelii alipolituhumu baraza zima la mawaziri na kuliombea laana.

Hata hivyo, Spika Samuel Sitta alimtetea akisema hawezi kumlazimisha kila mchangiaji amtaje waziri anayemtuhumu, na badala yake akashauri wachangiaji waeleze kuwa wataliwasilisha jina la waziri anayetuhumiwa kwa Waziri Mkuu Pinda.

Alipoulizwa na Mwananchi jana, Waziri Membe alisema, tayari pia alishapata simu nyingi kutoka Lindi na watu wengine ambao walimwambia kuwa ndiye alikuwa akitajwa na Mudhihir.

"Sikusikia hiyo hotuba, lakini nimepata simu nyingi kutoka Lindi zikinieleza kwamba, mimi ndiye nilikuwa nikitajwa," alikiri Membe.

Membe jana alisema baada ya kupata simu hizo kutoka Lindi, ameamua kujiandaa kulitolea suala hilo ufafanuzi katika vikao vya chama na serikali ngazi za wilaya na mkoa ili lieleweke vema na kuondoa hisia za uadui na chuki kwa watu ambao wanatoka katika mkoa mmoja na wanaoheshimiana.

"Nimeamua kulitolea ufafanuzi (halmashauri kuu ya CCM) NEC wilaya, kikao cha baraza la ushauri la mkoa. Haya ni mambo ya aibu hatuwezi kulipuana hadharani," alifafanua Membe.

Membe, ambaye ni mmoja wa wabunge wanaotokea mkoa wa Lindi, aliongeza kusema: "Nisingependa kufanya malumbano na ndugu yangu Mudhihir."

Alisema anamheshimu Mudhihir kwa muda mrefu na ni ndugu yake, hivyo ni vema jambo hilo akalizungumzia kwenye vikao hivyo ili kuondoa malumbano zaidi hadharani.

"Niko tayari kwenda Mchinga. Nitazungumza na wananchi wa kule ili waweze kuelewa vema suala hili," aliongeza.

Waziri huyo aliongeza kwamba yeye ni mtu wa maadili hivyo asingependa kukaa na kuzungumza mambo ya aibu hadharani bila kufuata maadili.

"Unajua katika kazi kuna mambo ya ethics (maadili), sasa sitaki kuanza kukaa na kuvunja maadili hayo, mimi ni mtu ambaye najiheshimu na nafanya kazi kwa misingi na miiko ya kazi," alifafanua.

Alipoulizwa iwapo anahisi matamshi ya Mudhihir yana msukumo wa maadui wake kisiasa ambao wanahisi anaweza kugombea urais 2015, Membe alisema kwa vyovyote itakuwa hivyo.

"Bila shaka ... bila shaka. Mudhihiri ninayemfahamu mimi asingeweza kutoa matamshi ya aina ile, lakini nasema sihitaji kulumbana naye namheshimu sana," alisisitiza Membe.

Membe aliongeza kwamba yeye si kampuni inayofanya mradi huo, hivyo hata akituhumiwa inakuwa ngumu kuelewa na hivyo kulimaliza suala hilo ataliripoti kwenye vikao husika.

"Kwa unyenyekevu mkubwa, nitalifafanua hili ili kuondoa haya malumbano ya aibu," alisema.

Alipoulizwa jana, Mudhihir, ambaye aliwahi kuwa naibu waziri kwenye Wizara ya Elimu na Utamaduni, alijibu: "Mtu niliyemtaja ni kondoo wa manyoya ambaye ni yeyote atakayezizima."

Alipokuwa akisisitiza hoja hiyo awali, Mudhihir aliapa kwamba waziri huyo ambaye anataka urais mwaka 2015, hata akiwa rais hakuna malighafi itakayochukuliwa kutoka Mchinga.

Tangu kuanza kwa bunge la bajeti, kumekuwa na makombora mbalimbali ya wabunge dhidi ya mawaziri na baraza zima la mawaziri.

Mbunge wa kwanza kuanza kulipua mawaziri alikuwa Selelii ambaye alililaani baraza hilo akisema limejaa watu wenye roho mbaya na wanaotaka kukwamisha baadhi ya wabunge majimboni kwao.
Wengine waliotoa shutuma nzito kwa mawaziri ni mbunge wa Maswa, John Shibuda, aliyehoji kipimo cha uzalendo cha baraza hilo, huku akilituhumu kuwa ndilo linalobariki mikataba ya kifisadi.
Tuma maoni kwa Mhariri
 
Kombora la Mbunge Mudhihir lamtikisa Waziri Membe
membe.jpg

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernad Membe, ametikiswa na kombora la Mbunge Mudhihir Mudhihir .

