Equation x
JF-Expert Member
- Sep 3, 2017
- 39,883
- 61,613
Kuna mpenzi wangu mmoja nilimpenda sana, kuliko yeye alivyonipenda mimi.
Upendo ukawa unaongezeka zaidi, pale ninapokuwa nampa vijisenti.
Baada ya kuona anatumia visalio vyangu vingi, nami nikawa namkomoa kwenye shoo, nikawa nampa shoo kali.
Iliyopelekea, akawa ananikwepa kwepa pale ninapokuwa namuhitaji.
Baada ya muda akawa amebeba ujauzito, ingawa simuamini sana kama yule mtoto ni wa kwangu, ingawa yeye anasema ni wa kwangu.
Mahusiano yetu yakawa ni ya migogoro hasa pale ninaposhindwa kumtumia visalio. Na nilikuwa nafanya makusudi ili niweze kupima upendo wa kweli.
Baada ya muda kupita, kila mmoja akaendelea na maisha yake; ingawa mara moja moja tulikuwa tunawasiliana pale ambapo hasira zinakuwa zimeisha.
Hivi karibuni, alipata ajali iliyopelekea kuvunjika mguu, na kusababisha tembea yake kuwa ya kuchechemea.
Tangu ajali itokee mpaka leo hii, imepita kama miezi sita hivi; sasa leo amenipigia simu na kulalamika watu aliokuwa akiwaamini wamemtelekeza na wamepunguza ukaribu naye.
Kwa hiyo anaomba tusameheane kwa yale yote yaliyotokea, na maisha yasonge mbele; Pia nijiandae mwakani mtoto aweze kwenda shule.
Hapa nilipo natafakari, baadaya kuona anachechemea na watu kutokuwa karibu naye, ndio ameona umuhimu wangu?
Wakuu, ebu nishaurini.
Upendo ukawa unaongezeka zaidi, pale ninapokuwa nampa vijisenti.
Baada ya kuona anatumia visalio vyangu vingi, nami nikawa namkomoa kwenye shoo, nikawa nampa shoo kali.
Iliyopelekea, akawa ananikwepa kwepa pale ninapokuwa namuhitaji.
Baada ya muda akawa amebeba ujauzito, ingawa simuamini sana kama yule mtoto ni wa kwangu, ingawa yeye anasema ni wa kwangu.
Mahusiano yetu yakawa ni ya migogoro hasa pale ninaposhindwa kumtumia visalio. Na nilikuwa nafanya makusudi ili niweze kupima upendo wa kweli.
Baada ya muda kupita, kila mmoja akaendelea na maisha yake; ingawa mara moja moja tulikuwa tunawasiliana pale ambapo hasira zinakuwa zimeisha.
Hivi karibuni, alipata ajali iliyopelekea kuvunjika mguu, na kusababisha tembea yake kuwa ya kuchechemea.
Tangu ajali itokee mpaka leo hii, imepita kama miezi sita hivi; sasa leo amenipigia simu na kulalamika watu aliokuwa akiwaamini wamemtelekeza na wamepunguza ukaribu naye.
Kwa hiyo anaomba tusameheane kwa yale yote yaliyotokea, na maisha yasonge mbele; Pia nijiandae mwakani mtoto aweze kwenda shule.
Hapa nilipo natafakari, baadaya kuona anachechemea na watu kutokuwa karibu naye, ndio ameona umuhimu wangu?
Wakuu, ebu nishaurini.