Backagain Afterages
Senior Member
- Jan 23, 2017
- 151
- 118
usione ile timu ya chama imekaa kimya. huyu bwana anaweza kuwa raisi wa kwanza toka ccm kuongoza kwa miaka mitano tu. watu wamechoka nae ujuaji mwingi mno. yeye kajifanya mchumi mkuu wa serikali matokeo yake ndo hayo. ninaona njia mbadala za kuua rushwa, kuua ufisadi, kurudisha nidhamu nk bila ya kuathiri maisha ya kwa kiwango kilichopo sasa. sasahivi kila mtu analia. kulikoni? ninapata mashaka sana kuona watanzania wote wanalalamika hapo najua kweli hali sio nzuri. kama unarekebisha uchumi katika style ambayo sekta binafsi nayo inafifia badala ya kushamiri basi ujue haurekebishi uchumi bali unauua. huwa nashangaa anaposema viwanda wakati anaua mazingira vutivu ya viwanda. nani avutiwe kuwekeza wakati uwezo wa kununua wa wananchi hauvutii kuwekeza? kodi za ajabuajabu? bajeti iliyopangwa mwaka jana nasikia hadi sasa utekelezaji ni kichekesho ikiwa imebaki miezi mitatu tu ipangwe bajeti nyingine. tabu inaanzia kwenye ujuaji tu. gavana wewe, igp wewe, mwanasheria mkuu wa serikali wewe, everything you hapo mambo hayawezi kwenda.Kama anadhani atafanikiwa kwa style hii,bwana huyu nampa pole sana na ajue tu yote haya yanayoendelea kwa sasa ni "kete turufu" kwa upinzani na ni cancer inayoua taratibu chama chake.
Kiukweli kadri siku zinavyokwenda ndivyo wengi wanagundua hafai na wengi wanaacha kumuunga mkono na mwisho wa siku atabaki na supprt ya kikundi kidogo sana cha watu wanaomuunga mkono na hawa watakuwa ni wale wanaonufaika na uwepo wake na hata hao sio wote watakaokuwa wanafurahishwa na matendo yake bali ni katika kulinda tu vibarua vyao.
Yuko gizani na haoni kilicho mbele yake mpaka pale yatakapotimia kwakuwa hivi ndivyo ilivyopangwa kwamba kupitia yeye Taifa litakombolewe.
Usiniulize imeandikwa katika kitabu gani na ni katika mstari gani bali subiri kuona haya yakitimia.
Mungu ana makusudi na watu wake na ana njia nyingi anazotumia kufanikisha mipango yake kwa faida ya watu wake na njia nyingine huwa ni chungu zeenye taabu na mateso mengi kama tunavyoshuhudia sasa katika nyakati hizi za mpito.
Time will tell.