*Ajitetea anamheshimu, atajibu kwenye vyombo vya mkoa

Na Ramadhan Semtawa, MWANANCHI

MBUNGE wa Mchinga, Mudhihir Mudhihir hakutaja jina la waziri aliyemfananisha na "nyoka wa mdimu", lakini akasema kondoo wa manyoya atazizima mwenyewe na kujitokeza hadharani.

Jana Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernad Membe alijitokeza na kusema kuwa amepigiwa simu na watu wengine waliomwambia kuwa makombora hayo ya Mudhihir yanaelekezwa kwake na hivyo atachukua hatua kwa kulifikisha suala hilo kwenye vikao vya chama na serikali vya wilaya na mkoa.

Mudhihir, mmoja wa wabunge wenye kupenda kutumia misemo na methali huku akinukuu wanafalsa na vitabu mbalimbali, juzi alimlaumu mtu huyo kuwa ndiye anayetaka kiwanda cha saruji kijengwe kilomita 35 kutoka eneo lenye malighafi ambalo ni Mchinga.

Alisema mtu huyo, ambaye alimuelezea kuwa atawania urais katika uchaguzi wa mwaka 2015 anafanya hivyo kwa roho mbaya kwa kuwa hatanufaika lolote na msimamo wake kuhusu kujengwa kwa kiwanda hicho na kumfananisha na nyoka anayeishi kwenye mti wa ndimu ambaye hali majani yake wala ndimu, lakini mtu anayekwenda kuchuma ndimu kwenye mti huo humng'ata.

"Unajua nyoka wa mdimu ana hila sana; anapenda kukaa kwenye mdimu, lakini hali ndimu, ila akija mtu anayetaka kuchuma ndimu humshambulia, sasa yeye kiwanda kinataka kujengwa Mchinga, lakini anakizuia," alisema Mudhihir juzi.

Mudhihir, ambaye alikuwa akitumia mafumbo kwa kunukuu wanafalsafa mbalimbali, alitetea uamuzi wake wa kueleza bayana suala hilo alipotumia mfano wa mwendawazimu ambaye anatembea huku akizungumza kwa sauti na mtu mwingine ambaye anatembea akiwaza akilini masuala tofauti.

"Wote ni sawa, tofauti yake ni kwamba mmoja anazungumza kwa sauti na mwingine anazungumza kimyakimya," alisema mbunge huyo ambaye ni mwanafasihi.

Mudhihir pia alimnukuu mwanafalsafa ambaye alisema mtu ambaye hatumii akili yake, mambo humgeuka na akili huanza kumtumia yeye.

Wakati akitoa hoja na mifano yake, Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Bunge, Sera na Uratibu), Philip Marmo aliingilia kati na kutaka wachangiaji wawe wanataja majina ya mawaziri wanaowatuhumu badala ya kutoa tuhuma za jumla. Alidai kuwa tabia hiyo imeanza kukomaa tangu mbunge wa Nzega, Lucas Selelii alipolituhumu baraza zima la mawaziri na kuliombea laana.

Hata hivyo, Spika Samuel Sitta alimtetea akisema hawezi kumlazimisha kila mchangiaji amtaje waziri anayemtuhumu, na badala yake akashauri wachangiaji waeleze kuwa wataliwasilisha jina la waziri anayetuhumiwa kwa Waziri Mkuu Pinda.

Alipoulizwa na Mwananchi jana, Waziri Membe alisema, tayari pia alishapata simu nyingi kutoka Lindi na watu wengine ambao walimwambia kuwa ndiye alikuwa akitajwa na Mudhihir.

"Sikusikia hiyo hotuba, lakini nimepata simu nyingi kutoka Lindi zikinieleza kwamba, mimi ndiye nilikuwa nikitajwa," alikiri Membe.

Membe jana alisema baada ya kupata simu hizo kutoka Lindi, ameamua kujiandaa kulitolea suala hilo ufafanuzi katika vikao vya chama na serikali ngazi za wilaya na mkoa ili lieleweke vema na kuondoa hisia za uadui na chuki kwa watu ambao wanatoka katika mkoa mmoja na wanaoheshimiana.

