Malyenge
JF-Expert Member
- Jan 16, 2012
- 6,658
- 3,646
Wakuu naanza kwa kuwasalimu salaam.
Leo nimeonelea niwaletee hili swala la kanuni za somo la hisabati. Sitaongelea kanuni zote, bali nataka kuongelea kanuni moja tu ya kuzidisha. Kwa kawaida ukichua machungwa manane ukayazidisha mara mbili jibu utapata machungwa kumi na sita. nakadhalika na kadhalika.
Tatizo langu liko kwenye ile kanuni inayosema "namba yoyote ukizidisha kwa sifuri jibu ni sifuri...." Mfano una machungwa manane ukayazidisha na sifuri (yaani hukuyazidisha na idadi au kitu chochote) jibu (kwa mujibu wa kanuni hapo juu ni kuwa) hakuna machungwa!!!! Hii si kweli kwa akili za kawaida. Mimi nakubaliana na kanuni kwamba namba yoyote ukiiongeza na sifuri jibu ni namba yenyewe. Lakini kwa nini 8 (nane) ikizidishwa na 0 (sifuri) jibu lake liwe sifuri?? Ukiangalia kanuni ya hesabu za "logarithm" tunaona kwamba kinyume cha kuzidisha ni kujumlisha. Hivyo kwa kutumia kanuni ya logarithm (kinyume cha kujumlisha na kuzidisha), tunategemea ya kuwa 8x0= 8 kama ilivyo kwa 8+0= 8!!!
Nawaomba wanahisabati wote wale waliobobea na hata wale wa kawaida tujadili. Lengo ni kujaribu kuondoa dhana ya elimu inayotelewa hapa duniani kwa sasa. Kwamba kile elimu inachokifundisha kwa watu hapa duniani katika maisha ya kweli hakitumiki. Tuibadili dunia kutoka mtazamo wa sasa hadi ulimwengu wa uhalisia (real life). Nawasilisha.
Karibuni wakuu tuchangie.
Leo nimeonelea niwaletee hili swala la kanuni za somo la hisabati. Sitaongelea kanuni zote, bali nataka kuongelea kanuni moja tu ya kuzidisha. Kwa kawaida ukichua machungwa manane ukayazidisha mara mbili jibu utapata machungwa kumi na sita. nakadhalika na kadhalika.
Tatizo langu liko kwenye ile kanuni inayosema "namba yoyote ukizidisha kwa sifuri jibu ni sifuri...." Mfano una machungwa manane ukayazidisha na sifuri (yaani hukuyazidisha na idadi au kitu chochote) jibu (kwa mujibu wa kanuni hapo juu ni kuwa) hakuna machungwa!!!! Hii si kweli kwa akili za kawaida. Mimi nakubaliana na kanuni kwamba namba yoyote ukiiongeza na sifuri jibu ni namba yenyewe. Lakini kwa nini 8 (nane) ikizidishwa na 0 (sifuri) jibu lake liwe sifuri?? Ukiangalia kanuni ya hesabu za "logarithm" tunaona kwamba kinyume cha kuzidisha ni kujumlisha. Hivyo kwa kutumia kanuni ya logarithm (kinyume cha kujumlisha na kuzidisha), tunategemea ya kuwa 8x0= 8 kama ilivyo kwa 8+0= 8!!!
Nawaomba wanahisabati wote wale waliobobea na hata wale wa kawaida tujadili. Lengo ni kujaribu kuondoa dhana ya elimu inayotelewa hapa duniani kwa sasa. Kwamba kile elimu inachokifundisha kwa watu hapa duniani katika maisha ya kweli hakitumiki. Tuibadili dunia kutoka mtazamo wa sasa hadi ulimwengu wa uhalisia (real life). Nawasilisha.
Karibuni wakuu tuchangie.