Kuna wakati macho na masikio huwa yanatudanganya

OMOYOGWANE

JF-Expert Member
Dec 30, 2016
3,630
9,175
Kazi ya macho ni kuona, vile vile kazi ya masikio ni kusikia,
Lakini sio kila tunachokiona au kukisikia kina ukweli ndani yake,
Kuna wakati macho na masilio hutudanganya

mfano: unaweza kuona samaki yupo mtoni kwenye kina kifupi cha maji kumbe yupo chini ktk kina kirefu tofauti kabisa na unachokiona kwa macho yako
slide15-l.jpg

Wapo waliopoteza uhai kwa kupima kina cha maji kwa miguu, sababu kubwa ni kwamba macho yaliwadanganya,

unaweza kuona mtu anafanya biashara flani na anauza sana, basi nawewe haraka haraka ukaamua kufungua biashsra kama yake, baada ya miezi mitatu ukajikuta umefilisika au kupata hasara takatifu,


Kuna wakati mtu anaweza kukuambia biashara flani inalipa, basi nawewe ukaamua kuingia kichwa kichwa mwisho wa siku unajikuta umechezea za uso biashara imedoda,

Ukipita mjini utaona mji umejaa maduka ya kila aina, yapo miaka yote hayafilisiki basi nawewe ukaamua kujichanga ukafungua duka hapo hapo mjini mwisho wa siku unajikuta matumizi ni makubwa kuliko faida 😄 unaikimbia fremu hata kabla kodi haijaisha,

Sio kila unachokiona au kukisikia ndivyo kilivyo, kuna wakati macho na masikio huwa yanatudanganya.
Tunachokiona au kukisikia kinakuwa tofauti kabisa na uhalisia

Wakuu amini amini nawaambieni kuna biashara ni cover, biashara yenyewe haifanyikii hapo,
Tuwe makini, wenye kazi msikurupuke kuacha kazi mkakimbilia kujiajili bila kufanya utafiti kwa utulivu mkubwa.

Nawasilisha, povu ruksa.​
 
Ni kweli kuna muda macho huwa yanadanganya lakini ubongo unakataa kabisa kwamba hiki nilichoona sio kweli.

Mfano mapanga ya helicopter au ndege unakuta ipo hewani halafu yanazunguka taratibu. Macho yanatuma picha kwenye ubongo kwa yalichokiona, lakini ubongo unakataa unasema haiwezekani yakazunguka taratibu hivyo halafu ndege ikawa hewani.
 
Hivi kwa elimu yetu hii division na gpa kuna ambaye ataacha kazi akajiajiri kwa kujitoa muhanga? Inawezekana macho na masikio hudanganya hata kwenye nyanja zingine za kimaisha
 
Macho hayadanganyi mbona hayajawahi kudanganya ukilenga mbususu,
Isipokuwa kinachotokea Ni mbinuko ( curved) unaotokea hasa kwenye kioo na maji.
 
Uvivu wa kufikiria beyond nfio chanzo cha kufanya bongo zetu zikubaliane na kila inachokisia na kukiona
 
kwenye masikio !
mfano bwana x “we mpumbavu”
masikio yako yalivyo sikia “wewe”
 
Ni kweli kuna muda macho huwa yanadanganya lakini ubongo unakataa kabisa kwamba hiki nilichoona sio kweli.

Mfano mapanga ya helicopter au ndege unakuta ipo hewani halafu yanazunguka taratibu. Macho yanatuma picha kwenye ubongo kwa yalichokiona, lakini ubongo unakataa unasema haiwezekani yakazunguka taratibu hivyo halafu ndege ikawa hewani.
Mkuu kitu chochote kikiwa kwenye speed kali kuna wakati huwezi kukiona kabisa, mfano mapanga ya feni kabla hujaiwasha unayaona kirahisi, lakini ukiwasha feni ikaanza kuzunguka huyaoni vizuri ukiiongeza speed unaweza usione chochote

Hivyo hivyo upepo na mwanga hatuna uwezo wa kuviona kwa sababu vina speed kubwa
 
Kazi ya macho ni kuona, vile vile kazi ya masikio ni kusikia,
Lakini sio kila tunachokiona au kukisikia kina ukweli ndani yake,
Kuna wakati macho na masilio hutudanganya

mfano: unaweza kuona samaki yupo mtoni kwenye kina kifupi cha maji kumbe yupo chini ktk kina kirefu tofauti kabisa na unachokiona kwa macho yako
View attachment 1974508
Wapo waliopoteza uhai kwa kupima kina cha maji kwa miguu, sababu kubwa ni kwamba macho yaliwadanganya,

unaweza kuona mtu anafanya biashara flani na anauza sana, basi nawewe haraka haraka ukaamua kufungua biashsra kama yake, baada ya miezi mitatu ukajikuta umefilisika au kupata hasara takatifu,


Kuna wakati mtu anaweza kukuambia biashara flani inalipa, basi nawewe ukaamua kuingia kichwa kichwa mwisho wa siku unajikuta umechezea za uso biashara imedoda,

Ukipita mjini utaona mji umejaa maduka ya kila aina, yapo miaka yote hayafilisiki basi nawewe ukaamua kujichanga ukafungua duka hapo hapo mjini mwisho wa siku unajikuta matumizi ni makubwa kuliko faida 😄 unaikimbia fremu hata kabla kodi haijaisha,

Sio kila unachokiona au kukisikia ndivyo kilivyo, kuna wakati macho na masikio huwa yanatudanganya.
Tunachokiona au kukisikia kinakuwa tofauti kabisa na uhalisia

Wakuu amini amini nawaambieni kuna biashara ni cover, biashara yenyewe haifanyikii hapo,
Tuwe makini, wenye kazi msikurupuke kuacha kazi mkakimbilia kujiajili bila kufanya utafiti kwa utulivu mkubwa.

Nawasilisha, povu ruksa.​
Bora hata masikio,
Macho ni complete illusion ya kila kitu,
Hatuoni vitu jinsi vilivyo tunaona jinsi tulivo.
 
Kwenye bible, Thomaso hakuamini alichokiona kwa macho, ikabidi akampapase yesu kwa mikono ili awe na imani kuwa ndiye yule aliyemuona...

Ikiwa na ww unaona mapanga ya helikopta yanazunguka very slowly, nashauri ukaguse kwa mkono kama Thomaso.

Last but one, ishu ya biashara n ishu nene sana kiasi kwamba huwezi kujiaminisha kwa kile ukionacho kwa macho. Kijue nje ndani, ikiwezekana gusa (dadisi kwa kina) kabla ya kufanya maamuzi.

Lastly.............. Izingatieni paragraph ya mwisho ya mtoa uzi.... Tuwe makini, wenye kazi msikurupuke kuacha kazi mkakimbilia kujiajili bila kufanya utafiti kwa utulivu mkubwa
 
Back
Top Bottom