Kutoka Bungeni: 2006 - 2010

Kutoka Bungeni: 2006 - 2010

nyeti. Nahisi Mdhihiry asingependa Membe awanie urais said:
Kama ni kweli basi atashangaza maana Watanzania walio wengi nikiwemo mie ninaona fahari Rais au hata Waziri Mkuu atoke mkoa wangu. Yeye aache chuki binafsi kama ni kweli, waungane waendeleze mkoa wao maana ni moja mikoa ambayo rasilimali zake ni sawa na wilaya moja Mwanga - Kilimanjaro. Wajitahidi kuundeleza mkoa wao
 
Huyu Mudhuhiri kama alivyotumika na mafisadi (Karamagi and group) kutoa hoja ya kumuondoa Zitto bungeni kwa sakata la Buzwagi, Ndiyo fitina hizo hizo anazitumia na kundi lake la mafisadi kumchafua Membe kisiasa. Hii hoja siyo ya kutetea wanachi wanyonge wa Mchinga bali ni muendelezo wa siasa chafu za makundi ndani ya CCM ili kumalizana kisiasa na kupoteza mweleokeo wa kweli wa kuwatetea wananchi ndani ya bunge
 
Nijuavyo mimi hawa wote wawili ni mashushushu wa miaka mingi sana. Membe aliingizwa kwenye ushushu kati ya 1969 - 70 wakati anasoma Seminari ya Namupa kule Lindi. Hii ilikuwa ni kutokana na u-sharp wake wa kiakili. Enzi za Mwalimu sifa kubwa ya kuingia kwenye ushushushu ilikuwa ni brain, tofauti na enzi hizi ambapo watu wanashikana mikono tu. No wonder hata watu ambao tunawafahamu kuwa sio ilntelligent wapo kwenye idara hii nyeti.
Kutokana na kuzidiana ujanja ndio maana mambo ya watu hawa wawili sasa yanajitokeza hadharani. Membe ni mjanja na Mdhihiry pia ni mjanja. Nahisi Mdhihiry asingependa Membe awanie urais, lakini sidhani kama yeye Mdhihiry ana lengo la kuwania urais. Yawezekana anatumiwa na watu wanaoangalia 2015 kumvurugia Membe au ni fitna tu.


In which case yeye ndoanakuwa joka la mdimu....
 
Nijuavyo mimi hawa wote wawili ni mashushushu wa miaka mingi sana. Membe aliingizwa kwenye ushushu kati ya 1969 - 70 wakati anasoma Seminari ya Namupa kule Lindi. Hii ilikuwa ni kutokana na u-sharp wake wa kiakili. Enzi za Mwalimu sifa kubwa ya kuingia kwenye ushushushu ilikuwa ni brain, tofauti na enzi hizi ambapo watu wanashikana mikono tu. No wonder hata watu ambao tunawafahamu kuwa sio ilntelligent wapo kwenye idara hii nyeti.
Kutokana na kuzidiana ujanja ndio maana mambo ya watu hawa wawili sasa yanajitokeza hadharani. Membe ni mjanja na Mdhihiry pia ni mjanja. Nahisi Mdhihiry asingependa Membe awanie urais, lakini sidhani kama yeye Mdhihiry ana lengo la kuwania urais. Yawezekana anatumiwa na watu wanaoangalia 2015 kumvurugia Membe au ni fitna tu.
Yote yanawezekana kwenye ulimwengu wa maspy.Mizengwe na propodanda mara nyingine ni sehemu ya kutimiza azma za yale wanayoyakusudia.Lakini kwangu cha msingi ni uwezo wa Mheshimiwa Membe kuwa raisi. Nionavyo watu wengi wengi wanahisi kama anautaka uraisi. Je matendo na uwezo wake unaweza kumsaidia kuufikia huo uraisi? Au ni suala tu la kuandika historia kwamba na yeye amewahi kuwa raisi na kufanya nalo ni suala dogo kama lile la kulipia hela za walipa kodi ufujaji kwenye bunge la Afrika?
 
