Kuna michepuko ni takataka kabisa

Kuna michepuko ni takataka kabisa

Chagueni kutokua na michepuko maisha yanawezekana bila michepuko, hizo nguvu za kuhudumia mchepuko muhudumie mkeo au somesha hata ndugu yako uhisani uanzie kwenye chimbuko lako la karibu halafu uje uniambie kama Mungu hajakubariki maradufu na kizazi chako chote
 
Ni hivi,
Ijumaa baada ya kufunga duka nlkua nna ratiba ya kwenda kwake, ghafla nikapewa taarifa MKE wangu kakimbizwa ghafla hospitali, analalamika Tumbo linaamuuma sana.

Kanipigia kuniuliza "vipi mbona ufiki"
Nikamtaarifu sitoweza kuja kwako, niko njiani naelekea hospitali, mke wangu kakimbizwa ghafla. Nashangaa ananitumia sms za kipumbavu, nikaona asije niharibia Siku, nikapata ajali barabarani, sikuzijibu sms zake.


Baadae kanipigia Akisema "Sasa Ni pesa ya matumizi vipi, hamna chochote cha kupika uku? "

Nikamwambia "nenda Duka la mangi Apo jirani, akakupe vitu unavyohitaji vya kupika, nkija ntamlipa pesa yake". Baadae kanirudishia mrejesho kua kamkuta mkewe, kasema hakopeshi.

Nikamwambia, Basi tumia balance yako, nunulia vitu vyote vya kupika, utanipa hesabu Kisha ntaifidia nikija uko kwako. Kasema sawa.

Tangu juzi sijakwenda kwake wala kumpigia Simu, nmetuliza akili namuuguza wife kwanza.

Leo ananiuliza hivi namchukuliaje,
Hata Salam kuulizia tu mgojwa niliemtaarifu anaumwa kapelekwa hospitali ghafla anaendeleaje, hamna.

Anachoulizia direct Ni pesa zake za matumizi nilizoahidi ntafidia baada ya kuzitumia kugharamia chakula chake mwenyewe.

HUYU MWANAMKE HANA UTU, UBINADAMU WALA USTAARABU KABISA
uyo unamlaumu bure tu.

mkeo yy anamhusu nini bana ww?

hlf wanawake km hawa hawaachiki kirahisi, apo unalo kiongozi
 
Kwani mahusiano Ni biashara mkuu,
Kias kwamba aangalie maslahi yake TU?
Unapata huduma lipia huduma njia kuu na bora ni kujiepusha na michepuko haikusaidii mkuu zaidi inakupa stress ona na uzi unafungua kisa anataka kukamata miliki zako

Hii kitu inawezekana kaa mbali na michepuko ni kweli haina tija haina maana, chagua rafiki wakike awe best friend wako wa karibu mtakae weza kusaidiana katika mambo mengi ya kiushauri na kutenga muda wa kurefresh na asiweze kuwa mchepuko na mkaishi fresh tu na mkeo ukampenda zaidi.
 
For me naona jamaa ndio akili hana na huyo manzi anatumia udhaifu wake kama fimbo ya kumchampia
We ndo umesema ukweli, hilo jamaa halina akili hata moja kwasababu mambo ya kipumbavu anayaleta mitandani na screenshots juu, huyo mama J naona kama ana afadhali vile maana anajua libwana lake halina akili ndomaana analiendesha kama gari bovu, hebu tuma namba ya M-PESA nikuwekee soda
 
Si ubaki njia kuu na mkeo, sasa ya nini unahangaika na usioweza kuwahudumia on time ... ideally alikuwa anakupima aone ka una misimamo isiyotetereka......mihemuko
Mtakapo rejeana ukuje kutupa mrejesho
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom