Unadhani wewe ndie mwenye kufikiri na kuwaza zaidi ya wanajamii wengi kutoka maeneo tofauti ya nchi hii?!
Ama wewe ndo mnadadavuaji kwa mifano ya vitabu na nadharia za kusadikika kutoka kwa maandiko ya watu kama wewe?!
Wale waliokulia katikati ya milio ya bundi na ndege kwijo ndio wanaeza kukupa mifano ya matukio ya aina hiyo mana njia nyingi zitumikazo huko vijijini ni nyembamba na si ajabu kukuta majani yamejiotea.
Kama umewahi kujikunguta umande ahsubuhi ama wakati wa mvua kuisha huwezi kosa majani aina ya (Kisokoro)yakiwa yametanda njiani kwa kusambaa chini.
Kuna mengi yapo huko vijijini kuliko ngano chache zilizofika mjini
Nachelea kusema utaona uzushi ikiwa tu hata mbuzi hujawahi kwenda mfunga kwenye majani,namaanisha kama hujawahi kuishi maisha yale ya ndani ya zi le jamii ambazo Radio tu ipo kwa mwenyekiti,sio hivi vijiji vilivyojaa taa za umeme.
zitto junior ,
hearly,
Da'Vinci