wkuu kumradhi mie nilidhani prof mwandosya ila kwa mujibu wa habari kumbe ni kaka membe

cha kushangaza membe anasema yeye hana bifu nae sasa kulikoni au ndio mudhihiri keshafulia
 
Kama ni kweli basi atashangaza maana Watanzania walio wengi nikiwemo mie ninaona fahari Rais au hata Waziri Mkuu atoke mkoa wangu. Yeye aache chuki binafsi kama ni kweli, waungane waendeleze mkoa wao maana ni moja mikoa ambayo rasilimali zake ni sawa na wilaya moja Mwanga - Kilimanjaro. Wajitahidi kuundeleza mkoa wao

Mkuu, unaongea ukweli au unatania? Yaani hata kama ni "Punda" katoka mkoa wako kawa raisi utaona fahari!!!!!!! sasa kama anakuabisha kwa kufanya mambo ya kipuuzi kama ufisadi, kupora wake za watu n.k yaani wewe utaona fahari tu!!
Hutakiwi kuwaza hivyo bwana, raisi atoke popote pale cha muhimu tu ni kuwa Raisi bora siyo bora raisi kama unavyofikiri wewe...hatuendi hivyo!
 
Siyo homa ya uchaguzi,bali ya inatakiwa kufahamu ya kuwa kila mbunge yupo pale bungeni akitetea jimbo lake na si vinginevyo sawa wazee. na ukitaka kupata uchaguliwe tena hakikisha unatumia muda wa miaka mitano uliyochaguliwa kuleta maendeleo pale jimboni kwako ambapo ndipo panapopangwa bajeti nzima kama anavyofanya Mudhihiri
HEBU KAA DAKIKA MOJA TAFAKARI NA KAMA UNGEKUWA WEWE INGEKUWAJE? MSILOPOKE TU.
 
Hivi kale 'kautaratibu' ka zamiu ya wenzetu kutoka visiwani ndio kameishia kinamna? Si nafikiri 2015 Presida atatoka visiwani? Ama?

zamu??????
mimi huwa nadhani ile ishu ya zamu ilikuwa ni kwa ajili ya kumpata salim mwaka 1985 tu baada ya hapo zamu ilikuwa imeisha,wangekuwa wana nia kweli ya kuwa nazamu wangeingiza katika katiba ya chama angalau iwe na nguvu,lakini otherwise kumbuka majibu yaliyotolewa 2005 wajumbe wa zanzibar walipolalamika kuwa ni zamu yao,
 
..imethibitika kwamba Mbunge Mudhihir alikuwa amemlenga Waziri Membe.
 
mkuu taarabu imekushinda kutafsiri, joka la mdimu ni mh. Membe na alisema litajitokeza, na kweli limeshajitokeza lenyewe
 
tutaonana mengi kipindi hiki cha bunge na hasa maandalizi ya chaguzi zinazofuata.
 
“Aliwakumbusha wabunge kuwa wote walikula kiapo kwamba wataitumikia na kuilinda nchi ya Tanzania. Mwenye Biblia alishika Biblia, mwenye Quran alishika Quran na asiyeamini kwa sababu anaamini kuna kitu kipo juu yetu aliapa vilevile.

“Mheshimiwa Mwenyekiti hata katika kitabu kitakatifu cha Biblia; kwa sababu ya muda sitaweza kusoma, lakini kwa wale ambao hawana Biblia nitawatumia baadaye. Katika Kitabu cha Nabii Hosea: 4 1- 3 na Ezekieli 18: 24, maneno ya Mungu yanasema; ukila kiapo ukifuate na ukisema uongo utakufa..,” alisema Owenya.

Alifafanua kuwa sababu ya kusema hivyo kwamba ni kutokana na baadhi ya wabunge wanaochangia hoja na kulalamika sana huku wakiwanyooshea vidole mawaziri na serikali, lakini mwishowe wanaunga mkono hoja.

