Arusha: Kero ya Rushwa ya Mdau yamfikia RPC; aapa kutowaonea haya Trafiki wala Rushwa. Je, kauli za maapizo zinatosha?

Lady Whistledown

JF-Expert Member
Aug 2, 2021
1,024
1,616
Akihitimisha Kikao cha Mafunzo yaliyotolewa na TAKUKURU ya kujiepusha na vitendo vya Rushwa vinavyoweza kusababisha kuchukuliwa hatua za kisheria kwa Askari wa Usalama Barabarani (Trafiki), Mkuu wa Jeshi la Polisi Mkoani humo ACP. Justine Masejo amesema baada ya Mafunzo hayo yeyote atakayebainika kujihusisha na Rushwa hatakuwa salama

Mafunzo hayo ni baada ya Mwananchi kulalamikia kukithiri kwa vitendo vya Rushwa miongoni mwa Askari wa Usalama Barabarani katika Jiji la Arusha na kutoa wito kwa RPC kufuatilia na kushughulikia changamoto hiyo

Mwananchi huyo alidai kuwa baadhi ya Askari wa Usalama Barabarani husimamisha Magari bila sababu za msingi kisha kuomba ‘kitu kidogo’ huku akiyataja maeneo ya Barabara ya Moshi Arusha, Barabara ya Monduli maeneo ya Shamsi, Barabara ya Njiro Maeneo ya Fire na Barabara ya Ngaramtoni kukithiri kwa changamoto hiyo

Madai ya Mdau haya hapa >>>> DOKEZO - RPC Arusha, tatua hii kero ya kuomba hela inayoshamiri kwa Trafiki
 
Akihitimisha Kikao cha Mafunzo yaliyotolewa na TAKUKURU ya kujiepusha na vitendo vya Rushwa vinavyoweza kusababisha kuchukuliwa hatua za kisheria kwa Askari wa Usalama Barabarani (Trafiki), Mkuu wa Jeshi la Polisi Mkoani humo ACP. Justine Masejo amesema baada ya Mafunzo hayo yeyote atakayebainika kujihusisha na Rushwa hatakuwa salama

Mafunzo hayo ni baada ya Mwananchi kulalamikia kukithiri kwa vitendo vya Rushwa miongoni mwa Askari wa Usalama Barabarani katika Jiji la Arusha na kutoa wito kwa RPC kufuatilia na kushughulikia changamoto hiyo

Mwananchi huyo alidai kuwa baadhi ya Askari wa Usalama Barabarani husimamisha Magari bila sababu za msingi kisha kuomba ‘kitu kidogo’ huku akiyataja maeneo ya Barabara ya Moshi Arusha, Barabara ya Monduli maeneo ya Shamsi, Barabara ya Njiro Maeneo ya Fire na Barabara ya Ngaramtoni kukithiri kwa changamoto hiyo
Hakuna lolote. Je, meno ya mbwa yanaweza kuumana??
 
Akihitimisha Kikao cha Mafunzo yaliyotolewa na TAKUKURU ya kujiepusha na vitendo vya Rushwa vinavyoweza kusababisha kuchukuliwa hatua za kisheria kwa Askari wa Usalama Barabarani (Trafiki), Mkuu wa Jeshi la Polisi Mkoani humo ACP. Justine Masejo amesema baada ya Mafunzo hayo yeyote atakayebainika kujihusisha na Rushwa hatakuwa salama

Mafunzo hayo ni baada ya Mwananchi kulalamikia kukithiri kwa vitendo vya Rushwa miongoni mwa Askari wa Usalama Barabarani katika Jiji la Arusha na kutoa wito kwa RPC kufuatilia na kushughulikia changamoto hiyo

Mwananchi huyo alidai kuwa baadhi ya Askari wa Usalama Barabarani husimamisha Magari bila sababu za msingi kisha kuomba ‘kitu kidogo’ huku akiyataja maeneo ya Barabara ya Moshi Arusha, Barabara ya Monduli maeneo ya Shamsi, Barabara ya Njiro Maeneo ya Fire na Barabara ya Ngaramtoni kukithiri kwa changamoto hiyo

Huko Arusha anasema kasikia na huku kwetu ushirombo inakuwa je sasa?
 
Sarakasi tu hizo wahuni wanasimamisha gari hilo hilo wiki nzima wanatafuta nini mpaka baadae anaona aibu unamwambia jana umelikagua leo unakagua nini tena au mnatafuta mabomu humu anabaki kucheka na kukwambia nenda tu si tupo kazini..
 
Ni mjinga tu ndo ataamini haya maneno,huyo RPC hadi kufika level hiyo kaua,katapeli na kudhurumu watu wengi sana,ni nadra sana kukutana na polisi mwadilifu
 
Yaani wananchi wanalalamikia rushwa. Badala ya kukamata na kuadhibu askari wahusika, inaitishwa semina na mafunzo, Wala rushwa wanalipwa posho, halafu warudi tena barabarani kuendelea kuomba rushwa. Makabati na meza za viongozi wa askari Wala rushwa zimejaa PGO, miongozo na code of conduct ya polisi, zimejaa vumbi, hazitumiki. Kule TAKUKURU nako Sheria za kushughulikia Wala rushwa ziko kabatini, hakuna mwenye uthubutu wa kuzitumia dhidi ya askari wala rushwa. .Hii nchi ngumu sana.
 
Things fall apart. Yaani yanayosemwa yangetekelezwa tungekuwa tuko nchi ya ahadi muda mrefu. Shida ni consume what we don't produce
 
Back
Top Bottom