Kama umekulia mjini na ukaishi mjini haya mambo utayasikia tu kama ni ngano flani hivi za kizamani,ama ukifika vijijini ukakutana na haya mambo utasema ni kwa sababu watu wa huko hawajastarabika ila sivyo ilivyo haya mambo yapo na tunayaishi baadhi yetu hasa tuliozaliwa na kukulia vijijini na elimu zetu kupatia huko huko vijijini tena kwa kutembea km kadhaa tukiwa peku.
Kama umewahi kung'oa kucha kisa huna viatu ama umewahi kushonewa mfuko wa kitambaa wenye kamba moja tu kwa sindano ya mkono kisha ukautumia kubebea daftari,basi huwezi kubishana na hili kabisa.
Kweli watalamu ukiwafikia wanaeza kukwambia maelezo mengi ya vitabuni ila bado ukweli utabaki palepale ya kuwa kuna mazingira ukiyafikia lazima utaathirika kwa namna moja ama nyingine.
Mfano ni mimi mwenyewe nimeyaishi sana mazingira haya,tangu nakuwa hadi nabalehe na kuja mjini kuhangaika bado mambo hayo yalikuwapo,kupotea tulishapotea sana iwe usiku ama mchana.
Nakumbuka miaka ya nyuma kidogo tukiwa shule ya msingi tuliwahi kutoroka na kwenda kucheza kwenye pori la Mwitongo,yalipo makazi ya Nyerere na lengo lilikuwa ni kuona sehemu iliosadikika kuna makazi ya mizimu ya Nyerere na siku hiyo ilikuwa ni Alhamis ambayo wakazi wengi wa Butiama wanajua mzimu wa Nyerere hutoka kwenye makazi yake na kwenda kwa demu wake ambae nae ni mzimu yuko ng'ambo kidogo.
Hivyo tukalazimika kwenda siku hiyo ili kuona maajabu ya hilo eneo analoishi huyo mzimu
Tukiwa katikati ya msitu,nikiwa mbele mwenzangu nyuma,tukayavuka majani flani hivi na bila kujua tukazidi kwenda mbele,lakini azima yetu haikutimia na tukajikuta tukizunguka msitu bila uelekeo maalumu.
Baada ya jua kuzama,taarifa zikagfika kijijini ya kuwa tuliingia Mwitongo,hivyo wanakijiji wakaja kututafuta na tulikutwa yalipo mabaki ya ndege iliodondoka miaka kadhaa huko nyuma.
Mbali ya kuambiwa chanzo ni yale majani,lakini pia tukaambiwa mmoja kati yetu ni mtoto aliezaliwa pacha na sikuwa mimi alikuwa ni mwenzangu.
Tukaambiwa kwa kuwa ni wadogo mzimu umetuonea huruma mana hadi wakati unarudi sisi tulikuwa bado tunazurura mle.
Na kisa hiki ndo kilifanya Nyerere aombe kutuona (alikuwa bado yu hai)
Tulipelekwa na akatuuliza kwa nini tulienda msituni peke yetu?! Tukamwambia shida yetu na akatuchukua na kutupeleka hapo tulipohitaji kupaona.
Tukawa watoto wa kutolewa mfano kama sisi ni wajinga,wengine wakisema mashujaa na wengine wakiwaasa watoto wao wasituige sisi.
Huo ni mfano kati ya mifano mingi sana nilioshuhudia japo sehemu zingine hatukutakiwa kwenda na watoto waliozaliwa pacha ama wanawake waliomwezini ama kama umelala na mke wa mtu ama,umeiba cha mtu nk nk