Kutoka Bungeni: 2006 - 2010

Kutoka Bungeni: 2006 - 2010

Mkuu Mtu wa Pwani, wewe ni mzoefu sana hapa jamvini, watu tunakutegemea sana, tutatarajia kupata full info sasa hii ya Prof. Mwadosya mbona haina mshiko? kwanin i usimtaje Hawa Ghasia (Lindi) au Bernard Membe (Lindi) (hawa ni Mawaziri wanatoka eneo jirani na majirani wa Mdhihir). Au waziri wa viwanda, mazingira nk.?
 
jamani jana jioni nilipo rudi kibaruani kwangu na kujipumzisha sebuleni huku nikiangalia kipindi kutoka bungeni tbc1

mara nikamuona mzee mudhihir akichangia bajeti kwa maneno makali sana na akimtuhumu waziri hadharani na kumfananisha na joka la mdimu

anasema waziri huyo anakwamisha ujenzi wa kiwanda cha saruji jimboni kwake kisa ni yeye mudhihir maana akisikia waziri jina la mudhihir huwa kama aliekuwa na mimba anakuwa hajifai huhitaji ndimu na mbirimbi mbichi

kwa kweli vijembe na lugha za kuudhi zilikuwa nyingi hadi nikajiuliza kuna nn nyuma ya pazia tusichokijua

Mtu wa Pwani heshima mbele.
Kwanza mimi sikuwa na bahati ya kumsikiliza Mudhihir,pengine ningepata bahati ya kumsikiliza nisingekuwa na maswali.

Mkuu nashindwa kuelewa Dr/Pro Mwandosya anaingiaje katika sakata la ujenzi wa kiwanda cha saruji katika jimbo la mheshimiwa Mudhihir.Pengine ungesema waziri wa viwanda na biashara mama Mary Nagu ningekuelewa kidogo.

Mheshimiwa Mudhirir nadhani tayari kashaingiwa na kale kaugonjwa ka homa ya uchaguzi ndiyo maana anaongea pumba zake hana hoja ya msingi kwanza siku hizi wawekezaji ndiyo wanaamua wapi wanataka kuwekeza baada ya kuangalia sababu mbali mbali hasa za kiuchumi.
 
Hapo nahisi anamsema waziri na viwanda na biashara ambaye kama nipo sahihi ni Dr Mary Nagu.
 
jamani jana jioni nilipo rudi kibaruani kwangu na kujipumzisha sebuleni huku nikiangalia kipindi kutoka bungeni tbc1

mara nikamuona mzee mudhihir akichangia bajeti kwa maneno makali sana na akimtuhumu waziri hadharani na kumfananisha na joka la mdimu

anasema waziri huyo anakwamisha ujenzi wa kiwanda cha saruji jimboni kwake kisa ni yeye mudhihir maana akisikia waziri jina la mudhihir huwa kama aliekuwa na mimba anakuwa hajifai huhitaji ndimu na mbirimbi mbichi

kwa kweli vijembe na lugha za kuudhi zilikuwa nyingi hadi nikajiuliza kuna nn nyuma ya pazia tusichokijua

Mtu wa Pwani, Waziri wa Viwanda ni Dk. Mary Nagu, si Prof Mwandosya. Kwa hiyo Thread inatakiwa isomeka Kuna nini kati ya Mudhihir na Dk Nagu? Edit mkuu.
 
Another Episode kwenye Series sijui ni Season ya ngapi? Mungu tusaidie. Uwabariki hawa wawakilishi wetu na uwape roho ya kukuogopaWewe Mungu wa Bwana Wetu Yesu Kristo.
 
Sasa ni nani huyoo?mbona hatuambiwii mnatuacha puzzled....
 
Mkuu Mtu wa Pwani, wewe ni mzoefu sana hapa jamvini, watu tunakutegemea sana, tutatarajia kupata full info sasa hii ya Prof. Mwadosya mbona haina mshiko? kwanin i usimtaje Hawa Ghasia (Lindi) au Bernard Membe (Lindi) (hawa ni Mawaziri wanatoka eneo jirani na majirani wa Mdhihir). Au waziri wa viwanda, mazingira nk.?

Naomba nikusahihishe kidogo Hawa Abddulrahman Ghasia ni Mbunge wa Mtwara vijijini mkoa wa Mtwara na sio Lindi kama ulivyosema na Bernad Membe ni Mbunge wa Mtama mkoa wa Lindi.
 
Hii ngoma ni nzito kuliko mnavyotaka kuijadili

jiulizeni kwa nini Nyerer alingoa reli ya kwenda kusini?

na kwa nini ule mradi wa hydroelectric ulihamishwa?

Na kwa nini wale wajaani walipokuja waliambiwa wakalime mpunga huko juu

acheni hizo mnajidai waTanzania lakini historia ya nchi yenu hamuijui..mind you humu kuna wanafunz wa UD ambao wana access to all sorts of data kuhusus hili suala

Mudhiri hapa anarudia story tuuu
 
Mtu wa Pwani heshima mbele.
Kwanza mimi sikuwa na bahati ya kumsikiliza Mudhihir,pengine ningepata bahati ya kumsikiliza nisingekuwa na maswali.