“Nawaombeni acheni unafiki, hata Mwenyezi Mungu haimpendezi,” alisema Owenya.
Kauli hiyo ya Owenya kuwataka wabunge waache unafiki ilimfanya Mbunge George Simba kusimama na kuomba mwongozo wa Spika akidai mchangiaji huyo alitumia lugha ya kuudhi na kumtaka afute kauli yake.

........MNAOJUA KISWAHILI CHA BUNGE, NI MANENO YAPI UKIYASEMA NI LUGHA YA KUUDHI? MANAKE KILA MBUNGE MBUNGE WA UPINZANI AKIPINGA JAMBO ANAAMBIWA ANATUMIA LUGHA HIYO!
 
Huyu Mudhuhiri kama alivyotumika na mafisadi (Karamagi and group) kutoa hoja ya kumuondoa Zitto bungeni kwa sakata la Buzwagi, Ndiyo fitina hizo hizo anazitumia na kundi lake la mafisadi kumchafua Membe kisiasa. Hii hoja siyo ya kutetea wanachi wanyonge wa Mchinga bali ni muendelezo wa siasa chafu za makundi ndani ya CCM ili kumalizana kisiasa na kupoteza mweleokeo wa kweli wa kuwatetea wananchi ndani ya bunge

kuna kitu kimoja naona kinaelekea kukua na kupata mashabiki japo inawezekana hakiko sahihi,nacho ni kwamba kila mtu anaetofautiana na upande flani[hasa wa wanaharakati]basi anaonekana anatumiwa na mafisadi,wakati inawezekana mtu katoa tu maoni yake.mheshimiwa mudhihiri inawezekana alitoa maoni yake kwa kadri ya uelewa wake kwa shughuli za bunge.
hoja ya kutaka kiwanda kibaki mchinga ni kwa maslahi ya wananchi na pia kwa maslahi ya mwekezaji pia,kiwanda kikibaki mchinga kwanza kitaongeza ajira kwa watu wa mchinga[kikiondoka ni kinyume chake], pia kiwanda kikibaki mchinga kinampunguzia gharama za uzalishaji mwekezaji,ila kwa fitna za huyo mheshimiwa aliyetajwa na mudhihiri anataka kiondoke kwenda labda karibu na jimbo lake[labda nae anataka kuongeza ajira kwake],kingine alichokataa mudhihiri ni kiwanda kiwe kwingine material itoke kwao,nani ***** huyo atakubali kuachiwa mashimo wakati kuna uwezekano wa kunufaika na hayo mashimo?????????????
 
Mwana wa Muntu,
Nimeuliza huko nyuma kama mnayo taarifa yoyote ya hiki kiwanda cha saruji lakini sijapata jibu hadi sasa hivi zaidi ya maneno matupu kuongozana..Ni sheria gani mnazitumia hapa maanake kama ni swala la uwekezaji, uchaguzi hauwezi kuwa wa Membe ila mwenye mali hatupo ktk Ujamaa jamani!.. nashindwa kuelewa Membe anahusika vipi na kutaka kiwanda kijengwe sehemu nyingine zaidi ya kutoa ushauri kwa muhusika (mwekezaji) kuwa sehemu nzuri kuwekeza ni wilaya yake na sababu ni kadha wa kadhaaa.

Jamani kila mtu anatafuta kuendeleza sehemu yake.. Upinzani kati ya wabunge kugombea Uwekezaji ni moja ya kazi za wabunge ktk mfumo wa kibepari. Mbunge ni mtongozaji mzuri wa wananchi huko Bungeni na pia anatakiwa kuwa kuhadi wa maendeleo ya wilaya yake kwa wawekezaji maadam anafuata taratibu zote za uwekezaji na sheria za kodi..
Kifupi, mbunge ni sawa na mume anayepeleka posa zake kwa mwanamke, akikuta wewe umetangulia haina maana aondowe posa yake.. Laa hasha atapigania ndoa hadi afanikiwe, hivyo matusi hayawezi kusaidia kitu kwani mwamuzi ni mwekezaji.

