Kupotea bila kujijua

Kupotea bila kujijua

hata mama namuuliza hapa anasema kipindi cha masika. na mvua iliwanyeshea masaa ma5 ,walitembea mpaka mto fulani watu Masasi wanaujua unaitwa Myesi
Kama ni ule mto Mhesi km kadhaa ukitoka tunduru basi nami naufahamu japo si mwenyeji wa huko
Mto huo wenyeji wanasema unatabia ya kuua mtu kila mwaka na kweli mmoja kati ya watu tuliokuwa kule tulikuwa tunautumia kuoga mana maji yalikuwa ni shida(ilikuwa kiangazi)mwenzetu mmoja akachotwa kiajabu na tukaja kumpata baada ya siku tatu,ikabidi na utafiti wetu tusitishe kabisa
Mwaka huu wameenda wengine tena
 
Ukijua sana muda mwingine ni matatizo, hivi unahisi alipagawa? Sikuwahi kumsikia kumtokea jambo hilo na lilitokea siku moja na halijamtokea tena. Kwenye hii dunia kuna mengine hutoyajua mpaka yakukute, naishia hapa.
Tatizo liko hapo unaposema "ukijua sana muda mwingine nitatizo".

Siombei iwe hivyo, lakini pengine mzee ana early onset Alzheimer or dementia. Haya ni magonjwa ya akiliyanayohusiana na utu uzima na ukiyawahi kuna dawa za kusaida kuyakabili/ kuyapunguza/ kuyasogeza yasidhuru sana mapema.

Ukisema "ukijua sana muda mwingine ni matatizo" unaweza kuwa sawa kulinganana mana yako, lakini unawezakuwa unalifumbia macho tatizo badala ya kujaribu kulitatua.

10 Early Signs and Symptoms of Alzheimer's
 
Tatizo liko hapo unaposema "ukijua sana muda mwingine nitatizo".

Siombei iwe hivyo, lakini pengine mzee ana early onset Alzheimer or dementia. Haya ni magonjwa ya akiliyanayohusiana na utu uzima na ukiyawahi kuna dawa za kusaida kuyakabili/ kuyapunguza/ kuyasogeza yasidhuru sana mapema.

Ukisema "ukijua sana muda mwingine ni matatizo" unaweza kuwa sawa kulinganana mana yako, lakini unawezakuwa unalifumbia macho tatizo badala ya kujaribu kulitatua.

10 Early Signs and Symptoms of Alzheimer's
Hizo ni perceptions zako tu hana tatizo lolote.
 
Unadhani wewe ndie mwenye kufikiri na kuwaza zaidi ya wanajamii wengi kutoka maeneo tofauti ya nchi hii?!

Ama wewe ndo mnadadavuaji kwa mifano ya vitabu na nadharia za kusadikika kutoka kwa maandiko ya watu kama wewe?!

Wale waliokulia katikati ya milio ya bundi na ndege kwijo ndio wanaeza kukupa mifano ya matukio ya aina hiyo mana njia nyingi zitumikazo huko vijijini ni nyembamba na si ajabu kukuta majani yamejiotea.

Kama umewahi kujikunguta umande ahsubuhi ama wakati wa mvua kuisha huwezi kosa majani aina ya (Kisokoro)yakiwa yametanda njiani kwa kusambaa chini.

Kuna mengi yapo huko vijijini kuliko ngano chache zilizofika mjini

Nachelea kusema utaona uzushi ikiwa tu hata mbuzi hujawahi kwenda mfunga kwenye majani,namaanisha kama hujawahi kuishi maisha yale ya ndani ya zile jamii ambazo Radio tu ipo kwa mwenyekiti,sio hivi vijiji vilivyojaa taa za umeme.

zitto junior ,hearly, Da'Vinci
Thibitisha habari zako, zaidi ya hapo huwezi kuepuka kuambiwa unaleta ngano tu.
 