Mkuu nashindwa kuelewa Dr/Pro Mwandosya anaingiaje katika sakata la ujenzi wa kiwanda cha saruji katika jimbo la mheshimiwa Mudhihir.Pengine ungesema waziri wa viwanda na biashara mama Mary Nagu ningekuelewa kidogo.

Mheshimiwa Mudhirir nadhani tayari kashaingiwa na kale kaugonjwa ka homa ya uchaguzi ndiyo maana anaongea pumba zake hana hoja ya msingi kwanza siku hizi wawekezaji ndiyo wanaamua wapi wanataka kuwekeza baada ya kuangalia sababu mbali mbali hasa za kiuchumi.
Na mimi nilimsikia Mudhihiri na kwa kweli hakutaja jina la waziri yeyote kiasi kwamba Marmo akaomba mwongoza wa Spika akimtaka mbunge huy ataje jina la waziri kuliko kutoa blanket statement inayoonyesha mawaziri wote ni wabaya. lakini spika alikataza kutajana majina
 
Mropokaji Mudhihiri in action again! Mchinga soundddddddddddddddd!.......
 
Uropokaji wa Mh Mudhihir uliwahi kumpa Unaibu Waziri enzi ya awamu ya tatu baada ya kumchambua vilivyo Mh Mrema. Mara hii nadhani ni masuala ya uchaguzi 2010.
 
Uropokaji wa Mh Mudhihir uliwahi kumpa Unaibu Waziri enzi ya awamu ya tatu baada ya kumchambua vilivyo Mh Mrema. Mara hii nadhani ni masuala ya uchaguzi 2010.


Mkuu Wildcard hata mimi nakumbuka sana hii,Mkapa wakati wake ukiweza kumshambulia vizuri mzee wa Kiraracha lazima akuzawadie cheo.Usisahau hata afande Mahita naye alizawadiwa ukuu wa jeshi la polisi IGP baada ya kumtangwa mabomu Bwana Mrema.

Mudhihir lazima aelewe wakati wa kuropoka umepitwa na wakati wananchi wanataka wawakilishi wabunifu,wanaoweza kujenga hoja na wanaoweza kuondoa kero zao.Inavyoelekea Bwana Mudhihir kagundua maji marefu na uchaguzi ndiyo umeshabisha hodi hana alilofanya.
 
Fahamuni kwamba tuhuma za Mudhihiri ni mwanzo tu
Kuna matatizomengi sana ya chinichini huyu mama waziri anayasababisha bilakujali.

Ninamhurumia JK kwani amejiaminisha kwa watu tusiowaamini.
Akibadilika atapendwa tena maana badokijitiacacho na nafasi japo ndogo ipo.
 
Hii ngoma ni nzito kuliko mnavyotaka kuijadili

jiulizeni kwa nini Nyerer alingoa reli ya kwenda kusini?

na kwa nini ule mradi wa hydroelectric ulihamishwa?

Na kwa nini wale wajaani walipokuja waliambiwa wakalime mpunga huko juu

acheni hizo mnajidai waTanzania lakini historia ya nchi yenu hamuijui..mind you humu kuna wanafunz wa UD ambao wana access to all sorts of data kuhusus hili suala

Mudhiri hapa anarudia story tuuu
Mradi upi wa Umeme? kwa ninavyo jua Stiggler Gorge kwa wakati ule ulikuwa mradi mkubwa saana kwetu na hizo Megawatts 3,000 tulikuwa hatuna mahali pa kuzitumia, lakini sasa ni wakati muuafaka. Reli iliondolewa au kungolewa kwa sababu ya kuanguka kwa zao la karanga kama sikosei etc, lakini pia ungeonyesha mwenyewe need ya kuwepo Reli huko kwa kuwepo production fulani ambayo wakati ule wa Mwl ulikwazwa kutokana na kutokuwepo kwa Reli infact Reli yenyewe ilikuwa inatoka Nachingwe kwenda bandarini Mtwara/Lindi kama sikosei.
Unajua wewe GT ni msomi , kwa hiyo muono wako unatakiwa kulenga huko kuliko kila kitu Mwalimu Mwalimu etc etc inakuwa kama una Personnal Vandetta nae, kwa mfano jana uliingiza mambo ya ufuska wa Slaa mahali pasipo pake, hivyo unapoteza maana zima ya suala unaloongelea hata kama uko sawa, tatizo ni mahali pa ku-advocate hilo suala, ni sawa unaulizwa hesabu ya kutoa wewe unajibu kwa kugawanya. (- unaifanya /)
Hata hapa tunaweza kuongelea mambo mengi ya kusini mfano huo wa Muhidhiri, lakini ni vizuri uka-stick to that point badala ya kuchanganya Pilau na Maharage na vyakula ambavyo haviendani pamoja. Mimi mwenyewe niko concern kwanini hatutumia nafasi tulizo nazo kujenga kusini kwa sasa huko nyuma na alot of theories ambazo zinaweza kuwa kweli au uongo, mfano vita ya Msumbiji mpaka 1975, uwezo wa nchi wakati ule, na vichocheo vingine vya investment, kama rasilimali watu, etc Usafiri wa watu etc. hata kaja Mkapa wa kwetu na ameshindwa kukamilisha vizuri hiyo barabara, kaamua kuka Ushoto.
 
Back
Top Bottom