DOKEZO Kuna mazingira ya rushwa kwa Askari wanaoomba kwenda Kozi

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
A

Anonymous

Guest
Nimeamua kuandika hapa kwa kuwa JamiiForums inafuatiliwa na watu wengi ndani na je ya Nchi, mtandao huu unafuatiliwa na watu wa kawaida, Viongozi na Watu wengine mashuhuri. Ningependa kuwaomba kwa unyenyekevu mkubwa kabisa andiko langu hili liende hewani.

Ikiwezekana andiko hili lifikisheni kwenye mitandao yenu ya Kijamii linalohusu malalamiko kwa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi hususani kwa Jeshi la Polisi.

Ipo hivi, mdogo wangu (naomba nisimtaje jina) ni Mtumishi wa Jeshi la Polisi ambaye amekuwa akiomba kusoma Shahada ya Sheria kwa miaka mitatu mfululizo akiwa ametimiza vigezo vyote ikiwa ni pamoja na Admission Letter ya chuo husika.

Viongozi wa Wilaya yake na Mkoa anaofanyia kazi wanampitishia maombi yake kuwa aruhusiwe kusoma lakini changamoto inakuja kwa watumishi wa Makao Makuu ya Polisi Dodoma Masjala ya Operation na Mafunzo.

Kitengo hicho kimsingizi ndiyo kinachohusika kupokea Maombi ya Askari wanaoomba kusoma Kozi mbalimbali, hupokelewa kisha kupelekwa kwa Kamishina wa Operation na Mafunzo kabla ya Kupelekwa kwa IGP ili kuidhinishwa.

Askari wa Masjala hiyo huwa wanahitaji kupewa kiasi kikubwa cha pesa angalau kuanzia Tsh. 300,000/= kwanza ndipo maombi yapelekwe kwa Viongozi wanaotakiwa kuyapitisha, kama mhusika hatatoa chochote kitu basi maombi hayo hutupwa au hata kuchomwa moto ilhali wengine wanaotuma pesa hizo huwa wanapata ruhusa za Masomo.

Hali hii inawavunja moyo Watumishi wa Jeshi hili na inapunguza Uaminifu kwa kuwa wanaombana Rushwa wao kwa wao lakini pia wanatenda kinyume na Sheria ukizingatia wanafanya kazi kwa Viapo vya Uaminifu na Utii.

Natanguliza shukrani zangu za dhati kwani naamini hii itawasaidia wengi ambao wameomba ruhusa za Masomo kwa Mwaka huu wa Masomo 2023/2024.
 
Hii kauli ya mkono mtupu haulambwi ....ni wa kiunyonyaji ila ndiyo hivyo inaitwa ahsante, shukurani,kipoozeo nk
 
Mwambie mdogo wako atoe hela (kama sio wewe) kwani watu wa makao hawana pa kula!! Nyie wa mikoani magendo nyingi sitaki kuzitaja kwani kila mtu anazijua
 
Nimeamua kuandika hapa kwa kuwa JamiiForums inafuatiliwa na watu wengi ndani na je ya Nchi, mtandao huu unafuatiliwa na watu wa kawaida, Viongozi na Watu wengine mashuhuri. Ningependa kuwaomba kwa unyenyekevu mkubwa kabisa andiko langu hili liende hewani.

Ikiwezekana andiko hili lifikisheni kwenye mitandao yenu ya Kijamii linalohusu malalamiko kwa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi hususani kwa Jeshi la Polisi.

Ipo hivi, mdogo wangu (naomba nisimtaje jina) ni Mtumishi wa Jeshi la Polisi ambaye amekuwa akiomba kusoma Shahada ya Sheria kwa miaka mitatu mfululizo akiwa ametimiza vigezo vyote ikiwa ni pamoja na Admission Letter ya chuo husika.

Viongozi wa Wilaya yake na Mkoa anaofanyia kazi wanampitishia maombi yake kuwa aruhusiwe kusoma lakini changamoto inakuja kwa watumishi wa Makao Makuu ya Polisi Dodoma Masjala ya Operation na Mafunzo.

Kitengo hicho kimsingizi ndiyo kinachohusika kupokea Maombi ya Askari wanaoomba kusoma Kozi mbalimbali, hupokelewa kisha kupelekwa kwa Kamishina wa Operation na Mafunzo kabla ya Kupelekwa kwa IGP ili kuidhinishwa.

Askari wa Masjala hiyo huwa wanahitaji kupewa kiasi kikubwa cha pesa angalau kuanzia Tsh. 300,000/= kwanza ndipo maombi yapelekwe kwa Viongozi wanaotakiwa kuyapitisha, kama mhusika hatatoa chochote kitu basi maombi hayo hutupwa au hata kuchomwa moto ilhali wengine wanaotuma pesa hizo huwa wanapata ruhusa za Masomo.

Hali hii inawavunja moyo Watumishi wa Jeshi hili na inapunguza Uaminifu kwa kuwa wanaombana Rushwa wao kwa wao lakini pia wanatenda kinyume na Sheria ukizingatia wanafanya kazi kwa Viapo vya Uaminifu na Utii.

Natanguliza shukrani zangu za dhati kwani naamini hii itawasaidia wengi ambao wameomba ruhusa za Masomo kwa Mwaka huu wa Masomo 2023/2024.
Mkono mtupu haulambwi, penye udhia penyeza rupia!!
 
Poti iyo ela ya chai.

Toa bila kuwaza,toa ya bia tukanywe bia malaika longe

Tuludi kiuhalisia kesi za majeshi hua hazi tatuliwi mitandaoni

Mnakanuni zenu na utaratibu wenu,tafuta njia ya kumfikia IGP personal mpelekee shida Yako kama unaona kurisk vilaki kazaa ni tatizo

Hata hivyo huko majeshini hua hampendi kupelekana shule maana wanajua ukiludi utatuzid vyeo
 
Hii nchi Kila sehemu inanuka rushwa sijui kazi ya mamlaka husika Nini kama tunao waamini ndio wachukua rushwa tumekosa uzalendo tumekosa utu
 
mwaka wa 3 anaomba kusoma anakataliwa sababu ikiwa ni ile ile,lakini anarudia kuomba kila mwaka akitegemea muujiza utatokea.

kwanza lazima ajue kwamba ruhusa ya kusoma inategemea zaidi ofa ya IGP na jopo lake yaani makao makuu,kwa kuzingatia mazingira ya kiutendaji,kwahiyo ruhusa itatolewa ikiwa tu jopo limeridhika kwamba kutoa ruhusa hakutaathiri utendaji kama malengo ya mwajiri yalivyopangwa,lakini pia unachokwenda kusomea kina uhitaji ama manufaa kwa taasisi zaidi na sio kwako binafsi,hivyo kuongeza elimu hiyo kunahesabika ni kama kutumwa na jeshi.

kama ana nia ya kweli ya kuongeza elimu inabidi ajisomee kwa muda wake wa ziada,kusubiri ruhusa sio jambo jepesi,na haitokei tu kirahisi maana unasimama kazi ukiendelea kulipwa na kuathiri utendaji wa taasisi,kwa kozi ya sheria inabidi awe mpore wasomi wa kada hiyo ni wengi.ingekuwa maswala ya hospital au uhandisi ingekuwa rahisi kiasi.
 
Back
Top Bottom