Kusaini kwenye vitabu getini

Kusaini kwenye vitabu getini

Duh, ni hilo kumbe

Mkuu lile daftari usilidharau kabisa, huwezi jua siku ya kukusaidia.

Kuna mkasa umetajwa hapa jukwaani kwamba kuna mahali tukio lilifanyika na mtu akapewa kesi, kilichomwokoa ni kwamba alijitetea kuwa muda huwa alikuwa mahala fulani na daftari kuletwa ikaonekana kweli alisign kuingia na kutoka mida inayotajwa.
 
Huu utaratibu hauna hata maana mkuu! Maana siyo kweli kwamba taarifa zote ni sahihi kuhusiana na hao wageni.

Labda wanataka tu kujua traficking ya watu katika hizo ofc
Ni shida kweli kweli
 
Mkuu lile daftari usilidharau kabisa, huwezi jua siku ya kukusaidia.

Kuna mkasa umetajwa hapa jukwaani kwamba kuna mahali tukio lilifanyika na mtu akapewa kesi, kilichomwokoa ni kwamba alijitetea kuwa muda huwa alikuwa mahala fulani na daftari kuletwa ikaonekana kweli alisign kuingia na kutoka mida inayotajwa.
I meant, sijadharau hilo zoezi mkuu! Ila argument yako sidhani kama kama ipo positively sana.


Yaani kwamba LENGO ni liwe kwamba kutambua mtu na hao watu wajulikanale??

Anyway inaweza kusaidia. Je hakuna jambo lingine zaidi ya hilo?
 
I meant, sijadharau hilo zoezi mkuu! Ila argument yako sidhani kama kama ipo positively sana.


Yaani kwamba LENGO ni liwe kwamba kutambua mtu na hao watu wajulikanale??

Anyway inaweza kusaidia. Je hakuna jambo lingine zaidi ya hilo?

Mkuu humu tuko wadau mbalimbali, kila mtu anakuwa anaweka point kadhaa anazojua ni muhimu.

Labda niongezee na hii moja.

Kukitokea upotevu wa kitu, tunaanza kuangalia nani na nani walikuwa around muda ule, ingawa mtu mwenye lengo la kuiba/dokoa sidhani kama ataweka majina halisi.
 
Mkuu humu tuko wadau mbalimbali, kila mtu anakuwa anaweka point kadhaa anazojua ni muhimu.

Labda niongezee na hii moja.

Kukitokea upotevu wa kitu, tunaanza kuangalia nani na nani walikuwa around muda ule, ingawa mtu mwenye lengo la kuiba/dokoa sidhani kama ataweka majina halisi.
Nakubaliana na wewe mkuu, sorry kwa attack, nimeshindwa kupangilia maelezo yangu nakiri hivyo.

Sorry once again boss
 
Nakubaliana na wewe mkuu, sorry kwa attack, nimeshindwa kupangilia maelezo yangu nakiri hivyo.

Sorry once again boss

Personally sijaona kama umefanya attack, ila ni njia tu ya kuulizana na kujulishana, maana mimi pia niliwahi kuuliza maana ya hilo daftari siku moja nikaelezwa baadhi na nikaona ni za msingi.

Kwa mfano makampuni mengine unapoingia unaacha kitambulisho chako wanakupa chao, so hapo ni lazima credentials ziwe za kweli, ukitoka ndo unapewa kitambulisho chako.

Just cool mkuu, but thanks.
 
Kwani huyo kibaka na mhuni anashindwa kusaini kwenye hiyo kaunta buku na kwenda kufanya yake?! ndio maana nikasema hivi huo utaratibu hauna tija. Hizi halmashauri nilizozitaja wajitahidi wanunue kale "kadude ka kupapasa mtu" akiingia pale getini
Kuna wengine wanaficha visu kwenye nyeti. Upo tayari kupapaswa huko?
 
Ata kama kiusalama hivi vitabu havina msaada ila ni vizuri mkuu... Kuna kipindi nilisikia mkaka alisingiziwa kesi moja kubwa sana na wakati yupo mahakamani akakumbuka kua siku ya tukio alikua ofisi fulani hivi na aliandikisha jina... Yaani hicho kitabu ndo kilitumika kama ushahidi kua hakuwepo kwenye tukio la uhalifu.

