Kuna mtu anaiua CCM kwa speed ya rocket

Kuna mtu anaiua CCM kwa speed ya rocket

Napata maono ya vikosi vyote vya jeshi kuranda mitaani, vijana kuwekewa vikwazo vya kupiga kura, wazee na mahajuza kufatwa na usafiri kwenda kupiga kura, na mwisho baadhi ya wagombea wa upinzani kufikishwa mahakamani kwa tuhuma zisizo na mashiko. Tuombe uzima.

Halafu 2020 Magufuli atawagaragaza kwa kipigo cha mbwa mwizi mje tena hapa kulia lia kuwa mmeibiwa kura sisi hatuangalii sura hata agombee nani sisi ushindi tumezaliwa kushinda na si kushindwa iwe jua ama mvua ushindi lazima
 
Kama anadhani atafanikiwa kwa style hii,bwana huyu nampa pole sana na ajue tu yote haya yanayoendelea kwa sasa ni "kete turufu" kwa upinzani na ni cancer inayoua taratibu chama chake.

Kiukweli kadri siku zinavyokwenda ndivyo wengi wanagundua hafai na wengi wanaacha kumuunga mkono na mwisho wa siku atabaki na supprt ya kikundi kidogo sana cha watu wanaomuunga mkono na hawa watakuwa ni wale wanaonufaika na uwepo wake na hata hao sio wote watakaokuwa wanafurahishwa na matendo yake bali ni katika kulinda tu vibarua vyao.

Yuko gizani na haoni kilicho mbele yake mpaka pale yatakapotimia kwakuwa hivi ndivyo ilivyopangwa kwamba kupitia yeye Taifa litakombolewe.

Usiniulize imeandikwa katika kitabu gani na ni katika mstari gani bali subiri kuona haya yakitimia.

Mungu ana makusudi na watu wake na ana njia nyingi anazotumia kufanikisha mipango yake kwa faida ya watu wake na njia nyingine huwa ni chungu zeenye taabu na mateso mengi kama tunavyoshuhudia sasa katika nyakati hizi za mpito.

Time will tell.
Hivi wapinzani huwa mnakula nini mpaka mnawazi upuizi mlefu hivi.
Turufu ya Mh Magufuli na ccm ni uwepo wa Reli ya kisasa, kupungua kwa foleni Dar, Kuhamia Dodoma, Kuwa na shirika la ndege lenye faida., utumishi wa umma wenye nidhamu na uwajibikaji.
 
usione ile timu ya chama imekaa kimya. huyu bwana anaweza kuwa raisi wa kwanza toka ccm kuongoza kwa miaka mitano tu. watu wamechoka nae ujuaji mwingi mno. yeye kajifanya mchumi mkuu wa serikali matokeo yake ndo hayo. ninaona njia mbadala za kuua rushwa, kuua ufisadi, kurudisha nidhamu nk bila ya kuathiri maisha ya kwa kiwango kilichopo sasa. sasahivi kila mtu analia. kulikoni? ninapata mashaka sana kuona watanzania wote wanalalamika hapo najua kweli hali sio nzuri. kama unarekebisha uchumi katika style ambayo sekta binafsi nayo inafifia badala ya kushamiri basi ujue haurekebishi uchumi bali unauua. huwa nashangaa anaposema viwanda wakati anaua mazingira vutivu ya viwanda. nani avutiwe kuwekeza wakati uwezo wa kununua wa wananchi hauvutii kuwekeza? kodi za ajabuajabu? bajeti iliyopangwa mwaka jana nasikia hadi sasa utekelezaji ni kichekesho ikiwa imebaki miezi mitatu tu ipangwe bajeti nyingine. tabu inaanzia kwenye ujuaji tu. gavana wewe, igp wewe, mwanasheria mkuu wa serikali wewe, everything you hapo mambo hayawezi kwenda.
Sasa hivi yeye ndiye mweka hazina ,yeye ndiye bunge, ndiye kila kitu fedha za SERIKALI anazigawa apendavyo. Piga picha huu upinzani anapingana nao sasa ukifa.
TUTAKWENDA KUPIGA MAGOTI CHATO
 
CCM
(Chama Dola)
kujifananisha na CHADEMA ni sawa na nini?
"I wish I could be IGP"
 
CCM wanaujua upinzani wa kitanzania,wanajua nguvu na udhaifu wao matokeo yake mzigo unawaelemea wnanchi wa kawaida kwa kugeuzwa geuzwa na CCM kama chapati zilizo kosa mteja.CCm wanajua hata waboronge vipi wao wataendelea kuwa watawala wa nchi hii kwa kua upinzani nchi hii bado butu sana,
 
Bandiko lako lina makosa kibao ya ukosefu wa ithibati, makosa ya kimantiki na limejaa dhahania kibao
Ina maana hivyo ndivyo unavyojadili hoja ya mleta mada? Uvivu wa kusoma na kufikiri ni uvivu mbaya kuliko uvivu wa aina nyingine yoyote chini ya jua!
 
Hivi wapinzani huwa mnakula nini mpaka mnawazi upuizi mlefu hivi.
Turufu ya Mh Magufuli na ccm ni uwepo wa Reli ya kisasa, kupungua kwa foleni Dar, Kuhamia Dodoma, Kuwa na shirika la ndege lenye faida., utumishi wa umma wenye nidhamu na uwajibikaji.
Mko gizani na mmekosa maarifa na zaidi mmeshindwa kuelewa matatizo ya msingi yanayogusa moja kwa moja maisha ya watanzania wengi wa kawaida.
 
Kwa hiyo kama ccm inkufa wapinzani mnajipangaje kuchukua nchi.?
Kuendesha nchi hakuhitaji semina elekezi. Mbona Dikteta Malaika anapuyanga tu kivyake?
Tusipokuwa na Tume huru yeye anaweza kupeta lakini anguko kuu kupitia wabunge wengi wa CCM kuangukia pua halikwepeki na baada ya uchaguzi huo kutakuwa na kesi nyingi sana za kupinga matokeo ya ubunge hasa sehemu ambazo haki haitatendeke kuwabeba wabunge wa chama fulani watakaotaka kutumia wasimami wa uchaguzi kulazimisha ushindi.

Kesi za kupinga matokeo ya ubunge mwaka 2020 natabiri zitavunja rekodi.
 
Kuna mambo mawili yasiyo kosolewa la kwanza Mungu na la pili ni Kichaa.kichaa huwa akosolewi
 
Sasa hivi yeye ndiye mweka hazina ,yeye ndiye bunge, ndiye kila kitu fedha za SERIKALI anazigawa apendavyo. Piga picha huu upinzani anapingana nao sasa ukifa.
TUTAKWENDA KUPIGA MAGOTI CHATO
yani ni shida kubwa tena sana. na hamu yake ni kama upinzani ufe na kutokomea kabisa kusikojulikana. anajiona makini kumbe amejawa na substandards. kuna watu walisema kabla ya uchaguzi kuwa huyu bwana angefaa uwaziri mkuu na sio ukuu. walikuwa sahihi
 
Halafu 2020 Magufuli atawagaragaza kwa kipigo cha mbwa mwizi mje tena hapa kulia lia kuwa mmeibiwa kura sisi hatuangalii sura hata agombee nani sisi ushindi tumezaliwa kushinda na si kushindwa iwe jua ama mvua ushindi lazima
Wizi wa kura ni kawaida yenu.
 
Kama anadhani atafanikiwa kwa style hii,bwana huyu nampa pole sana na ajue tu yote haya yanayoendelea kwa sasa ni "kete turufu" kwa upinzani na ni cancer inayoua taratibu chama chake.

Kiukweli kadri siku zinavyokwenda ndivyo wengi wanagundua hafai na wengi wanaacha kumuunga mkono na mwisho wa siku atabaki na supprt ya kikundi kidogo sana cha watu wanaomuunga mkono na hawa watakuwa ni wale wanaonufaika na uwepo wake na hata hao sio wote watakaokuwa wanafurahishwa na matendo yake bali ni katika kulinda tu vibarua vyao.

Yuko gizani na haoni kilicho mbele yake mpaka pale yatakapotimia kwakuwa hivi ndivyo ilivyopangwa kwamba kupitia yeye Taifa litakombolewe.

Usiniulize imeandikwa katika kitabu gani na ni katika mstari gani bali subiri kuona haya yakitimia.

Mungu ana makusudi na watu wake na ana njia nyingi anazotumia kufanikisha mipango yake kwa faida ya watu wake na njia nyingine huwa ni chungu zeenye taabu na mateso mengi kama tunavyoshuhudia sasa katika nyakati hizi za mpito.

Time will tell.
ushahidi wa CCM kufa ni pamoja na kushinda kata 21 kati ya kata 22 za uchaguzi mdogo mwaka huu? hebu tupe dalili zaidi ya hii
 
Nazani wewe unaandika kutokana na unayosoma humu kwenye mitandao, nenda kwenye jamii huko, utaona vitu anavyofanya magufuli, nyie kuweni busy mahakamani na kwenye mitandao mwisho wa siku mtasema mmeibiwa.
Kazi anayofanya magufuli haijawahi tokea, na akibahatika kupata hela hadi 2020 upinzani hamtaenda tena kwa wananchi. Acheni kushinda humu tafuteni mbinu mpya.
Tutoke tukuache wewe unaware.
 
Na anaenda kubadili katiba ya chama chao akifanikiwa, atakuja kwenye katiba ya nchi yetu atafanya kama ya kina Kagame.... Yote haya yanatokea kwa sababu ya Paul Kagame ndio ametuletea ushauri wa kipuuzi kwa Faru joni wa chato
 
Acha
Na anaenda kubadili katiba ya chama chao akifanikiwa, atakuja kwenye katiba ya nchi yetu atafanya kama ya kina Kagame.... Yote haya yanatokea kwa sababu ya Paul Kagame ndio ametuletea ushauri wa kipuuzi kwa Faru joni wa chato
Acha hofe ndugu
 
Back
Top Bottom