Kurejea kwa Vitendo vya Uhalifu. Rais wangu Samia acha polisi wafanye kazi

Lord denning

JF-Expert Member
Jun 3, 2015
13,226
26,048
Hivi karibuni kumetokea kuongezeka kwa vitendo vya kihalifu hasa katika jiji la Dar es Salaam.

Leo hii kwenye taarifa ya habari imetangazwa kuwa wahalifu hawa wameua mtu mmoja eneo la Kawe.

Haya yanatokea kukiwa kumemalizika kikao cha wakuu wa polisi ambapo Rais Samia aliwaeleza mambo mengi sana polisi ikiwemo kuwaachia watu endapo upelelezi haujakamilika.

Leo kwa maslahi mapana ya nchi yangu napenda kumshauri Rais wangu mpendwa Samia kuwa, tunajua anapenda sana haki, anataka haki itendeke, ila kwenye kushughulikia wahalifu na uhalifu ni vizuri aviachie vyombo vyetu kufanya kazi ambayo wamekuwa wanaifanya kila siku katika kushughulikia wahalifu.

Kwa Tanzania yetu kuna watu bila kuwa ndani hawawezi kuacha uhalifu na wanawekwaga ndani kwa sababu maalum ikiwemo kuhakikisha kwenye jamii yetu kunakuwa na amani na utulivu. Ukitaka kuwaweka ndani ukiwa na ushahidi hutapata huo ushahidi kwa namna wanavyofanya matukio yao na kwa namna nchi yetu ilivyo nyuma kiteknolojia. Wenzetu wako vizuri kiteknolojia ikiwemo kuwa na kamera za mitaani na teknolojia ya DNA na database za wanachi wote ndo mana likitokea tukio upelelezi unakamilika haraka.

Nakuomba Rais wangu mpendwa, waachie polisi wetu wafanye kazi yao dhidi ya hawa wahalifu kulingana na mazingira yetu yalivyo. Kila nchi ina mazingira yake, Sio kwamba Marekani alishindwa kutawala Afghanistan ila kwa jinsi Afghanistan ilivyo nchi haiwezi kwenda bila utawala wa manguvu na ndo mana Leo Taliban karudi kutawala Afghanistan tena kwa baraka za Mmarekani yuleyule aliwafurusha pale mwanzoni
 
Hivi karibuni kumetokea kuongezeka kwa vitendo vya kihalifu hasa katika jiji la Dar es Salaam.

Leo hii kwenye taarifa ya habari imetangazwa kuwa wahalifu hawa wameua mtu mmoja eneo la Kawe.

Haya yanatokea kukiwa kumemalizika kikao cha wakuu wa polisi ambapo Rais Samia aliwaeleza mambo mengi sana polisi ikiwemo kuwaachia watu endapo upelelezi haujakamilika.

Leo kwa maslahi mapana ya nchi yangu napenda kumshauri Rais wangu mpendwa Samia kuwa, tunajua anapenda sana haki, anataka haki itendeke, ila kwenye kushughulikia wahalifu na uhalifu ni vizuri aviachie vyombo vyetu kufanya kazi ambayo wamekuwa wanaifanya kila siku katika kushughulikia wahalifu.

Kwa Tanzania yetu kuna watu bila kuwa ndani hawawezi kuacha uhalifu na wanawekwaga ndani kwa sababu maalum ikiwemo kuhakikisha kwenye jamii yetu kunakuwa na amani na utulivu. Ukitaka kuwaweka ndani ukiwa na ushahidi hutapata huo ushahidi kwa namna wanavyofanya matukio yao na kwa namna nchi yetu ilivyo nyuma kiteknolojia. Wenzetu wako vizuri kiteknolojia ikiwemo kuwa na kamera za mitaani na teknolojia ya DNA na database za wanachi wote ndo mana likitokea tukio upelelezi unakamilika haraka.

Nakuomba Rais wangu mpendwa, waachie polisi wetu wafanye kazi yao dhidi ya hawa wahalifu kulingana na mazingira yetu yalivyo. Kila nchi ina mazingira yake, Sio kwamba Marekani alishindwa kutawala Afghanistan ila kwa jinsi Afghanistan ilivyo nchi haiwezi kwenda bila utawala wa manguvu na ndo mana Leo Taliban karudi kutawala Afghanistan.
Kauli za Rais zinahusikaje na Polisi kushindwa kusimamia Usalama?

Hivyo nyie watu wa Dar mkiendelea kuwaficha hao watoto wenu mtakwisha,pia ni lazima muwe ma sungusungu na mfanye vikao vya kuwataja ila mnajifanyaga mko busy Sana na kusaka pesa.
 
Kauli za Rais zinahusikaje na Polisi kushindwa kusimamia Usalama?

Hivyo nyie watu wa Dar mkiendelea kuwaficha hao watoto wenu mtakwisha,pia ni lazima muwe ma sungusungu na mfanye vikao vya kuwataja ila mnajifanyaga mko busy Sana na kusaka pesa.
Kuna wahalifu wengi sana wako mtaani saivi kutokana na maelekezo ya upelelezi kukamilika ndo mtu kushikiliwa au kupelekwa mahakamani. Tunaishi mtaani tunawaona
 
Inasikitisha sana juzi hawa vijana wanaojiita panya road wamemuua kijana mmoja pale Buguruni kwa kumchoma kisu.
Mkuu wa Mkoa Mh Makala yupo kweli?
Hawa watoto ni kuwapoteza mazima ..inasikitisha sana...
 
Inasikitisha sana juzi hawa vijana wanaojiita panya road wamemuua kijana mmoja pale Buguruni kwa kumchoma kisu.
Mkuu wa Mkoa Mh Makala yupo kweli?
Hawa watoto ni kuwapoteza mazima ..inasikitisha sana...
Tusipokuwa makini nchi yetu inaweza kuwa kama Mexico au Colombia au Afrika ya kusini.

Kuna namna polisi wanadeal na wahalifu tuwaache tu. tukitaka wafanye tunavyotaka basi nchi yetu haitakalika asilani.
 
Leo kidogo naweza kuunga mkono. Ni ngumu sana hawa wakabaji wa mtaani ukawakuta na ushahidi. Ila mtaa mzima unamjua nani mwizi nani mkabaji. Kuthibitisha ni mkabaji ni ngumu sana maana akishakaba na kujeruhi anakimbia.

Kuna bwege mmoja alitusumbua sana alikuwa akiitwa Aron, kila akikamatwa anakaa baada ya muda anatoka kwa sababu hizohizo za kukosekana ushahidi wa kutosha. Ila ni mwizi na mkabaji aliyekubuhu tena hana huruma kabisa kwa kina mama
 
Tusipokuwa makini nchi yetu inaweza kuwa kama Mexico au Colombia au Afrika ya kusini.

Kuna namna polisi wanadeal na wahalifu tuwaache tu. tukitaka wafanye tunavyotaka basi nchi yetu haitakalika asilani.
Itakalika tu wala hilo ondoa shaka...
Nakuambia hawa watoto ni kuwafukia tu.....
Hii ndio dawa.
 
Ninyi watu wa Dar acheni ujinga. RC Chalamila wakati huo akiwa RC wa Mbeya aliwahi kusema kibaka anapokuvamia anakuwa amekusudia ama kukuua ama kuuawa.

Akatoa ushauri kwamba "jitahidi kupambana ili asikuue badala yake auawe yeye".

Wanaume wazima mnauawa na panya road? Inawezekanaje?

Mnashangaza kwa kweli. Acheni tabia ya kujichubua na kula chipis, haya mamabo waachieni wanawake. Acheni tabia ya kupakuliwa, haya mambo wachieni wanawake.

Mkiendelea kuna siku panya road wataisimamisha Dar kwa siku 3 nzima. Watazuia magari Mbezi Mwisho, Bunju B na Mbagala. Hakuna gari ya kutoka awala kuingia Dar, ni kipondo tu.
 
Kwani Samia kawazuia polisi wasifanye kazi?!
Maelekezo ya kutowashikilia watu upelelezi usipokamilika ndo matokeo yake haya

Moja ya mbinu za kufanya kusiwepo na uhalifu mitaani ni kukamata wahalifu na kuwaweka ndani kwa mda fulani. Hili Tanzania limesaidia sana kufanya mitaani kuwe na amani. Maana ukisema umkamate mtu ukishakamilisha upelelezi basi wahalifu wengi watazagaa mitaani na kuwazidi nguvu polisi maana polisi hawawezi kuwa kila mahali na kila wakati.
 
Ninyi watu wa Dar acheni ujinga. RC Chalamila wakati huo akiwa RC wa Mbeya aliwahi kusema kibaka anapokuvamia anakuwa amekusudia ama kukuua ama kuuawa.

Akatoa ushauri kwamba "jitahidi kupambana ili asikuue badala yake auawe yeye".

Wanaume wazima mnauawa na panya road? Inawezekanaje?

Mnashangaza kwa kweli. Acheni tabia ya kujichubua na kula chipis, haya mamabo waachieni wanawake. Acheni tabia ya kupakuliwa, haya mambo wachieni wanawake.

Mkiendelea kuna siku panya road wataisimamisha Dar kwa siku 3 nzima. Watazuia magari Mbezi Mwisho, Bunju B na Mbagala. Hakuna gari ya kutoka awala kuingia Dar, ni kipondo tu.
Nitake radhi. Mie nakaa Songea. Dar nina ndugu na marafiki
 
Back
Top Bottom