Mi nilishawahi kupoteza baiskeli porini sikuiona kwa miaka minne mwaka wa tano nilikuja kuiona palepale haikuguswa wala kusogezwa mpk Leo siamini niliota au lakini ndio ukweli
 
Kwahiyo mkuu ulizurula si mchezo
emoji23.png
emoji23.png

Sasa hawa wanaopotea kutwa?
Yalikuwa masi
Hayo mambo yapo na yametokea sana vijijini huko;
Mvuha kuna kijiji kinaitwa magogoni 2005 kuna majamaa walikwenda kuwinda mbugani,wakat wanarud na mizigo yao ya nyama wakiwa jirani na kijiji wakatawanyika ili kupunguza msongamano wa watu maaana wakionekana watu kama10 harafu na mifurushi ya nyama watu watahamaki kidogo na km unavyojua maliasiri nao hawa chezi mbali.
Sasa ktk ule mtawanyo kwamb watakutana nyumban watu wamefika yule jmaaa bado hajafika,wakasubiria sana hawakumuona so ikabid watu walale kesho asubuh wakaanza kwenda kumfuatilia hawakufanikia walimtafuta kutwa nzima,wakarudi.
Siku ya pili inabid watafute ngoma ili wakipiga jamaa aweze kusikia walitoka pale saa kumi usiku jamaa walimkuta zaid ya km80,maaana walimkuta juu ya mti kabisa hata nguvu hana.
NB:HAYA MAMBO YAPO,ILA KWENYE USIBITISHO WA NN AMEKANYAGA HAPO HUONGELEKA VINGI,KUNA WANAOSEMA KUNA KADUDU UKIKAJAGA BAS NAWE UTATEMBEA TU,WENGINE HUSEMA MAJAN NA HATA WENGINE USEMA NDEGE,UKWELI WA SABABU HAMNA
Hata kwa sasa ukimgusa Jiwe tu utapotea hivyo hivyo, so inawezekana hayo utokea
 
Hizo ni perceptions zako tu hana tatizo lolote.
Hana tatizo lolote wakati kapotea kurudi kwake hivyo na so far tunaona hajafanyiwa hata tests za cognitive ability?

Are you in denial?
 
Kama umekulia mjini na ukaishi mjini haya mambo utayasikia tu kama ni ngano flani hivi za kizamani,ama ukifika vijijini ukakutana na haya mambo utasema ni kwa sababu watu wa huko hawajastarabika ila sivyo ilivyo haya mambo yapo na tunayaishi baadhi yetu hasa tuliozaliwa na kukulia vijijini na elimu zetu kupatia huko huko vijijini tena kwa kutembea km kadhaa tukiwa peku.

Kama umewahi kung'oa kucha kisa huna viatu ama umewahi kushonewa mfuko wa kitambaa wenye kamba moja tu kwa sindano ya mkono kisha ukautumia kubebea daftari,basi huwezi kubishana na hili kabisa.

Kweli watalamu ukiwafikia wanaeza kukwambia maelezo mengi ya vitabuni ila bado ukweli utabaki palepale ya kuwa kuna mazingira ukiyafikia lazima utaathirika kwa namna moja ama nyingine.

Mfano ni mimi mwenyewe nimeyaishi sana mazingira haya,tangu nakuwa hadi nabalehe na kuja mjini kuhangaika bado mambo hayo yalikuwapo,kupotea tulishapotea sana iwe usiku ama mchana.

Nakumbuka miaka ya nyuma kidogo tukiwa shule ya msingi tuliwahi kutoroka na kwenda kucheza kwenye pori la Mwitongo,yalipo makazi ya Nyerere na lengo lilikuwa ni kuona sehemu iliosadikika kuna makazi ya mizimu ya Nyerere na siku hiyo ilikuwa ni Alhamis ambayo wakazi wengi wa Butiama wanajua mzimu wa Nyerere hutoka kwenye makazi yake na kwenda kwa demu wake ambae nae ni mzimu yuko ng'ambo kidogo.

Hivyo tukalazimika kwenda siku hiyo ili kuona maajabu ya hilo eneo analoishi huyo mzimu

Tukiwa katikati ya msitu,nikiwa mbele mwenzangu nyuma,tukayavuka majani flani hivi na bila kujua tukazidi kwenda mbele,lakini azima yetu haikutimia na tukajikuta tukizunguka msitu bila uelekeo maalumu.

Baada ya jua kuzama,taarifa zikagfika kijijini ya kuwa tuliingia Mwitongo,hivyo wanakijiji wakaja kututafuta na tulikutwa yalipo mabaki ya ndege iliodondoka miaka kadhaa huko nyuma.