"Nimeamua kulitolea ufafanuzi (halmashauri kuu ya CCM) NEC wilaya, kikao cha baraza la ushauri la mkoa. Haya ni mambo ya aibu hatuwezi kulipuana hadharani," alifafanua Membe.

Membe, ambaye ni mmoja wa wabunge wanaotokea mkoa wa Lindi, aliongeza kusema: "Nisingependa kufanya malumbano na ndugu yangu Mudhihir."

Alisema anamheshimu Mudhihir kwa muda mrefu na ni ndugu yake, hivyo ni vema jambo hilo akalizungumzia kwenye vikao hivyo ili kuondoa malumbano zaidi hadharani.

"Niko tayari kwenda Mchinga. Nitazungumza na wananchi wa kule ili waweze kuelewa vema suala hili," aliongeza.

Waziri huyo aliongeza kwamba yeye ni mtu wa maadili hivyo asingependa kukaa na kuzungumza mambo ya aibu hadharani bila kufuata maadili.

"Unajua katika kazi kuna mambo ya ethics (maadili), sasa sitaki kuanza kukaa na kuvunja maadili hayo, mimi ni mtu ambaye najiheshimu na nafanya kazi kwa misingi na miiko ya kazi," alifafanua.

Alipoulizwa iwapo anahisi matamshi ya Mudhihir yana msukumo wa maadui wake kisiasa ambao wanahisi anaweza kugombea urais 2015, Membe alisema kwa vyovyote itakuwa hivyo.

"Bila shaka ... bila shaka. Mudhihiri ninayemfahamu mimi asingeweza kutoa matamshi ya aina ile, lakini nasema sihitaji kulumbana naye namheshimu sana," alisisitiza Membe.

Membe aliongeza kwamba yeye si kampuni inayofanya mradi huo, hivyo hata akituhumiwa inakuwa ngumu kuelewa na hivyo kulimaliza suala hilo ataliripoti kwenye vikao husika.

"Kwa unyenyekevu mkubwa, nitalifafanua hili ili kuondoa haya malumbano ya aibu," alisema.

Alipoulizwa jana, Mudhihir, ambaye aliwahi kuwa naibu waziri kwenye Wizara ya Elimu na Utamaduni, alijibu: "Mtu niliyemtaja ni kondoo wa manyoya ambaye ni yeyote atakayezizima."

Alipokuwa akisisitiza hoja hiyo awali, Mudhihir aliapa kwamba waziri huyo ambaye anataka urais mwaka 2015, hata akiwa rais hakuna malighafi itakayochukuliwa kutoka Mchinga.

Tangu kuanza kwa bunge la bajeti, kumekuwa na makombora mbalimbali ya wabunge dhidi ya mawaziri na baraza zima la mawaziri.

Mbunge wa kwanza kuanza kulipua mawaziri alikuwa Selelii ambaye alililaani baraza hilo akisema limejaa watu wenye roho mbaya na wanaotaka kukwamisha baadhi ya wabunge majimboni kwao. Wengine waliotoa shutuma nzito kwa mawaziri ni mbunge wa Maswa, John Shibuda, aliyehoji kipimo cha uzalendo cha baraza hilo, huku akilituhumu kuwa ndilo linalobariki mikataba ya kifisadi.
 
................"Nimeamua kulitolea ufafanuzi (halmashauri kuu ya CCM) NEC wilaya, kikao cha baraza la ushauri la mkoa. Haya ni mambo ya aibu hatuwezi kulipuana hadharani," alifafanua Membe.

Membe, ambaye ni mmoja wa wabunge wanaotokea mkoa wa Lindi, aliongeza kusema: "Nisingependa kufanya malumbano na ndugu yangu Mudhihir."

....................................Waziri huyo aliongeza kwamba yeye ni mtu wa maadili hivyo asingependa kukaa na kuzungumza mambo ya aibu hadharani bila kufuata maadili.

"Unajua katika kazi kuna mambo ya ethics (maadili), sasa sitaki kuanza kukaa na kuvunja maadili hayo, mimi ni mtu ambaye najiheshimu na nafanya kazi kwa misingi na miiko ya kazi," alifafanua...........................