Viendelee tu kuwepo na njia nyingine mbadala za kuimarisha ulinzi ziongezwe.
 
Ata kama kiusalama hivi vitabu havina msaada ila ni vizuri mkuu... Kuna kipindi nilisikia mkaka alisingiziwa kesi moja kubwa sana na wakati yupo mahakamani akakumbuka kua siku ya tukio alikua ofisi fulani hivi na aliandikisha jina... Yaani hicho kitabu ndo kilitumika kama ushahidi kua hakuwepo kwenye tukio la uhalifu.

Viendelee tu kuwepo na njia nyingine mbadala za kuimarisha ulinzi ziongezwe.
Aiseee!!!
 
Kama hujui mambo kaa kimya.
Searching mirror, gareri , CCTV's zipo ofisi za umma kulingana na uhitaji wa usalama katika eneo husika.
Nenda central , wizara ya ulinzi, wizara yao mambo ya ndani utaanza kuheshimu walinzi na maaskari.
Mimi ukiandika nambari ya simu nikiwa na shaka nawe naipiga kama umedanganya nakupiga pingu.
Macho ya mlinzi ni zaidi ya bastola au CCTV camera.
Sawa kamanda
 
Tatizo ni usimamizi wa hilo KAUNTA BUKU kama walinzi wako makini. Kwa mahojiano na ukaguzi wa vitambulisho kwa kila anayeingia na kutoka heshima na thamani ya hicho kinachofanyika ingeonekana.
 
Sasa Babati hebu niambie kusaini pale kwenye kaunta buku kunasaidia kuzuia mtu mwenye nia mbaya? ndio maana mie nimewaza kuwa labda wanataka wapate idadi ya watu waliofika hapo siku hiyo.
Mkuu usiache kujaza vile vitabu, tena jaza majina yako kamili, ni muhimu. Kuna Jamaa ndio kilichomuokoa na mikono ya Pilato akanusurika kuingia korokoroni. Hiyo kesi alidai kuwa hakuwepo siku ya tukio na kusema kuwa alikuwa ofisi ya kampuni flani. Ushahidi uliomuokoa ni lile daftari mkuu.
 
Mkuu usiache kujaza vile vitabu, tena jaza majina yako kamili, ni muhimu. Kuna Jamaa ndio kilichomuokoa na mikono ya Pilato akanusurika kuingia korokoroni. Hiyo kesi alidai kuwa hakuwepo siku ya tukio na kusema kuwa alikuwa ofisi ya kampuni flani. Ushahidi uliomuokoa ni lile daftari mkuu.
Ahsante Mwarukuni ahsante sana
 
Vitu unavoona vidogo ndio huwa na umuhimu na msaada mkubwa sana kwenye maisha ya mwanadamu.
Uzuri wake huwa tunaandika jina na muda ulioingia na kutoka.

hii itakusaidia mahakamani kama utasingizia wizi wakati muda huo hukuwepo eneo la tukio

Majanga kama moto,tetemeko yakitokea itasaidia kutambua idadi na majina ya walio athirika.

bahati mbaya umefia chooni,au umepata tatizo la moyo itasaidia kutambua nn kinaendelea mana unavotoka lazima usaini tena

Inawasaidia ofisi kupata takwimu ya watu waliowahudumia iwe kwa siku wiki mwezi na mwaka pia kupunguza wahuni kuingia ingia ofisi za watu bila sababu za msingi.
 
Mfano kikitokea cha kutokea labda jengo likalipuka, inakuwa rahisi kujua nani na nani walikuwa ndani na hivyo ndugu wa waathirika kupata habari.
Mbona kanisani ,sokoni, msikitini nk hatuandiki, hakiwezi kutokea huko?chambua upya
 
Mfano kikitokea cha kutokea labda jengo likalipuka, inakuwa rahisi kujua nani na nani walikuwa ndani na hivyo ndugu wa waathirika kupata habari.
Kwani watajuaje kama jina nililoandika ni langu au wanaombaga na copy ya kitambulisho cha mpigakura.?
Labda wangekuwa wanaomba hata ka picha
 
Back
Top Bottom