Huyu Mudhihir toka aseme hovyo na kusababisha Zitto kufungiwa Bungeni kisha akajigamba sana ktk magazeti nilimchoka siku hiyi hiyo..Na asivyokuwa na aibu aliwatetea sana Lowassa na Karamagi, leo hii anakuja na hizi habari akitafuta umaarufu mwingine..
Hatujasahau na wala hatuwezi kumsikiliza Machingai ambaye hata ukimfumba mdomo wake bado atazungumza kwa nyero!..inaonyesha wazi ana kile kitu kinaitwa Kisokorokwinyo!
 
sual la Mudhihir si suala dogo kwa mtu anayemfahamu kwani kwa miaka mingi amekuwa ni mtu apendaye ugomvi na mwenye mambo ya kiswahili sana. Msikilize Lugha anayotumia, Mudhihir alitakiwa awe mwalimu wa kufundisha watu kutunga misitari ya nyimbo za mipasho na wala si mbunge. kuna mtu anajua historia ya Mudhihir? alitokea kuwa mwalimu wa shule za msingi, tena maarufu sana kwa kufundisha nyimbo za kwaya na wala hana elimu ya juu. na ndio maana amekuwa mtu wa vicheksho bungeni na mtu wa mipasho tu hana la maana la kuwapa wananchi
 
Kwa kweli mudhuhir kisiasa ameisha tena sana tu, enzi zake zimepita na haziwezi kurudi tena na huu ugonjwa wa kupoteza jimbo sasa umemwingia anataka kutafuta mchawi, namshauri arudi akafundishe kwaya shule za msingi, elimu yake ndogo haiwezi kutusaidia kujenga Tanzania Imara na ya matarajio kwa vizazi vya sasa na vijavyo.
Kwa elimu ndogo aliyonayo Mudhihir anadhani wawekezaji huwekeza kwa kuangalia maligafi inapopatikana tu? hicho ni kigezo mkimoja lakini vipo vigezo vingi zaidi ya hicho ila kwa kuwa uwezo na uelewa wa kuchambua mambo wa Mudhihir ni mdogo sana kama elimu yake ilivyo ndogo ndo maana hajui sababu za kwa nini ujenzi ufanyike kilometa 35 toka mali ghafi inapopatikana. yeye anaona kilometa 35 ni mbali sana? tunakuomba acha usanii wa taarabu toa hoja na sio hoja za kuogopa kupoteza jimbo
 
Jamani vitu vingine ni common sense.
Katika utengenezaji wa cement 65-75% limestone ndo inatumika na viwanda vyote Tanga,Twiga na Mbeya Cement hayo malighafi yako ndani ya 2-3km from the plant kwa kuogopa hauling cost.Vingine kama gypsum ni 2-5% while other materials if necessesary ni 20-30% kama pozolana,flied ash
Na limestone ndo inadetermine kiwanda kijengwe wapi jamani not otherwise production cost zitashoot!
Tuache siasa huwezi locate kiwanda cha saruji mbali na limestone

kwa jinsi watu wanavyopenda ushabiki humu dont expect kama utapata watu wa kujadiliana based on hoja yako ya msingi

welcome to JF ya 2009
 
Huyu Mudhuhiri naamini anatumiwa sana na mafisadi kwa kuwa elimu yake ni ndogo sana ila ni fundi wa lugha ya taarabu na mafumbo, kwa wenye akili watamkumbuka alivyotumika na mafisadi (Karamagi and group) katika kujenga hoja tena kabla hata ya wakati ya kumuangamiza Zitto bungeni kwa sakata la Buzwagi, Na kwa kuwa mafisadi wanajua Membe ni mwadilifu wanaogopa akiupata urais 2015 atawashughulikia mafisadi wote sasa wanamtumia ila kumchafua Membe kisiasa. Hii hoja siyo ya kutetea wanachi wanyonge wa Mchinga bali ni muendelezo wa siasa chafu za makundi ndani ya CCM ili kumalizana kisiasa na kupoteza mweleokeo wa kweli wa kuwatetea wananchi ndani ya bunge. Namshauri Mudhihir awe mwanamapinduzi na mzalendo kwa wananchi wake sio tu wa mchinga bali watanzania wote, aache unafiki na kutumia lugha za mashaitri na mafumbo kubomoa watu. hilo linaonyesha udhaifu na uishiwa wa fikra na uwezo mdogo wa kupambanua mambo alionao mudhihir, mafisadi wanamtumia kama kasuku tu anakariri wana falsa bila hata kujua maudhui ya yale wanayomaanisha wana falsafa. Kwa kuwa anajijua kuwa ana elimu ndogo anataka kujitutumua mbele ya watanzania wamdhani kuwa na yeye kasoma kwa kunukuu wanafalsafa tena kwa lugha ya kiingereza ambayo yeye mwenyewe haijui hata kuiongea
 
Na Leon Bahati, Dodoma
MBUNGE wa Mchinga, Mudhihir Mudhihir (CCM) amesema hatishiki na uamuzi wa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe kuwa atamshtaki vikao vya CCM vya wilaya na mkoa baada ya kumtuhumu kuwa anakwamisha maendeleo kwenye jimbo lake.

Mudhihir, akiongea kwa mafumbo na kunukuu wanafalsafa mbalimbali, alimfananisha waziri huyo na nyoka anayeishi kwenye mti wa mdimu na kuuma watu wanaotaka kuchuma ndimu wakati hali matunda hayo.

Alikuwa akimaanisha kuwa Membe anatumia wadhifa wake kutaka kiwanda cha saruji kisijengwe kwenye jimbo la Mchinga wakati uamuzi huo hatanufaika nao.

Pamoja na Mudhihir kutomtaja Membe, waziri huyo alijitokeza na kusema kuwa ameshapigiwa simu na watu wengi waliomuhusisha na mafumbo hayo na hivyo akaahidi kulifikisha suala hilo kwenye vikao vya CCM vya wilaya na mkoa.

Juzi akizungumza na Mwananchi, Mudhihir alielezea kushangazwa na kauli ya Membe kujihisi kuwa ndiye aliyemzungumzia katika mafumbo yake, lakini akasema haogopi kushtakiwa kwa sababu anajiamini kuwa ana uzoefu katika mambo ya kisiasa na bunge kwa miaka 14.

"Kwa miaka 14 nimekuwa bungeni, sijawahi kumtaja mtu kwa kumsingizia," alisema Mudhidir huku akisisitiza kuwa hawezi kujibu hoja za kusadikika, akiimanisha tuhuma zilizotolewa na Membe juzi.

Alisema kuwa atamchukulia hatua kwa kufikisha suala hilo kwenye vikao vya CCM ili wamuadhibu.

Katika madai yake aliyotoa Jumatatu wiki hii wakati akichangia hotuba ya makadirio ya matumizi ya ofisi ya Waziri Mkuu, Mudhihir alidai kuwa mtu huyo anataka kiwanda kijengwe kilomita 35 kutoka eneo ambalo malighafi zinapatikana, ambako ni Mchinga.

Alisema karibu viwanda vyote vya saruji nchini vimejengwa kwenye maeneo ambayo yana malighafi, akitoa mfano wa kiwanda cha Twiga Cement kilicho Dar es salaam, na vingine vilivyo mkoani Tanga na Mbeya.

Alidiriki kusema endapo nia hiyo ya kujenga kiwanda mbali na eneo lenye malighafi itatekelezwa, wananchi wa Mchinga hawatakubali malighafi hiyo ichukuliwe hata kama mtu huyo atakuwa rais na kusema "watampiga mawe".
 
Back
Top Bottom