Mkuu Membe kama hayo ni maneno yako hapo juu.........kwa kigezo hicho hicho inabidi uwajibike
 
Si Membe wala Mudhihir watakaopita kuchaguliwa kugombea Urais mwaka 2015. Sasa kinachowawasha ni nini? Wanatoleana macho kisa waanza kuchafuana? Siasa za chini chini, vijembe, kashfa, majungu, zimebobea sana ndani ya hiki chama cha mafisadi! Mwaka huu tutayaona mengi. Waache wachafuane, wamwage siri zote hadharani, ili wananchi wawajue vema, mwaka 2010 wajue nani chuya nani mchele!
 
Si Membe wala Mudhihir watakaopita kuchaguliwa kugombea Urais mwaka 2015. Sasa kinachowawasha ni nini? Wanatoleana macho kisa waanza kuchafuana? Siasa za chini chini, vijembe, kashfa, majungu, zimebobea sana ndani ya hiki chama cha mafisadi! Mwaka huu tutayaona mengi. Waache wachafuane, wamwage siri zote hadharani, ili wananchi wawajue vema, mwaka 2010 wajue nani chuya nani mchele!

Mazee suala la Membe kukitamani kiti cha Magogoni Feri ni very obvious, suala ni je wanamtandao wana mtu mbadala? Hilo jambo la kuzingatia kwa sasa.
 
Hivi kale 'kautaratibu' ka zamiu ya wenzetu kutoka visiwani ndio kameishia kinamna? Si nafikiri 2015 Presida atatoka visiwani? Ama?
 
Jimbo la mchinga la Mh Mdhihir na mtama la Mh Membe yapo karibu sana, kuna kipindi cha nyuma niliwahi kumsikia Mh Mdhihir akilalamika kuwa Membe anamwingilia katika jimbo lake. Alidai kuwa Membe alikuwa akitoa misaada jimboni kwa Mdhihir na kuwaambia wananchi kuwa Mdhihir siyo mtu mzuri.

Suala la Membe kuwania urais mwaka 2015 ni wazi, kwani hamjui? Mbona alama za nyakati zinaonyesha tuu. Mfano mdogo ni kuteuliwa kwa aliyekuwa DC wa Lindi (Kwa Mh Membe) kuwa Katibu Mkuu wa UVCCM. Huyu ni kijana wa Membe na ni marafiki toka akiwa DC Lindi. Na sasa ndiye mtendaji mkuu wa UVCCM, na mjue kuwa UVCCM ina nguvu sana katika Chama Tawala.

Wacha waparurane, sisi yetu macho. Ila kazi ni nzito kwelikweli, kwani badala ya kufanya kazi watu wanafikiria 2015.
 
Hivi kale 'kautaratibu' ka zamiu ya wenzetu kutoka visiwani ndio kameishia kinamna? Si nafikiri 2015 Presida atatoka visiwani? Ama?
Zanzibar ni NCHI. Ina RAIS wake. Kutawaliwa na Rais kutoka "Nchi" nyingine itakuwa vigumu kidogo. Pia naunga mkono watu kujitokeza sasa kuonesha nia ya kugombea Urais 2015. Tuwajadili.
 
Mazee suala la Membe kukitamani kiti cha Magogoni Feri ni very obvious, suala ni je wanamtandao wana mtu mbadala? Hilo jambo la kuzingatia kwa sasa.
Yeah, ni kweli kuwa anakitaka sana kiti cha Magogoni. Na nadhani anatamani hata apewe nafasi hiyo sasa hivi. Ila ukweli unabaki kuwa, kadiri siku zinavyokwenda ndivyo anavyokipoteza kiti hicho.

Ifikapo 2015, itakuwa kutafuta laana ukitaka kuzungumzia mwanamtandao. Itakuwa balaa kisiasa na si ajabu hata kijamii kukumbushia serikali hii ya wanamtandao. Mtandao utapigwa vita kali kila kona ya nchi. Labda aonyeshe dhahiri kuwa yeye si mmoja wao.

Hivi kale 'kautaratibu' ka zamiu ya wenzetu kutoka visiwani ndio kameishia kinamna? Si nafikiri 2015 Presida atatoka visiwani? Ama?

Kale ka utaratibu hakatekelezeki tena Mkuu. Ni wazi kuwa chama chochote kinachotaka kuweka mgombea uRais na mgombea wake apate ushindi ni lazima kiweze kumnadi kwa wananchi. Kwahiyo si rahisi (hasa kwa muungano tulionao) kuchagua wagombea kwa kujali anatoka wapi. Unaweza kushindwa uchaguzi kwa kuzingatia utamaduni.
 
