Kiranga
Platinum Member
- Jan 29, 2009
- 87,473
- 151,579
Nimekuuliza kusudi la nani, hujajibu.Ahsante kwa mtazamo wako.
Ila Kusema Mandela alichagua/kuyapa mwenyewe kupambana na ubaguzi hakuonyeshi kwamba hakukuwa na kusudi la awali. Mtu anaweza kufanya uchaguzi wake na bado uchaguzi huo ukawa sehemu ya kusudi la awali. Una ushahidi gani kwamba hakukuwa na kusudi la awali?
Mfano mtu anaamua mwenyewe kusomea udaktari. Lakini mtu mwingine anaweza kusema vipaji, mazingira na nafasi alizopewa vilimwelekeza kwenye kusudi hilo. Ukweli kwamba kuchagua hauondoi uwezekano wa kusudi,
Wangapi wanachagua au wqnayapa maisha malengo na hayafikiki.
Kila mtoto.alitamani KUWA kama flani, kusomea kitu flani hayo ni malengo lakini vipi wote walifanikiwa?
Ukisema kusudi/lengo la wali hili ni lazima litafanyika bilabchangamoto kubwa ukilijganisha na lile la kujipa
Dhana ya maisha kuwa na kusudi ni ya kidini zaidi. Inatokana na dhana ya maisha kuumbwa na Mungu na Mungu kuwa na kusudi ya kuumba maisha.
Ukimuondoa Mungu, dhana ya maisha kuwa na kusudi maalum inaondoka.
Kusudi la nani?
Processes za nature zinaendelea bila kusudi. Kwa sababu, kuwa na kusudi ni lazima kudhamiria, nature haifikiri, haina dhamira, inaenda tu kwa conbenience. Inafuata tu the path of least resistance.
Maji yanashuka ktoni kutoka mlimani kuja moaka baharini si kwa sababu yanakusudia kufanya hivyo, yqnafuata the oath of keast resiatance kwa kufuata gravity tu.
Sayari zinazunguka nyota hivyo hivyo, si kwa sababu zina dhamira fulani, zinafuata path of least resistance kufuata gravity tu.
Maji yanaposhuka mtoni kutoka mlimani kwenda chini baharini, hayana kusudi la kuishia baharini. Yanaishia baharini kwa sababu baharini kuko chini.
Sasa hapo ukianza kuuliza kusudi ka maji kushuka kutoka mlimani kwenda baharini utakuwa umeuliza swali vibaya. Kwa sababu maji hayana kusudi.
Maji hayo kushuka ni sawa na maisha. A natural process. Natural processes hazina kusudi.
Swali la kusudi la maisha ni nini, ni sawa na swali la kusudi la maji kushuka kutoka mlimani kwenda baharini ni nini.
Maji hayana kusudi. Maisha hayana kusudi.
Evolution inatokea bila kusudi.
Ukiondoa kusudi ambalo mtu anayapa maisha yake mwenyewe, dhana nzima ya maisha kuwa na kusudi maalum ni ya kidini, inaendana na dhana ya uwepo wa Mungu ambaye hayupo, na haina maana.
Swali zima la kusudi la maiaha ni anthropic bias, ni sisi watu, ambao tunafanya mambo kwa makusudi fulani, kuviwekea vitu vingine tabia hiyo ya kufanya mambo kwa kusudi, kuwekea maisha kusudi, wakati maisha yenyewe hayana kusudi, wewe ndiye unayapa maisha yako kusudi.
Kuuliza swali hiki ni sawa na kiziwi ambaye hajui sauti, anajua rangi tu kqa sababu anaona, anapoukiza "rangi ya wimbo wa taifa ni rangi gani?".
Yeye kiziwi anachojua ni rangi, haelewi kuwa wimbo wa taifa ni wa sauti, hauna rangi.