Mbali ya kuambiwa chanzo ni yale majani,lakini pia tukaambiwa mmoja kati yetu ni mtoto aliezaliwa pacha na sikuwa mimi alikuwa ni mwenzangu.

Tukaambiwa kwa kuwa ni wadogo mzimu umetuonea huruma mana hadi wakati unarudi sisi tulikuwa bado tunazurura mle.

Na kisa hiki ndo kilifanya Nyerere aombe kutuona (alikuwa bado yu hai)
Tulipelekwa na akatuuliza kwa nini tulienda msituni peke yetu?! Tukamwambia shida yetu na akatuchukua na kutupeleka hapo tulipohitaji kupaona.

Tukawa watoto wa kutolewa mfano kama sisi ni wajinga,wengine wakisema mashujaa na wengine wakiwaasa watoto wao wasituige sisi.

Huo ni mfano kati ya mifano mingi sana nilioshuhudia japo sehemu zingine hatukutakiwa kwenda na watoto waliozaliwa pacha ama wanawake waliomwezini ama kama umelala na mke wa mtu ama,umeiba cha mtu nk nk
Mzee baba tusilishane matango bana... Musoma kwetu pia
 
Hizi habari nyingine zinaweza kuwa ni myths ambazo zinahitaji uchambuzi wa kifasihi.

Naweza kukuambia

Mboga ni mazao.

Kuchuma mboga ni kutafuta mazao. It is no coincidence kwamba kuna style ya kufanya mapenzi inaitwa "chuma mboga". Kwa maana nyingine ya lugha ya tafsida kutafuta kuzaa.

Mwanamke ambaye yupo kwenye siku zake hizo, ukitaka kutafuta mtoto (mazao, mboga) wakati wa siku hizo, zitanyauka tu (mimba haitashika). Uwezekano wa mwanamke kupata mimba akiwa katika siku zake ni mdogo sana.

Kwa hiyo, inawezekana watu wanaongea kitafsida mwanamke aliye katika siku zake asichume mboga, zitanyauka.

Ukisoma moja kwa moja unapata maana tofauti.

Ukitafsiri ki myth na tafsida unapata tafsiri tofauti.

Inanikumbusha Kunta Kinte katika tamthiliya ya "Roots". Alikuwa anamlalamikia Fiddler kwamba hana mbegu ya kupanda apate mazao (nafikiri alikuwa ana miss maembe ya kwao Gambia).

Fiddler alivyo muhuni akatafsiri vingine kabisa. Akamwambia Kunta, weee kijana mdogo bado. Mbegu unazo nyingi. Tafuta mwanamke tu.

Huo ndio ukawa mwanzo wa Kunta Kinte kuoa.

Naonesha tu sehemu nyingine pale mazao ya kilimo yalipolinganishwa na mazao kwa maana ya watoto.

The good thing (or bad thing if you are a Paul Dirac) with myths is that they are subject to interpretation.

Nimetoka kumaliza kijitabu cha Claude Levi-Stauss "Myth and Meaning: Cracking the Code of Culture".

A very interesting perspective. Especially for a skeptic.
Safi sana, wengi tumeshindwa kufikiri nje ya box ila pia tu wavivu wa kusoma. Mpaka vijana wa le bado kila kitu wanakihusisha na mambo ya giza
 
Akili yako haiko sawa
Kumradhi, nia ya akili hii isiyo sawa ilikuwa kumtakia mema mzazi wako na kama kuna namna ya kumuagua mapema kabla pengine matatizo makubwa zaidi hayajamfika, itafutwe.

Lakini naona tunatoka dunia mbili tofauti.

Akili yangu haiko sawa katika dunia yako mkuu.

Kila la heri kwako wewe na familia yako.

Kwa heshima na taadhima.
 
Safi sana, wengi tumeshindwa kufikiri nje ya box ila pia tu wavivu wa kusoma. Mpaka vijana wa le bado kila kitu wanakihusisha na mambo ya giza
Vitu vingine ni Natural mkuu.
sio mambo ya giza wala sayansi.
Duniani kila kitu ni maajabu ila tu yanatofautiana. huoni ajabu kupanda mbegu ukaota mti ,sio mysterio hayo?
kwahiyo hayo mambo yapo ni natural ukifanya hiki kitatokea hiki, ndio maana kuna vitu vinaitwa najisi....
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom