OKW BOBAN SUNZU
Platinum Member
- Aug 24, 2011
- 49,206
- 103,778
Tunaendelea.....
Katika awamu ya 5 mambo mengi ya hovyo yalifichwa kupitia propaganda mfu za uzalendo. Watu wengi waliumizwa na kudhulumiwa. Kesi za uongo na kubambikiza zilikuwa za kufikia tu.
Tuliopewa macho ya kuona haya na wapenda haki tulipiga kelele ikaonekana tunakosa uzalendo. Tukasema aliyekuwa Rais wa Tz John Pombe anaumiza watu na hazingatii haki za binadamu. Hatukusikilizwa!
Lakini leo hii mambo yapo hadharani,vijana wanasema walitumwa na ngazi za juu.
Fikiria DC anaweza kutenda unyama wa kiwango hiki na mamlaka ya uteuzi ikakaa kimya tu. Unafikiri haikujua? Unafikiri hakupewa taarifa na vyombo vya usalama? DC anavamia watu na kupora mali waziwazi mkuu wa nchi yupo!
Fikiria huyo ni mteule tu, sasa mteuaji alikuwaje?
Kwa hiyo ndugu zangu mmepata picha kamili na rangi halisi ya JPM tukiyemlalamikia. Kila kitu kimekuwa hadharani kwamba Nchi iliendeshwa kwa mkono wa chuma.
Katika awamu ya 5 mambo mengi ya hovyo yalifichwa kupitia propaganda mfu za uzalendo. Watu wengi waliumizwa na kudhulumiwa. Kesi za uongo na kubambikiza zilikuwa za kufikia tu.
Tuliopewa macho ya kuona haya na wapenda haki tulipiga kelele ikaonekana tunakosa uzalendo. Tukasema aliyekuwa Rais wa Tz John Pombe anaumiza watu na hazingatii haki za binadamu. Hatukusikilizwa!
Lakini leo hii mambo yapo hadharani,vijana wanasema walitumwa na ngazi za juu.
Fikiria DC anaweza kutenda unyama wa kiwango hiki na mamlaka ya uteuzi ikakaa kimya tu. Unafikiri haikujua? Unafikiri hakupewa taarifa na vyombo vya usalama? DC anavamia watu na kupora mali waziwazi mkuu wa nchi yupo!
Fikiria huyo ni mteule tu, sasa mteuaji alikuwaje?
Kwa hiyo ndugu zangu mmepata picha kamili na rangi halisi ya JPM tukiyemlalamikia. Kila kitu kimekuwa hadharani kwamba Nchi iliendeshwa kwa mkono wa chuma.