Wadau mbona inaonekana watanzania ni wagumu kubadilika? kutoka na Comments zote nilizozisoma kwenye hii thread inaonekana wazi kuwa bado wadanganyika tunahutaji kuongozwa na Serikali ya SISIEMU.

Kwani nini hatufikirii mabadiliko ndani ya nchi yetu? Serikali hii ya SISIEMU imekaa madarakani kwa muda mrefu sana bila ya faida wala maendeleo yoyote yale. Sasa hivi hatuhitaji kufikiria kuwa kuna utamaduni wa kupokezana Uraisi kati ya Tanzania Bara na Visiwani, tunachohitaji ni kutafuta namna ya kuichomoa SISIEMU madarakani. Kikubwa ni kuhakikisha Vyama Vya Upinzani vinapata idadi kubwa ya Majimbo na hii itasaidia kuidondosha SISIEMU.

Hii habari ya Membe na Mudhihir wala sio dili sana kwenye mustakabali wa maendeleo ya Taifa letu.
 
Jamani Membe duu...makombora yameshamuanziaa....mara ashutumiwe na alim support Mama Kahama ili aje amsaidie kugombea urais 2015 akagombana na JK wake...alipewa ujumbe kupitia Mama Salma(kaka na dada)....kazi ipo.....Joka la mdimu hahaha duu siasa mchezo mchafu....nyiue ndugu jamani siasa tu hizi msipitilizeee
 
Jamani vitu vingine ni common sense.
Katika utengenezaji wa cement 65-75% limestone ndo inatumika na viwanda vyote Tanga,Twiga na Mbeya Cement hayo malighafi yako ndani ya 2-3km from the plant kwa kuogopa hauling cost.Vingine kama gypsum ni 2-5% while other materials if necessesary ni 20-30% kama pozolana,flied ash
Na limestone ndo inadetermine kiwanda kijengwe wapi jamani not otherwise production cost zitashoot!
Tuache siasa huwezi locate kiwanda cha saruji mbali na limestone
 
Ni ajabu watu wanaotoka mkoa mmoja kuanza kutoleana mafumbo bungeni na hali wana vikao vingi vya chama wanaweza kukutana nakuongea. Ila Mudhir naye mh!
 
Jamani vitu vingine ni common sense.
Katika utengenezaji wa cement 65-75% limestone ndo inatumika na viwanda vyote Tanga,Twiga na Mbeya Cement hayo malighafi yako ndani ya 2-3km from the plant kwa kuogopa hauling cost.Vingine kama gypsum ni 2-5% while other materials if necessesary ni 20-30% kama pozolana,flied ash
Na limestone ndo inadetermine kiwanda kijengwe wapi jamani not otherwise production cost zitashoot!
Tuache siasa huwezi locate kiwanda cha saruji mbali na limestone

Sasa huko Mchinga sijui, kuna hizo limestone? Kama zipo basi sema tumkome Membe na kama hazipo basi tumshambulie huyu Mbunge.
 
umetoa data nzuri za kitaaluma lakini hujasema availability za hizo material huko bwana Muzihir....zipo? hazipo? je walikuwa wamepanga zitoke wapi? na kama kweli Membe alipinga..ni kwa sababu zipi? kupitia utaratibu gani? na nani alikuwa ni investor...

kuna taarifa za ujenzi wa kiwanda cha saruji kujengwa kisarawe..je vinauhusiano??? na barabara ishanza kuchongwa toka last month....
 
Nijuavyo mimi hawa wote wawili ni mashushushu wa miaka mingi sana. Membe aliingizwa kwenye ushushu kati ya 1969 - 70 wakati anasoma Seminari ya Namupa kule Lindi. Hii ilikuwa ni kutokana na u-sharp wake wa kiakili. Enzi za Mwalimu sifa kubwa ya kuingia kwenye ushushushu ilikuwa ni brain, tofauti na enzi hizi ambapo watu wanashikana mikono tu. No wonder hata watu ambao tunawafahamu kuwa sio ilntelligent wapo kwenye idara hii nyeti.
Kutokana na kuzidiana ujanja ndio maana mambo ya watu hawa wawili sasa yanajitokeza hadharani. Membe ni mjanja na Mdhihiry pia ni mjanja. Nahisi Mdhihiry asingependa Membe awanie urais, lakini sidhani kama yeye Mdhihiry ana lengo la kuwania urais. Yawezekana anatumiwa na watu wanaoangalia 2015 kumvurugia Membe au ni fitna tu.
 
Back
Top Bottom