Kuna kama mlipuko wa homa na mafua dsm

Kuna kama mlipuko wa homa na mafua dsm

Labda kama wewe ni mtoto mdogo umezaliwa miaka ya 2015 kuja mbele ila kama ni mtu mzima utajua kwamba kila mwaka kutokana na mabadiliko ya hali ya hewa huwa watu wanapatwa na homa za mara kwa mara ambazo homa huambatana na mafua.

Na pia ni kipindi kama hiki watu hupata maralia kwa zamu. Sasa msianze kutuletea story za Corona hapa as if hili ni swala geni.
 
Ni hatari, Mimi Hadi nilihisi kifo kimekaribia, joto la mwili lilikuwa juu Sana,na kichwa kuuma, yaan mpaka leo Bado mwili hauna nguvu kabisa
Yani mimi ilianza kuwa naskia joto flani la kuuzi nikanywa maji wee wapi, kufika mchana naanza kubanwa kifua, kichwa kinauma na mwili joto linazidi, nikameza Panadol huku nashindwa hata kuongea, aisee nimeteseka sana, mpaka nikapiga azuma ndio napona na ku sweti hatari, na mafua ya Sasa ni mabaya yana ambukiza Mimi mwenyewe ni mtu alikuwa na hyo Hali na tuko close naye sana
 
Hii ni taarifa kama taarifa nyingine , kama kuna mlipuko ndo tujue
Mafua ni moja ya dalili za korona kwa sasa ndo sababu watu wanakuwa concerned. Unless uniambie korona inauwa watu laini laini wa dar na sio nyie wababe wa mikoani.
Wana ubabe gani ?Wao ni fursa tu kwetu
 
Yani mimi ilianza kuwa naskia joto flani la kuuzi nikanywa maji wee wapi, kufika mchana naanza kubanwa kifua, kichwa kinauma na mwili joto linazidi, nikameza Panadol huku nashindwa hata kuongea, aisee nimeteseka sana, mpaka nikapiga azuma ndio napona na ku sweti hatari, na mafua ya Sasa ni mabaya yana ambukiza Mimi mwenyewe ni mtu alikuwa na hyo Hali na tuko close naye sana
Dah,ndio Hali niliyopitia Mimi au nnayopitia, hapa naendelea na Dozi ya Azuma,

Nimenunua matunda kibao kurudisha mwili kwenye hali yake
 
Yaani tumetishwa hadi tunasahau kuwa mafua yapo wakati wote na wanaougua mafua hadi wanashindwa kufanya kazi ni hao ngozi nyeupe kama ya kiti moto,sisi weusi mafua ni kitu cha kawaida sawa na kusikia joto au baridi.
 
Hivi mmeliona hilo?Kuna hali fulani kama mlipuko wa homa na mafuta kila mahali katika jiji la Dar es Sallam
Hasa kwenye ma office ya Serekali, Watumishi wengi sana Wana mafua au kikohozi, utawaona na vitambaa vyao na jinsi wanavyoongelea puwani! Mafuwa si mchezo,hasa yakiaamua kukubana!!

Sent from my TECNO KC8 using JamiiForums mobile app
 
Hiyo ni kila mwaka tangu 2015 ikifika December mpaka January kunakuwa na mlipuko wa homa ya mafua..wahanga wakubwa huwa ni wakazi wa Kimara Ubungo,sinza,Magomeni,Mwenge na maeneo mengine ya karibu
 
Dah,ndio Hali niliyopitia Mimi au nnayopitia, hapa naendelea na Dozi ya Azuma,

Nimenunua matunda kibao kurudisha mwili kwenye hali yake
Mimi azuma niliacha nikameza antibiotics maana nilivokuwa Sina nguvu plus hyo azuma huchosha zaidi Sasa hivi nadunda ingawa nakunywa sana tangawizi nyingi kwenye chai na asali, nimeanza kufikiria tu kupata hyo chanjo ingawa kirusi kina change.
 
Mimi nimeugua mafua makali sana na homa Alhamisi iliyopita ila sasa hali ni nzuri kiasi
 
Kweli na mimi hoi homa, kichwa na mafua makali tangu jumamosi. Yaani kchwa hakiskii panadol. Nashukuru naendelea vizuri.
 
dawa ni vaccination, mostly likely OMICRON ameishatia timu bongo.
Sasa ndg huyo Omicron anadhoofu kwa sindano ngapi au ipi, mchina, mrusi au mmarekani au zote tatu tudungwe tu !.

Maana baada ya huyo omi kuna wengine wengi bado wanakuja!.
 
composition ya vaccines zote kutoka huko ulipopataja, is almost the same, therefore booster is not created by mixing vaccines. This is my assumption
 
Back
Top Bottom