Kichuguu
Platinum Member
- Oct 11, 2006
- 18,035
- 25,031
udaktari wa slaa ni sawa na form 6....wa kutoa sacramenti....na kufungisha ndoa....hamna kitu hapa.....udaktari wa kikwete ni wa heshima baada ya kufanya ubunifu mwingi kwa maendeleo ya watanzania...
Hata phd ni reseach work tu.....sasa kama umefanya mengi kwa ubunifu basi unastahili phd...uelewa wake ni zaidi ya aliekwenda chuo kikuu.
Wacheni wivu...jamaa ni zaidi na zaidi
Swali kubwa hapa ni kuwa digrii hiyo imesomewa au imepikwa tu. Kuna madokta wa kupamba nyumba, madokta wa kupiga vinanda na kadhalika na wamesomea udokta wao na unatambulika. Hata kama Slaa kasomea udokta wa kufungisha ndoa na ikatambulika kitaalamu, basi huwezi kumlinganisha na mtu anayelala na kuamka kukuta kesho yeye ni dokta fulani bila kujua amefanya nini cha kuhalalisha udokta huo.
Nadhani kuwa Kenya wamewaona viongozi wetu kuwa ni so myopic kuwa ukiwapa jina la dokta fulani tu basi wanafungua mipaka ya nchi kwa makampuni ya Kenya kuvuna. Nilishangaa kusikia kuwa rais wa malawi naye alipewa hadhi ya profesa, na leo anaitwa profesa sijui nani, wachina wako huru nchini kwake. Sishangani kuwa Kenya wanaingilia Kampeini zetu kwa sababu Slaa kaonya kuwa jumuia bado muda wake na wanasiasa na wafanya biashara wa kenya hilo linawauma sana.