Kutendwa kumenifanya nisijielewe

Kutendwa kumenifanya nisijielewe

Pole sana nakushauri usirudiane nae kwani hujui kilichomtoa huko mpaka atake kurudiana na wewe tena..pili jitahidi kuikubali hali iliyokupata na uisahau kwani wanaume wote siyo wasaliti..muombe mungu sana hakika atakusaidia na kukuonyesha njia iliyo sahihi..!
 
Wapendwa katika Bwana wana MMU: Nitumie nafasi hii kutoa shukrani zangu za dhati kabisa kwa wote mlionishauri katika jambo hili hadharan na hata pm. Mungu azidi kuwapa hekima na maisha marefu yenye kila aina ya furaha.

Kwasasa naishi kwa amani kabisa bila hata huyo jamaa na hata ile hasira niliyokua nayo mwanzo haipo tena. MMU imenifanya nijione niko strong kupitia ushauri wenu. Na ningependa hata wale wanaopitia maumivu ya kimapenzi kwasasa wapige moyo konde waone kwamba kuna maisha mengine mbele ya hao ma x zao. Tujifunze kukubali matokea na kusonga mbele,maisha yako yanakutegemea wewe mwenyewe uyajenge wala usisubiri mwingine akujengee.


I strongly agree with you Valentina.

Big up.
 
nimependa ushauri wako mkuu.

BTW wengi tunaumizwa kwa kutosimama imara, Mungu hakutuumba ili tuje tulie bali kumtukuza kwa kila sekunde anayotupa nafasi kuishi hapa duniani. Binafsi nimetokea kumchukia huyo rafiki yake wa karibu maana yeye haswa ndo chanzo cha maumivu ya Valentina.

Nikushauri piga moyo konde na chonde chonde usimrudie tena maana huwez jua Mungu alikuwa anakuepusha nini. cha msingi piga goti kwa Mungu na umsihi akupe mwanaume wako wa maisha na pili huna sababu ya kuyafikiria uliyotendewa ukiwa na new rltn.
Kuna msemo waswahili husema wanaume wote ni sawa wamezaliwa na mama mmoja mimi nakataa kabisa, wanaume wanatofautina na kamwe usiweke akilin mwako kuwa utatendwa kila siku. Kumbuka Mungu anakupenda sana na hawezi kamwe kukubali upitie tena magumu uliyopitia kama unamtegemea.

Tena wakati mwingine Mungu huruhusu mapito ili uwe imara zaidi.

nikutakie maisha mema na Mungu awe nawe katika relation ambayo unayo au unayotegemea kuinza.
Amen Amen sweetheart

Ila huna haja ya kumchukia huyo rafiki ake Vale wala huyo ex. Wote walitumika tu kumpa Vale somo fulani. So unashukuru tu kuwa part yao katika maisha yako is over. Tunaganga yajayo
 
Nilitendwa mwisho nimeachana nao mia kwa mia. Nawaogopa. Heri nisifanye niiponye roho yangu.
 
Ukiendekeza hizo hali utakuja kurevenge kwa wrong person,utajialumu sana,kwasababu upo bitter utataka jinsi ya kupona hutathamini mahusiano matokeo yake siku atakuja mtu wa kweli utafanya fujo then utagundua alikua perfect match for you,aisee hutakaa ujisamehe....pia mdogo wangu never stop to love,upendo ni kwaajili ya moyo na afya ya uso wako sio kwaajili ya mtu mwingine jifunze hilo.
Pia usiwaze kama utapata malaika kwasababu hata wewe sio malaika jifunze tu kuelewa kinacjoendelea nakusamehe na kusonga mbele,
Kuhusu kumrudia huyo bwana isipoteze muda katika hali ya kawaida alikua na sababu gani ya kufanya hivyo?kama ni shetani basi ujue atampitia tena utalia zaidi.
 
Kasafishe nyota,huyo rafiki yako hakua mtu mzuri,
 
Me kwanza nakupongeza Kwa moyo wa kuwa mpole, na kuwaruhusu waendelee na ka mchezo. kudadadekii...!!!!! me ningedeadisha mtu hapo. yani nikufumanie then nikuache bili ngeo hapana!!!!

Pili. Usithubutu kurudiana na huyo malaya atakuja kukuua. yatakuja kukupata makubwa zaidi ya hayo yalokupata.

Tatu. Sasa acha uoga ondoa hofu soon kuna penzi moja la ukweli linakuja mbele yako. ondoa ile dhana kuwa eti wanaume wote ni sawa. hapana ni tofauti sana. so plz just patient
 
Unajua nn nimejifunza kitu fulani juu ya uhusiano uliokufa then end of ze day men kukurudia hurudi kwa kisasi kati ya mahusiano 10 yaliyokufa basi mahusiano saba huishia maafa ( nikimaanisha utackia kamrudia bwana wake wa zamani wameenda guest au hotel wamekuta maiti ya mwanamke kachinjwa) I don't know why itatokeaga hv, km mimi naogopa kurudianaga hata km nilimpendaga vp, ila kwa upande fulan huwamuz ni wako usiogope
 
Wapendwa ni matumaini yangu mpo wazima na mko vizuri katika majukumu yenu

Leo ninaomba kushare nanyi jambo ambalo limekua likinitatiza kwa muda sasa. Ninatambua kila mmoja wetu ana historia yake ya kimapenzi na wengi tumetendwa na wale ambao tuliwekeza mioyo yetu kwao kwa kuwaamini kwamba wataiendeleza furaha yetu, ila kwasababu mbalimbali au kwa bahati mbaya wengi hatukuweza kufikia matarajio yetu juu ya hao wenzetu.

Binafsi nilikua katika mahusiano na mtu ambae nilimpenda mno narudia tena nilimpenda tena mno. Na ndie mwanaume wangu wa kwanza kukutana nae kimwili.

Naye kwa upande wake alionyesha uaminifu na moyo wakujali,maneno yote mazuri yenye matumaini mtoto wa kike niliambiwa, kifupi tulipanga uhusiano wetu uzae ndoa.

Ilifika hatua mwezi wa sita mwaka jana akaja Arusha kwalengo la kujitambulisha nyumbani kwetu. Lakini ghafla katika hali ambayo sikuitarajia akabadilisha maamuzi yake akanipa visingizio.

Baada ya muda mfupi kabla ya yeye kurejea kwenye makazi yake, nikamfumania akiwa na rafiki yangu wa karibu, rafiki niliye mchukulia kama ndugu yangu na kushare nae baadhi ya mambo.

Waliosalitiwa bila shaka wanaelewa uzito wa maumivu hayo. Ikabidi niwe mpole,na kuwaambia waendelee mbele,siku zilivosonga yule binti akaanza mambo ya dharau kwangu ila namshkuru Mungu nilipata moyo wa kumsamehe na kupuuza dharau zake.

Ilipofika mwezi wa 9 yule binti aliacha kazi kwa shari na kurudi kwao.

Sasa kilichonifanya nije hapa mbele yenu leo, nikwamba yule mwanaume anataka kurudi kwangu na mimi moyo wangu unakua mzito kumrudia, nimetokea kumchukia.

Jambo linalonisumbua zaidi kila ninapoanza mahusiano mapya hua nashindwa kuendelea mbele, hofu ya kwamba huyu atanifanyia kama yule inanijia mara kwa mara na matokeo yake nakua sababu ya kuvunjika uhusiano huo.

Wapendwa nifanye nini kukabiliana na hali hii ya pili? Ninatamani sana hali hii iniondoke. Karibu kwa mchango wako kimawazo.
Kwenye makosa ya kiuandishi mnisamehe maana natumia simu.

Japo ni ya zamani ila nitashauri kesho...nikumbushe!
 
miaka 20 hadi 30 . hiki nikipindi kigumu sana kwa binadamu. maboy magirl kila mtu analia na lake.wallahi ujana maji ya moto. mfano hai hata mie nilikuwa na mpenzi kiukweli nilimkubali nilimuherewa lakini kuduu namie hataki au kuja maskani mpaka umlazimishe. pesa zangu anataka sasa nimemwambia nipe mzigo utaki tembea mpaka leo ajanijibu hivyo kama akishoboka tena namkazia. mwingine naye hataki kuja maskani ukitaka kuduu naye anasema yuko kwenye siku zake. mwingine anasema mpaka nikamtambulishe kwanza. sasa wote nimewapotezea wakishoboka nawakazia kama kawaida. sst kwa ushauri wangu usichukie wewe mrudie mungu atakupa akupendaye hila kama una mdomo unaongea sana punguza na virungu punguza kama huko hivyo! nawasilisha
 
pole sana best yaani jitie nguvu usimruhusu huyo mtu kurudiana naye kwani hujui huko alitoka ilikuwaje mpaka akuombe urudiane naye
cha kufanya wewe ishi maisha mapya na ondoa moyoni hayo mawazo ya kutendwa jivike ujasiri na angalia maisha yako ya sasa

usijiingize tena kwenye mahusiano mpaka moyo wako upone na uone sasa unaweza kuwa na chungu kipya

usikaatae watu wapya wanapokujia wachunguze na jiangalie moyo wako umeridhika kwao anza upya sasa na ikiwezekana mwambie mtu
mpya kuwa hutaki msihara kwenye mahusiano na muweke wazi kuwa wewe si kokoto bali ni jembe jipya
 
Me kwanza nakupongeza Kwa moyo wa kuwa mpole, na kuwaruhusu waendelee na ka mchezo. kudadadekii...!!!!! me ningedeadisha mtu hapo. yani nikufumanie then nikuache bili ngeo hapana!!!!

Pili. Usithubutu kurudiana na huyo malaya atakuja kukuua. yatakuja kukupata makubwa zaidi ya hayo yalokupata.

Tatu. Sasa acha uoga ondoa hofu soon kuna penzi moja la ukweli linakuja mbele yako. ondoa ile dhana kuwa eti wanaume wote ni sawa. hapana ni tofauti sana. so plz just patient
ndio maana nakupenda dotto
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom