Kuna kama mlipuko wa homa na mafua dsm

Kuna kama mlipuko wa homa na mafua dsm

Hivi mmeliona hilo?Kuna hali fulani kama mlipuko wa homa na mafuta kila mahali katika jiji la Dar es Sallam
Ni kweli kabisa mkuu, na hospitali zimefurika wagonjwa, jana nimeenda hospitali mbili hivi mmh!
 
Hivi mmeliona hilo?Kuna hali fulani kama mlipuko wa homa na mafuta kila mahali katika jiji la Dar es Sallam
Yako hapa yananipeleka less, yani hata nikigusa nywele zangu kichwa kinauma.
 
mbona kama yameanza mapema mno

kwani si tulikubaliana mafua ni mpk mwakani au
 
Ndio ngoma inarudi hio!! 3rd wave Omicron. Sema hii haitishi sana. Wameteleza kwenye formula.

Nakumbuka 2019 miezi ya mwishoni Kama hiihii zilikuja post kama hizi hizi humu JF kabla mamlaka zozote Afrika hazijajua chochote kuhusu Corona.


Nikiwa kama mtaalam wa magonjwa ambukizi niliona JF ilitisha sana na vyombo yetu vya ku monitor AFYA ya jamii ni vya hovyo kabisa.
Siyo DAR ES SALAMU tu bali ni Tanzania nzima,, mm hapa naenda wiki ya tatu nauma (CORONAVIRUS)
 
Mimi azuma niliacha nikameza antibiotics maana nilivokuwa Sina nguvu plus hyo azuma huchosha zaidi Sasa hivi nadunda ingawa nakunywa sana tangawizi nyingi kwenye chai na asali, nimeanza kufikiria tu kupata hyo chanjo ingawa kirusi kina change.
Aisee bora utulie kwanza dalili zote ziishe ndio ufikirie kuchanja, vinginevyo utaenda kujiletea matatizo, chanjo inaleta immune response na hicho unachoumwa kimeleta immune response ukizichanganya kiutani utani unaweza kujikuta upo ER
 
Ni kweli hata mimi nimeugua hyo Hali na kubanwa kifua na mafua makali, thank God nimepona nilivoenda hospital nilivokuta Kuna wagonjwa wanashindwa kupumua niligeuza nduki nika ghairi kupima kabisa.

[emoji1787][emoji1787][emoji1787] umenichekesha so haukutibiwa
 
Aisee bora utulie kwanza dalili zote ziishe ndio ufikirie kuchanja, vinginevyo utaenda kujiletea matatizo, chanjo inaleta immune response na hicho unachoumwa kimeleta immune response ukizichanganya kiutani utani unaweza kujikuta upo ER
Duh ndio sichanji naogopa sindano, ila muoga kweli
 
Kifo cha wengi harusi, nilijua niko peke yangu Sasa nimepona
 
Back
Top Bottom